Dkt. Louis Shika aeleza Magumu aliyopitia hadi akatoroka Urusi. Alitekwa na kukatwa Vidole, Tanzania ilimtelekeza...

Jina lenyewe la Dr LOUS SHIKA siyo lake, jina lake halisi ni Lunyalula Kidola, hela anazosema anazo siyo kweli hana hizo hela. Shika ni mwongo na kichwani hayuko vizuri, Mimi huyo shika namfahamu tangu mwaka 1977alikuwa anasoma chuo cha waganga wasaidizi Mbeya.
 
kuna lecture mmoja pale chuo cha uhasibu Arusha(IAA) anafundisha hesabu nae alisomea urusi mambo nuclear na inasemekana aliishi mda mrefu sana urusi.ukimuona au hata ukiongea nae unaona dish kidogo limecheza ila class yuko vizuri sana.ana stor nyingi sana za urusi tena hawependi warusi kinyama na yy sijui walimfanya nn
Mrussia au mashauri mwalimu wangu wa business maths
 
Kwanza tuanze na kukanyana kwa unafiki,
Inaonekana mzee Shika siyo mwendawazimu kama watu walivyosambaza ujumbe kwamba ni mbovu wa akili,

Wengine wakasema hana nyumba anadaiwa kodi, kumbe watanzania unafiki tutauacha lini?

MAELEZO YAKE NIMEYAWEKA KWA KIFUPI

Katika mahojiano na kituo kimoja ameeleza yafuatayo
1. Anadai ana nia bado ya kununua nyumba za Lugumi

2. Alitekwa nchini Russia na kuteswa na warusi kwa kutaka awape hela na kumkata vidole kama anavyoonesha kwenye video

3. Aliwekwa ndani ya andaki kwa siku 28 na vijana wahuni wa urusi bila majirani zake kujua alipo na kujua atapatikana wapi, baadae akatumia mbinu mbadala kuwatoroka baada ya wao kulewa sana,

4. Alipopelekwa hospitali alitembelewa na ubalozi wa marekani, lakini ubalozi wa Tanzania ulimtelekeza.

Hapa nakubaliana na Shika, huku Urusi kuishi kwa wasiwasi sana kwa kifupi SISI HUKU NI NYANI, NAITWA NYANI na incidence kama hii imenikuta nilipotembelea SARATOV mwaka 2016 nilihisi mazingira ya sintofahamu, Mpaka nilipo rudi kazini kwangu ST PETERSBERG.

Hebu pitia video yake, weka bando la kutosha upitie,


Dar es Salaam. Dk Louis Shika ‘bilionea’ aliyejitokeza kununua majumba ya kifahari ya mfanyabiashara maarufu Said Lugumi ameelezea siku 28 za mateso aliyodai kuyapata baada ya kutekwa nyara nchini Urusi miaka 13 iliyopita.

Dk Shika, ambaye jana aliachiwa kwa dhamana na polisi amesema haikuwa rahisi kujinasua kwa sababu alipata mateso makali na alijua ndiyo mwisho wa maisha yake, lakini kwa uhodari na nguvu za Mungu alifanikiwa kutoroka kutoka mikononi mwa watekaji hao.

Hata hivyo aliendelea kusisitiza kuwa mpango wake wa kununua nyumba za Lugumi haujabadilika na kwamba ataishangaza dunia.

Alisema hayo jana jioni katika mahojiano maalumu na Mwananchi nyumbani kwake Tabata Mawenzi baada ya kurejea kutoka mahabusu ya Kituo Kikuu cha Polisi alikoshikiliwa kwa siku sita akituhumiwa kuvuruga mnada huku leo akitakiwa kuripoti kituoni hapo saa tatu asubuhi.

Dk Shika, ambaye alidai kuwa alikwenda Urusi kwa masomo na baadaye kufanya kazi nchini humo alisimulia kuwa alitekwa na watu wasiojulikana Juni mwaka 2004 huku ‘watekaji’ wakimtaka awape Dola1.5 milioni za Marekani (Sh3 bilioni kwa sasa) ambazo hakuwa tayari kuzitoa licha ya kuwa na uwezo wa kuwapa.

