DK Slaa ana miaka 70 Sasa, je ni sahihi kuendelea kuwa Balozi?

Mzito Kabwela

JF-Expert Member
Nov 28, 2009
18,857
7,617
Nijuavyo Ubalozi ni utumishi wa Umma unaolindwa kwa sheria za utumishi za nchi.

Dk. Slaa aliyekuwa katibu Mkuu wa Chadema ana miaka 70 sasa, amevuka kikomo cha miaka 60 cha kuendelea kuwa mtumishi wa Umma.

Je si sahihi kuwa sheria imevunjwa kwa kumwacha aendelee kuwa balozi?

Kwa kuwa tayari amezeeka imefika wakati anapoteza kumbukumbu jambo ambalo ni hatari sana kwa shughuli za kidiplomasia.

Mathalan, Dk. Slaa wakati alipokuwa KM Chadema alizunguka nchi nzima kuikosoa Serikali, ana account hapa JF kwa jina lake ambapo kila mara alikuwa akidondosha 'madini' humu. Leo anakataza watu wasikosoe mtandaoni..amesahau kazi aliyokuwa akiifanya kwa miaka zaidi ya 15 alipokuwa siasa za Upinzani.

Dk Slaa ni msahaulifu sana kwa sababu ya Umri wake kiasi kwamba anafananisha siasa za Tanzania kama za Sweden, anadhani huku kwetu wapo wa kuwasemea wanaoishi kwenye nyumba za Tembe kama alivyokuwa anafanya, anadhani wanahabari wapo huru kufanya kazi, amesahau Marehemu Mwangosi alivyouawa na Hajui kabisa yaliyomkuta Kabendera.

Dk.Slaa amesahau alivyokuwa akiitwa Padri Mzinzi...alivyokejeliwa humu kwa kuwana PhD ya Kanoni na hakutikisika kwakuwa alisema yeye kuwa ana ngozi ngumu. Ameshindwa kuwashauri wanaomfanya ale vizuri hivi sasa na wao kuwa na ngozi ngumu.

Dk. Slaa amesahau alivyokuwa huru kumsema Katibu Mkuu fulani wa CCM kuwa alifumaniwa akimla mtoto wa Shule wakati KM huyobwa CCM akiwa Kigoma....alikuwa huru kusema.

Slaa amesahau alipokuwa anayaanika madudu ya Deep Green, Kagoda na mengineyo.....

Kwa nini anaendelea kuwepo ubalozini mtu aliyepitiliza umri wa kustaafu? Madhara ya kumweka mzee ofisi za umma moja wapo ni usahaulifu.
 
Ulichohoji Mleta Mada, Kilihojiwa Bungeni Pia Na Majibu Ya Waziri Wa Utawala Bora Yalikuwa Haya,
Mtu Hata Akifikisha Miaka Uliyoitaja Wewe, Huwa Haimzuii Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Kumteua.
Nafasi Ya Kuwa Balozi Huwa Ni Busara Ya Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Haiangalii Umri Wa Mteuliwa
 
Tuna katiba mbovu ni hakuna mfano, eti busara ya rais. Rais hana tofauti na "Medieval Monarchs". Ovyo sana hii.
 
Kwanini iwe kwa dk Slaa tu? Mabalozi wangapi 'vimbabu' waliotumika katika balozi zetu nje ya nchi tangia tupate uhuru?
Kama siyo personal attack kwa Slaa, basi ungelijadili mfumo wa watumishi mabalozi na si kutaja jina la mtu.
Huyu kiongozi alivyokuwa mahiri kwenye upinzani, sidhani kama ana sifa mbofumbofu hata1 kati ya ulizoziainisha wewe.
 
Kwanini iwe kwa dk Slaa tu? Mabalozi wangapi 'vimbabu' waliotumika katika balozi zetu nje ya nchi tangia tupate uhuru?
Kama siyo personal attack kwa Slaa, basi ungelijadili mfumo wa watumishi mabalozi na si kutaja jina la mtu.
Huyu kiongozi alivyokuwa mahiri kwenye upinzani, sidhani kama ana sifa mbofumbofu hata1 kati ya ulizoziainisha wewe.

Sheria ziko wazi, utumishi wa umma miaka 60 unastaafu
Balozi ni mtumishi wa umma na miaka yote mabalozi wakifikisha 60 years wanastaafu
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Swali la kujazia nyama: kama Dkt angekuwa rais 2015-2020 kupitia CHADEMA ungehoji umri wake? au ungefunika kombe? prof. Safari ana umri gani? mgombea wa ukawa kupitia cuf 2015 upande wa zanzibar ana umri gani?
 
Ulichohoji Mleta Mada, Kilihojiwa Bungeni Pia Na Majibu Ya Waziri Wa Utawala Bora Yalikuwa Haya,
Mtu Hata Akifikisha Miaka Uliyoitaja Wewe, Huwa Haimzuii Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Kumteua.
Nafasi Ya Kuwa Balozi Huwa Ni Busara Ya Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Haiangalii Umri Wa Mteuliwa
Sasa vikongwe waking'ang'ania madaraka nyinyi vijana mtaajiriwa lini ?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Back
Top Bottom