Mpekuzi Tanzania
JF-Expert Member
- Mar 11, 2018
- 586
- 908
TAARIFA YA UJIO WA KATIBU MKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI DR BASHIRU ALLY KAKURWA MKOANI TABORA
Ndugu zangu wanaCCM tarehe 7 na 8 Disemba 2019 tutakua na ugeni wa katibu mkuu wa CCM katika mkoa wetu wa Tabora. Atakua na shughuli maalumu katika wilaya ya Nzega Jimbo la Nzega mjini.
Amealikwa kuwa mgeni Rasmi katika mkutano mkuu wa Jimbo la Nzega mjini.
Mapokezi ya kimkoa yatafanyika Wilaya ya IGUNGA saa 2:40 asubuhi tarehe 07.12.19 Jumamosi. Katibu mkuu atatembelea miradi na kuona utekelezaji wa ILANI ya CCM ulivyotekelezwa katika jimbo la Nzega mjini siku hiyohiyo ya Jumamosi .
Pia tarehe 07.12.19 Dr Bashiru atakutana na wafanyabiashara mbalimbali na ataendesha Harambee ilioandaliwa na mh BASHE kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Ukumbi wa kisasa wa CCM
Tarehe 08.12.19 atashiriki mkutano mkuu wa Jimbo akiwa ni mgeni Rasmi kusikiliza taarifa ya utekelezaji wa ILANI itakayowasilishwa na Mh HUSSEIN M. BASHE mbunge na Naibu Waziri wa Kilimo na Ushirika.
Katibu bora kabisa na mzalendo wa kweli wa CCM DR BASHIRU ALLY KAKURWA, Karibu sana mkoani Tabora
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Imetolewa na
Majaliwa Bilali
Katibu siasa na uenezi CCM Mkoa wa Tabora
Ndugu zangu wanaCCM tarehe 7 na 8 Disemba 2019 tutakua na ugeni wa katibu mkuu wa CCM katika mkoa wetu wa Tabora. Atakua na shughuli maalumu katika wilaya ya Nzega Jimbo la Nzega mjini.
Amealikwa kuwa mgeni Rasmi katika mkutano mkuu wa Jimbo la Nzega mjini.
Mapokezi ya kimkoa yatafanyika Wilaya ya IGUNGA saa 2:40 asubuhi tarehe 07.12.19 Jumamosi. Katibu mkuu atatembelea miradi na kuona utekelezaji wa ILANI ya CCM ulivyotekelezwa katika jimbo la Nzega mjini siku hiyohiyo ya Jumamosi .
Pia tarehe 07.12.19 Dr Bashiru atakutana na wafanyabiashara mbalimbali na ataendesha Harambee ilioandaliwa na mh BASHE kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Ukumbi wa kisasa wa CCM
Tarehe 08.12.19 atashiriki mkutano mkuu wa Jimbo akiwa ni mgeni Rasmi kusikiliza taarifa ya utekelezaji wa ILANI itakayowasilishwa na Mh HUSSEIN M. BASHE mbunge na Naibu Waziri wa Kilimo na Ushirika.
Katibu bora kabisa na mzalendo wa kweli wa CCM DR BASHIRU ALLY KAKURWA, Karibu sana mkoani Tabora
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Imetolewa na
Majaliwa Bilali
Katibu siasa na uenezi CCM Mkoa wa Tabora