“Nilipokamatwa walinipeleka sehemu huku nikipigwa, nikiteswa kwa siku 28 na nilijua ndio itakuwa kifo changu. Nilipigwa ngumi, niliteswa vikali, walitumia nyaya za umeme kunitesa, walinikata vidole kimoja kwa nyundo na viwili kwa panga, yote wakitaka niwape dola milioni moja na nusu,” alisema Dk Shika, ambaye mwandishi wa habari hizi alishuhudia kuona mkono wake wa kushoto ukiwa umekatwa vidole viwili na kidole kimoja mkono wa kulia.

“Sikuwa tayari kutoa, uwezo huo nilikuwa nao, siku 28 zilikuwa ngumu kwani chakula nilikula kile ambacho walibakiza wao, mwili wangu ulijaa damu, wale Warusi walinitesa sana kwani hata sikio langu (la kushoto, anamuonyesha mwandishi) limebondwabondwa, ni tofauti na hili la kulia hadi nafika Tanzania ni Mungu pekee anajua.”

Dk Shika alisema mateso hayo yalimsababishia maumivu makali ikiwamo kuvunjika mbavu tatu upande wa kulia na mbili kushoto ambazo bado hazijaunga vizuri.

Aliuhusisha mkakati wa kumteka na mmoja wa wafanyakazi katika kampuni yake aliyodai inaitwa Ralcefort ili kujipatia kiasi hicho cha fedha, lakini hawakufanikiwa baada ya kuwazidi ujanja na kutoroka.

Mwananchi lilipotaka kujua alitumia mbinu gani kutoroka ikiwa alikuwa hana nguvu na ndani ya jumba asiloweza kujua mlango ulipo, Dk Shika alidai, “ilikuwa siku moja wale watu walitoka na kumwacha mwenzao, akaanza kunywa pombe aina ya vodka na kujidunga unga, mimi nilipoona hivyo wakati huo nimefungiwa katika pipa la maji nilianza kufikiria mbinu za kumtoka.”

“Nilimhesabia tu muda, kuna muda ulifika nikamwona amelala na kwa kawaida mtu akilala ukimwangalia usoni anaweza kuamka, kwa hiyo mimi nikalibinua lile pipa na nikatoka, kule nje nilipotoka nilikutana na binti ambaye hakunisaidia.”

Dk Shika, ambaye huongea kwa kujiamini alisema baada ya kutoroka alipata msaada kutoka kwa wasamaria wema ambao walimchukua na kumpatia huduma ya kwanza wakati huo mwili wake ukiwa umeloa damu.

Alisema watu waliomsaidia walitaka awapeleke eneo alipotekwa, lakini siku ya kwanza hawakufanikiwa kwa sababu alikuwa hapajui vizuri ila siku ya pili walifanikiwa kupaona.

“Tulipofika mle ndani tulikuta damu imetapakaa chumba chote, kumbe wale watu walimuua yule mwenzao niliyemtoroka baada ya kudhani nilimpa fedha ili aniachie, wakadhani amewasaliti.

Kuhusu familia yake kumtenga kama alivyosema kaka yake anayeitwa Pelanya Lunyalula (84), katika mahojiano na Mwananchi, Dk Shika alisema, “mawasiliano mabaya, kama hatuwasiliani ni ukosefu wa mawasiliano, yawezekana mwenzangu akawa hana simu, sasa tutawasilianaje na sidhani kama nitakwenda (Simiyu) kwani kama wazazi wamekufa hata nikienda haitasaidia. Sasa ninachokiangalia ni kumaliza kwanza hili la kuzipata nyumba zangu.”

“Siku nikipeleka fedha nataka Yono (Kampuni ya Udalali iliyoendesha mnada huo) na TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) waite waandishi wa habari waone na wautangazie umma,” alisema kwa kujiamini.

Polisi wamwachia kwa dhamana

Awali, kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa alilieleza Mwananchi kuwa wamemwachia Dk Shika kwa kujidhamini mwenyewe baada ya kukosa mtu wa kumdhamini ila atakuwa akiripoti kila siku saa tatu asubuhi.

