Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amesema chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, huduma za matibabu zimeimarika kutokana na kuboreshwa kwa hospitali za rufaa za mikoa.
Ameongeza kuwa ajenda kuu ya chama hicho ni kuendelea kuboresha huduma za afya kwa Watanzania.
Dkt. Nchimbi ameyasema hayo mjini Musoma wakati akipokea taarifa ya maendeleo ya mradi wa Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo Kata ya Kwangwa, ambapo amesema kuwa taarifa kuhusu idadi ya wagonjwa wanaotibiwa kutoka ndani na nje ya nchi zinaonyesha kuimarika kwa huduma za afya.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Katika hatua nyingine, amemuelekeza Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba, kuhakikisha ndani ya kipindi cha wiki mbili fedha kwa ajili ya ununuzi wa jenereta zinatolewa ili kuwezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika hospitalini hapo wakati wote.
Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere ilianza tangu awamu ya kwanza ya serikali.
Ameongeza kuwa ajenda kuu ya chama hicho ni kuendelea kuboresha huduma za afya kwa Watanzania.
Dkt. Nchimbi ameyasema hayo mjini Musoma wakati akipokea taarifa ya maendeleo ya mradi wa Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo Kata ya Kwangwa, ambapo amesema kuwa taarifa kuhusu idadi ya wagonjwa wanaotibiwa kutoka ndani na nje ya nchi zinaonyesha kuimarika kwa huduma za afya.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Katika hatua nyingine, amemuelekeza Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba, kuhakikisha ndani ya kipindi cha wiki mbili fedha kwa ajili ya ununuzi wa jenereta zinatolewa ili kuwezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika hospitalini hapo wakati wote.
Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere ilianza tangu awamu ya kwanza ya serikali.