PAYE
JF-Expert Member
- Jun 19, 2025
- 354
- 395
Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Bukoba Vijijini kimetangaza matokeo ya uchaguzi wa kura za maoni ya wabunge wa Jimbo hilo ambapo aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Dkt. Jason Rweikiza ameongoza kwa kupata kura 6,465 huku mgombea mwenzake aliyekuwa mwenyekiti wa UVCCM, mkoani Kagera, Faris Buruhan akifuatia kwa kupata kura 4,619.
Akitangaza matokeo ya kura hizo usiku huu wa kuamkia Jumanne Agosti 5,2025 katibu wa CCM Wilaya ya Bukoba Vijijini mkoani Kagera,Jesca Ndyamkama amesema kura zilizopigwa ni 11,682 na kura 100 zimeharibika.
Amewataja wagombea wengine ni Fahami Juma(239),Asted Mpita(124),Edmundi Rutaraka(89),na Philebart Bagenda(44).
Faris,Baada ya kutangazwa matokeo hayo amepata nafasi ya kuongea na vyombo vya habari huku akitaja kutoridhishwa na matokeo hayo na kusema yaligubikwa na vitendo vya rushwa jambo lilompelekea kutosaini fomu za kukubaliana na matokeo, akisema kuwa tayari ameanza hatua za kupeleka malalamiko kwenye chama ngazi ya mkoa.
Amewataja wagombea wengine ni Fahami Juma(239),Asted Mpita(124),Edmundi Rutaraka(89),na Philebart Bagenda(44).
Faris,Baada ya kutangazwa matokeo hayo amepata nafasi ya kuongea na vyombo vya habari huku akitaja kutoridhishwa na matokeo hayo na kusema yaligubikwa na vitendo vya rushwa jambo lilompelekea kutosaini fomu za kukubaliana na matokeo, akisema kuwa tayari ameanza hatua za kupeleka malalamiko kwenye chama ngazi ya mkoa.