“Uchunguzi wa tuhuma dhidi yake unaendelea, lakini mpaka sasa hakuna mtu aliyefika kutaka kumuwekea dhamana, anaishi kama mtu wa nyikani. Nimeagiza watendaji wangu wamwachie kwa dhamana ajidhamini yeye mwenyewe na awe anakuja kuripoti kila siku,” alisema.

Njiani wakati akielekea kituo cha daladala cha Mnazi Mmoja baada ya kuachiwa na polisi, Dk Shika alikuwa kivutio kwa watu aliokuwa akipishana nao.

Hata allipopanda daladala la kwenda Tabata Mawenzi, kondakta alimkaribisha kwa kumweleza, “karibu mzee Shika”, huku ndani ya gari hilo watu wakipiga naye picha na alipowasili nyumbani kwake aligonga geti na kujitambulisha “choka mbaya bin mlalahoi” jambo lililowafurahisha waliojitokeza kumpokea.

Chanzo: Mwananchi

*R.I.P DR. SHIKA😭*

Dr.Shika alikuwa ni miongoni mwa wasomi wazuri lakini bahati mbaya elimu yake haijaweza kusaidia taifa hili achilia mbali kumsaidia yeye binafsi.

Wengi walimchukulia kimzaha tangu alipoonekana kwenye tukio la mnada wa nyumba za Lugumi (mia tisa itapendeza). Makampuni ya kibiashara yalitumia umaarufu wake kama fursa ya matangazo lakini yakamuacha hohehahe asiye hata na mahali rasmi pa kuishi. Aliwahi kuripotiwa na kituo kimoja cha TV kufukuzwa kwenye nyumba aliyokua akiishi huko Tabata baada ya kushindwa kulipia kodi.

Vyombo vingi vya habari vilikuwa vikimdhihaki na vingine kumuita Kalubandika. Lakini bila shaka vilifanya hivyo pasipo kumjua kiundani *Dr.Shika.*

Ni mzaliwa wa kijiji cha Kalemela wilaya ya Busega, mkoani Simiyu. Majina yake halisi ni Louis Shika Kidola. Yeye na ndugu yake Jeremiah Shika Kidola *(marehemu pia)* walikuwa wanafunzi wenye akili sana na waliofaulu vizuri masomo yao ya sekondari kwa alama za juu na kupata ufadhili wa kusoma udaktari nchini Urusi mwaka 1984 hadi 1991 waliporejea na kuanza kutibu hospitali ya taifa Muhimbili.

Mwaka 1994 Louis Shika alirejea Urusi kujiendeleza kimasomo. Alisomea shahada ya uzamili katika magonjwa ya kuambukiza (MSc in Infectious Diseases) na udaktari bingwa wa magonjwa ya akili Master of Medicine (Psychiatry). Akiwa huko alishirikiana na wenzake kuanzisha kampuni ya usambazaji wa kemikali viwandani iitwayo Lancefort Ltd.

Kwa sasa ni moja ya makampuni makubwa ya usambazaji wa kemikali nchini Urusi, na jina la Dr.Shika lipo kwenye website yao kama Muasisi na Rais wa kwanza wa kampuni.

Inadaiwa shirika la ujasusi la Urusi (KGB) liligundua kwamba akina Shika walipata fedha za kuanzisha kampuni kutoka Marekani kama mkakati wa Marekani kudukua taarifa za Urusi. Kwahiyo baadhi ya viongozi wa kampuni hiyo walikamatwa. Dr.Shika alitekwa na watu waliodhaniwa kuwa majambazi kupewa mateso makali sana ikiwemo kukatwa vidole.

Balozi wa zamani wa Tanzania nchini Urusi, Patrick Chokala mwaka 2017 alinukuliwa na vyombo vya habari kwamba ilibidi kutumia mbinu za "kijasusi" kumnasua Dr.Shika na kumrudisha nchini kwa dharura. Tangu aliporejea alijiingiza kwenye ulevi wa kupindukia kutokana na msongo wa mawazo.

Kwahiyo ukifuatilia historia ya *Marehemu Dr.Shika* utagundua hakuwa "kalubandika" kama ilivyodhaniwa. Ni mtu aliyekua na maono makubwa. Kama si mipango yake kuvurugika huenda angekuwa daktari bingwa na mfanyabiashara mkubwa wa kemikali duniani.

