Dkt. Ayub Rioba Vs Prof. Mruma

Sifi Leo

Platinum Member
Joined
Mar 30, 2012
Posts
5,939
Reaction score
10,823
Kusema la kweli nchi hii ina wasomi wengi.

Nakumbuka Dkt. Ayub Rioba wa TBC enzi akiwa chuoni hakika alikuwa mwanazuoni na tishio la watawala enzi hizo.

Makala zake nzito ndizo zilizopelekea Rais wa awamu ya tano kumteua kusimamia shirika la umma la TBC na wengi tulijua anaenda kutema cheche, kilichotokea ni aibu kubwa kwa taifa mpaka leo hasikiki amebakia kuwa mhariri yaani mathalani wakiitwa wahariri nae tunamwona anaenda badala ya kutuma watoto wadogo waliopo chini yake.

Mathalani nilimwona juzi kwenye tume ya Haki Jinai ulipo ilipokuwa ikizungumza na wahariri.

Ebu jiulize Prof. Mruma kama alienda kujadili Jambo ambalo linausiana na mikataba alishindwa nini kuwaomba wakina Mwabukusi, Peter Kibatala aende nao wakatetee mikataba hiyo?
 
Ila Kibatala na Lissu wako poa.
 
CCM ndo inawamaluza wasomi wetu na kuwarudisha nyuma. Job Ndugai wanadai zilikuwa zina chaji ni msomi mwanazuoni wa aina yake nchini. Darasani alikuwa kipanga genius. Angalia XCM ilivyomfanta. Kina kabudi Aidan moto wa kuotea mbali enzi hizo CCM ikamdhohofisha kielimu na kitaaluma.

Yamebaki mapoyoyo kina mwijaku yanakonfidence balaa. Hayana mshipa wa aibu Ukiyaambia hata yakunye hadharan yanakunya tu.
 
Ni utahira wa kupindukia kuacha kutumia Mtanzania mwenye uwezo mkubwa kwenye nyanja fulani kisa tu ni mpinzani.

Hii inchi ingekuwa inathamini "vichwa" pamoja na taaluma (profession), hakika ingekuwa imepiga hatua kubwa sana.

Tatizo ni kikundi fulani kiitwacho "chama" kinachoongoza inchi, hakithamini hivyo vitu viwili zaidi ya kuthamini ujinga, wingi, ushirikina na ubabe.
 
good
 
Wanapelekwa machawa kwenda kutetea mikataba badala ya wajuzi
 
Ishu ni usomi au ishu ni lugha.Kwani inakatazwa kuhojiwa kwa lugha yako ya kiswahili?
 
Wengi wetu humu hawaelewi, tatizo sio wanasheria ila sisi kama nchi hatukuwa na hoja za maana kujitetea mahakamani, nchi yetu ilifuta leseni za wawekezaji zilizopo kisheria kwa kutumia ubabe!
walioshauri zifutwe si ndiyo hawa akina Mruma na wakaonekana mashujaa kweli kweli?
 
Tangu lini hao kina kibatala wakatetea maslahi ya taifa? Hao wapo kutetea chadema basi maslahi ya taifa siyo kipaumbele chao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…