Njilembera
JF-Expert Member
- May 10, 2008
- 1,496
- 607
Mimi nakuunga mkono 100%. Hawa CCM pamoja na matusi yao wanayoandika katika vijigazeti vyao walivyovinunua na kisha kuvisambaza bure ndiyo wanaonekana kuingiwa na hofu kubwa. Hii ya Dr Slaa inaitwa 'two-pronged assault' yaani shambulio lenye ncha kali mbili. Kukosoa na hapo hapo kutwanga sera. Wanachojua CCM ni strategy ya kutoa ahadi tu -- ambazo nyingi sana hazitekelezeki.
Naam, wanachokifanya ni kuufanya ule wimbo wa Profesa - wenye kutoa ahadi mingi zisizowekana uwe ni tabiri ya kweli! Mikakati ya kuondoa msongomano wa magari Dar uko kileleni, tafiti zinaonyesha pengine mabasi ya mwendo kasi ndio njia yenye kuwezekana kwa sasa, huyu Mkuu wa CCM anakurupuka ataweka usafiri wa treni, utaanzia wapi? Ile reli ya kuja pale Ubungo? Utaweka daraja la juu pale Nelson Mandela au utaachia yapishane magari na treni pale? Yaani kesha sahau licha ya kale treni kuwa kakubahatisha, ajali za pale relini zilitisha!