Ni kwamba tu alijikwaa, akadondoka na hakuweza kusimama tena. Serikali ilipaswa kumsaidia kusimama lakini nayo ilimtelekeza. Kwahiyo ameishi maisha ya upweke, masononeko na msongo wa mawazo kwa muda mrefu.

Kampuni aliyoanzisha ya Lancefort Ltd ambayo kwa sasa inamilikiwa na serikali ya Urusi (ilitaifishwa) ina thamani ya $27Bil sawa na TZS 60Trilioni (Bajeti ya nchi kwa miaka miwili).
_
Kwa hiyo Dr.Shika alikuwa anajiita "Bilionea" si kwamba alikuwa anaota. He used to have money. Na hiki ndicho kilichokuwa kinamtesa maana alishindwa kukubaliana na hali yake ya sasa. Hakutaka kuamini kama aliwahi kuwa na pesa.

Kujikwaa na kuanguka ni kawaida katika maisha lakini jambo la msingi ni uwezo wa kusimama tena baada ya kuanguka. Whinston Churchil aliwahi kusema "Success is not final and failure is not fatal. It is the courage to continue that counts"
_
Mtu kama huyo hakuwa mtu wa "kumchukulia poa" hata kidogo. Serikali haikutakiwa kumtelekeza. Alipaswa kupewa nafasi nyingine. Either angerudishwa Muhimbili kutibu au angetafutiwa fursa mahali pengine ambapo taifa lingeweza kufaidi ujuzi wake na pia ingekua njia ya kumsaidia kuondokana na msongo wa mawazo na kusahau "mabilioni" yake kule Urusi.

*Pumzika kwa amani Mr. mia tisa itapendeza*

C&P from WhatsApp group.

RIP Dr. Louis Shika.

P
 
*R.I.P DR. SHIKA😭*

Dr.Shika alikuwa ni miongoni mwa wasomi wazuri lakini bahati mbaya elimu yake haijaweza kusaidia taifa hili achilia mbali kumsaidia yeye binafsi.

Wengi walimchukulia kimzaha tangu alipoonekana kwenye tukio la mnada wa nyumba za Lugumi (mia tisa itapendeza). Makampuni ya kibiashara yalitumia umaarufu wake kama fursa ya matangazo lakini yakamuacha hohehahe asiye hata na mahali rasmi pa kuishi. Aliwahi kuripotiwa na kituo kimoja cha TV kufukuzwa kwenye nyumba aliyokua akiishi huko Tabata baada ya kushindwa kulipia kodi.

Vyombo vingi vya habari vilikuwa vikimdhihaki na vingine kumuita Kalubandika. Lakini bila shaka vilifanya hivyo pasipo kumjua kiundani *Dr.Shika.*

Ni mzaliwa wa kijiji cha Kalemela wilaya ya Busega, mkoani Simiyu. Majina yake halisi ni Louis Shika Kidola. Yeye na ndugu yake Jeremiah Shika Kidola *(marehemu pia)* walikuwa wanafunzi wenye akili sana na waliofaulu vizuri masomo yao ya sekondari kwa alama za juu na kupata ufadhili wa kusoma udaktari nchini Urusi mwaka 1984 hadi 1991 waliporejea na kuanza kutibu hospitali ya taifa Muhimbili.

Mwaka 1994 Louis Shika alirejea Urusi kujiendeleza kimasomo. Alisomea shahada ya uzamili katika magonjwa ya kuambukiza (MSc in Infectious Diseases) na udaktari bingwa wa magonjwa ya akili Master of Medicine (Psychiatry). Akiwa huko alishirikiana na wenzake kuanzisha kampuni ya usambazaji wa kemikali viwandani iitwayo Lancefort Ltd.

Kwa sasa ni moja ya makampuni makubwa ya usambazaji wa kemikali nchini Urusi, na jina la Dr.Shika lipo kwenye website yao kama Muasisi na Rais wa kwanza wa kampuni.

