Kamanda Asiyechoka
JF-Expert Member
- Sep 13, 2020
- 3,164
- 4,581
Anapokuwa kwenye majukwaa anakudanganya kuwa wananchi wamekuja kusherehekea utekelezaji wa ilani ya Ccm. Ukweli ni kuwa nusu ya hivyo viwawanja ni watoto wadogo. Na wanakuja kuangalia wasanii ambao umetumia gharama nyingi kuwakodi na kuwasafirisha.
Gharama ambazo kama ungetumia wasanii wa mikoa unayofanya kampeni zisingekuwa kubwa kama hivyo.
Pili huyu mwenezi wa sasa wa CCM hakuambii ukweli kuwa wanachi wanamagumu na mioyo yao imejaa huzuni. Mara baada ya midundo ya wanamziki kama Harmonize, Diamond au Snura wakimaliza kutumbuiza, hawa wanachi hurudi makwao na huko hukuta hali mbaya.
Maana hata hapo uwanjani huwa hamuwapatii chakula.
Hao wananchi kama wangepata nafasi ya kukujoji mh rais wangekuuuliza, mbona unanunua midege wakati hata maeneo mengi hayana maji? Kwa hiyo ili Polepole asikudanganye uwe unaruhusu swali hata moja toka kwa wananchi ndio utajua midege na miradi mingine mikubwa haikuwa na tija kwa sasa wakati wananchi wanashida.
Mwananchi kama huyu anakuuliza ndege 11 za nini wakati hata maji haujasambaza sehemu nyingi tu Tanzania? Toa nafasi ili uulizwe maswali kwenye mikutano yako.
Gharama ambazo kama ungetumia wasanii wa mikoa unayofanya kampeni zisingekuwa kubwa kama hivyo.
Pili huyu mwenezi wa sasa wa CCM hakuambii ukweli kuwa wanachi wanamagumu na mioyo yao imejaa huzuni. Mara baada ya midundo ya wanamziki kama Harmonize, Diamond au Snura wakimaliza kutumbuiza, hawa wanachi hurudi makwao na huko hukuta hali mbaya.
Maana hata hapo uwanjani huwa hamuwapatii chakula.
Hao wananchi kama wangepata nafasi ya kukujoji mh rais wangekuuuliza, mbona unanunua midege wakati hata maeneo mengi hayana maji? Kwa hiyo ili Polepole asikudanganye uwe unaruhusu swali hata moja toka kwa wananchi ndio utajua midege na miradi mingine mikubwa haikuwa na tija kwa sasa wakati wananchi wanashida.
Mwananchi kama huyu anakuuliza ndege 11 za nini wakati hata maji haujasambaza sehemu nyingi tu Tanzania? Toa nafasi ili uulizwe maswali kwenye mikutano yako.