Dkt. Mpango: Kodi si tatizo Bandarini

Kipenzi Changu

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
58,073
Reaction score
134,453
HATUA ya kupungua kwa mizigo inayotoka nje ya nchi kwenye Bandari ya Salama haitokani na ongezeko la kodi, anaadika Regina Mkonde.

Dk. Phillip Mpango, Waziri wa Fedha na Mpango amesema kuwa, pamoja na kuwepo kwa madai kwamba, mizigo kutoka nje ya nchi imepungua kutokana na ongezeko la kodi “kauli hii si ya kweli.”

Dk Mpango ametoa kauli hiyo leo katika mkutano wa uorodheshwaji wa hisa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Mpango amefafanua kuwa, kuyumba kwa soko la China ndiyo sababu ya mizigo hiyo kupungua kwa kuwa, Tanzania inashirikiana na nchi hiyo katika masuala ya kiuchumi.

“Muangalie uchumi wa China unavyokwenda, soko lake limepungua ulimwenguni, kutokana na sababu ya nchi kuwa na ushirikiano wa kiuchumi na china kumeathiri.

Kodi haiathiri chochote kile, na kelele zote zinazoendelea zinafanywa na wale wakwepa kulipa kodi.

“Waambie waache porojo, waende kwenye takwimu, hata kwa nchi jirani ya Kenya mizigo inayoingia imepungua kwenye Bandari ya Mombasa. Waende wakapate ripoti.”

Amesema kuwa, serikali ipo makini na wafanyabishara ambao hawataki kulipa kodi.

“Walipe kodi tu ili serikali iweze kuwahudumia, haiwezekani bandari itoe huduma kwa wafanyabiashara pasi na wao kulipa kodi, hapana.”
 
Magufuli kiboko nowdays watu wanafuatilia mizigo inayoingia bandarini na kodi inayopaswa kulipa.Awamu iliyopita umuhimu wa bandari haukujulikana hadi Kagame akatushangaa sana
 
Time will tell.
Je mizigo ya nchi jirani kama Zambia, Malawi, Rwanda, Burundi na Congo bado inapita kwa wingi kama zamani?

Je wale wanaoenda kuleta toothpicks na earbuds kule China bado wanaenda?
 
Ukweli wafanyabiashara hawapendi kulipa kodi, kama wameshindwa kufanya biashara hapa tanzania wapo huru kuondoka na kwenda kufunya nchi nyingine ambako watafanya ufisadi wao wa kutokulipa kodi.
😀😀😀😀😀😀 time will tell who is chinese na who is tanzania ?
 
Pengine hata angefafanua kwa nini sukari imepanda bei. Hilo la bandarini mimi sina tatizo nalo.
 
Sasa mkuu Dr Mpango kama shida ni china mbona hata magari yanayotoka Japan nayo yamekauka ?
 
Leo hakuna wakuhoji sukari kwanini imepanda bei na tulihakikishiwa malighafi hiyo itashuka bei hadi 1800! Ngoja tusubiri maana wao wamekuwa wazee wa kubadili gia hewani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…