Inadaiwa shirika la ujasusi la Urusi (KGB) liligundua kwamba akina Shika walipata fedha za kuanzisha kampuni kutoka Marekani kama mkakati wa Marekani kudukua taarifa za Urusi. Kwahiyo baadhi ya viongozi wa kampuni hiyo walikamatwa. Dr.Shika alitekwa na watu waliodhaniwa kuwa majambazi kupewa mateso makali sana ikiwemo kukatwa vidole.

Balozi wa zamani wa Tanzania nchini Urusi, Patrick Chokala mwaka 2017 alinukuliwa na vyombo vya habari kwamba ilibidi kutumia mbinu za "kijasusi" kumnasua Dr.Shika na kumrudisha nchini kwa dharura. Tangu aliporejea alijiingiza kwenye ulevi wa kupindukia kutokana na msongo wa mawazo.

Kwahiyo ukifuatilia historia ya *Marehemu Dr.Shika* utagundua hakuwa "kalubandika" kama ilivyodhaniwa. Ni mtu aliyekua na maono makubwa. Kama si mipango yake kuvurugika huenda angekuwa daktari bingwa na mfanyabiashara mkubwa wa kemikali duniani.

Ni kwamba tu alijikwaa, akadondoka na hakuweza kusimama tena. Serikali ilipaswa kumsaidia kusimama lakini nayo ilimtelekeza. Kwahiyo ameishi maisha ya upweke, masononeko na msongo wa mawazo kwa muda mrefu.

Kampuni aliyoanzisha ya Lancefort Ltd ambayo kwa sasa inamilikiwa na serikali ya Urusi (ilitaifishwa) ina thamani ya $27Bil sawa na TZS 60Trilioni (Bajeti ya nchi kwa miaka miwili).
_
Kwa hiyo Dr.Shika alikuwa anajiita "Bilionea" si kwamba alikuwa anaota. He used to have money. Na hiki ndicho kilichokuwa kinamtesa maana alishindwa kukubaliana na hali yake ya sasa. Hakutaka kuamini kama aliwahi kuwa na pesa.

Kujikwaa na kuanguka ni kawaida katika maisha lakini jambo la msingi ni uwezo wa kusimama tena baada ya kuanguka. Whinston Churchil aliwahi kusema "Success is not final and failure is not fatal. It is the courage to continue that counts"
_
Mtu kama huyo hakuwa mtu wa "kumchukulia poa" hata kidogo. Serikali haikutakiwa kumtelekeza. Alipaswa kupewa nafasi nyingine. Either angerudishwa Muhimbili kutibu au angetafutiwa fursa mahali pengine ambapo taifa lingeweza kufaidi ujuzi wake na pia ingekua njia ya kumsaidia kuondokana na msongo wa mawazo na kusahau "mabilioni" yake kule Urusi.

*Pumzika kwa amani Mr. mia tisa itapendeza*

C&P from WhatsApp group.

RIP Dr. Louis Shika.

P
Umefanya sawa kuyaandika haya, wengi walimpuuza
 
RIP Dr. Shika. Bahati mbaya umetangulia mbele ya haki, wakati bado tunasubiri bajaj Yenye hela zako kutoka mtoni iweze kuwasili Tanzania, ili tuelewane
 
*R.I.P DR. SHIKA😭*

Dr.Shika alikuwa ni miongoni mwa wasomi wazuri lakini bahati mbaya elimu yake haijaweza kusaidia taifa hili achilia mbali kumsaidia yeye binafsi.

Wengi walimchukulia kimzaha tangu alipoonekana kwenye tukio la mnada wa nyumba za Lugumi (mia tisa itapendeza). Makampuni ya kibiashara yalitumia umaarufu wake kama fursa ya matangazo lakini yakamuacha hohehahe asiye hata na mahali rasmi pa kuishi. Aliwahi kuripotiwa na kituo kimoja cha TV kufukuzwa kwenye nyumba aliyokua akiishi huko Tabata baada ya kushindwa kulipia kodi.

Vyombo vingi vya habari vilikuwa vikimdhihaki na vingine kumuita Kalubandika. Lakini bila shaka vilifanya hivyo pasipo kumjua kiundani *Dr.Shika.*

Ni mzaliwa wa kijiji cha Kalemela wilaya ya Busega, mkoani Simiyu. Majina yake halisi ni Louis Shika Kidola. Yeye na ndugu yake Jeremiah Shika Kidola *(marehemu pia)* walikuwa wanafunzi wenye akili sana na waliofaulu vizuri masomo yao ya sekondari kwa alama za juu na kupata ufadhili wa kusoma udaktari nchini Urusi mwaka 1984 hadi 1991 waliporejea na kuanza kutibu hospitali ya taifa Muhimbili.

Mwaka 1994 Louis Shika alirejea Urusi kujiendeleza kimasomo. Alisomea shahada ya uzamili katika magonjwa ya kuambukiza (MSc in Infectious Diseases) na udaktari bingwa wa magonjwa ya akili Master of Medicine (Psychiatry). Akiwa huko alishirikiana na wenzake kuanzisha kampuni ya usambazaji wa kemikali viwandani iitwayo Lancefort Ltd.

Kwa sasa ni moja ya makampuni makubwa ya usambazaji wa kemikali nchini Urusi, na jina la Dr.Shika lipo kwenye website yao kama Muasisi na Rais wa kwanza wa kampuni.

Inadaiwa shirika la ujasusi la Urusi (KGB) liligundua kwamba akina Shika walipata fedha za kuanzisha kampuni kutoka Marekani kama mkakati wa Marekani kudukua taarifa za Urusi. Kwahiyo baadhi ya viongozi wa kampuni hiyo walikamatwa. Dr.Shika alitekwa na watu waliodhaniwa kuwa majambazi kupewa mateso makali sana ikiwemo kukatwa vidole.

Balozi wa zamani wa Tanzania nchini Urusi, Patrick Chokala mwaka 2017 alinukuliwa na vyombo vya habari kwamba ilibidi kutumia mbinu za "kijasusi" kumnasua Dr.Shika na kumrudisha nchini kwa dharura. Tangu aliporejea alijiingiza kwenye ulevi wa kupindukia kutokana na msongo wa mawazo.

Kwahiyo ukifuatilia historia ya *Marehemu Dr.Shika* utagundua hakuwa "kalubandika" kama ilivyodhaniwa. Ni mtu aliyekua na maono makubwa. Kama si mipango yake kuvurugika huenda angekuwa daktari bingwa na mfanyabiashara mkubwa wa kemikali duniani.

Ni kwamba tu alijikwaa, akadondoka na hakuweza kusimama tena. Serikali ilipaswa kumsaidia kusimama lakini nayo ilimtelekeza. Kwahiyo ameishi maisha ya upweke, masononeko na msongo wa mawazo kwa muda mrefu.

Kampuni aliyoanzisha ya Lancefort Ltd ambayo kwa sasa inamilikiwa na serikali ya Urusi (ilitaifishwa) ina thamani ya $27Bil sawa na TZS 60Trilioni (Bajeti ya nchi kwa miaka miwili).
_
Kwa hiyo Dr.Shika alikuwa anajiita "Bilionea" si kwamba alikuwa anaota. He used to have money. Na hiki ndicho kilichokuwa kinamtesa maana alishindwa kukubaliana na hali yake ya sasa. Hakutaka kuamini kama aliwahi kuwa na pesa.

Kujikwaa na kuanguka ni kawaida katika maisha lakini jambo la msingi ni uwezo wa kusimama tena baada ya kuanguka. Whinston Churchil aliwahi kusema "Success is not final and failure is not fatal. It is the courage to continue that counts"
_
Mtu kama huyo hakuwa mtu wa "kumchukulia poa" hata kidogo. Serikali haikutakiwa kumtelekeza. Alipaswa kupewa nafasi nyingine. Either angerudishwa Muhimbili kutibu au angetafutiwa fursa mahali pengine ambapo taifa lingeweza kufaidi ujuzi wake na pia ingekua njia ya kumsaidia kuondokana na msongo wa mawazo na kusahau "mabilioni" yake kule Urusi.

*Pumzika kwa amani Mr. mia tisa itapendeza*

C&P from WhatsApp group.

RIP Dr. Louis Shika.

P
Lancefort ilikuwa ya CIA kwa mgongo wa Dr shika,CIA wakamtelekeza .
 
Back
Top Bottom