Inawezekana mim nina madhaifu, kuwa sijawahi kumuona rais Kikwete ameonekana amekerwa au hata kuwa serious kukemea wizi hasa mkubwa kama huu uliotokea hivi karbuni. Sasa mimi huwa najiuliza labda kwa kuwa ni rais bas ana hela nying sana kias kuwa hela zinazopotea ni kidogo na hana machungu kabisa.
Hivi angekuwa Mwl Nyerere anahutubia jana taifa lingezizima hata watoto wadongo wangejua leo rais anaongea na wananchi.
Jana rais wangu hujalitendea haki taifa, kwanza ulionekana kutoa maamuzi kwa kuogopa, kusitasita utadhani na wewe umeiba hizo hela ,unaaingizia kikohozi kweli rais? Hvi ulijua kama dunia nzima walikuwa wanakufuatlia? Wewe unaongea na sisi utadhani tumekaa barazani tunapiga stori za mechi za nje?
Binafsi nilichukia sana, kwani nilitegemea kwa mda wote uliodai wajiandaa ili uongee na wananchi ulitakiwa kuja na majawabu yanayowasumbua wananchi hadi sasa! Ulikuwa unafanya nini ni almost siku 23 hadi jana toka ulipoahidi kuongea na kutoa maamuzi juu ya watuhumiwa.
Kwanza hotuba yako ilikuwa ni ya kawaida sana kama hakuna tatizo lolote ndani ya taifa!
Rais Kikwete, au ndio na wewe unajua ikoje? Ndio maana unaogopa kuwa mkali juu ya wizi kama huu? Au ndio unataka uondoke salama? Au ndio unataka kutupooza tu wananchi kwa kumtoa kafara mama Tibaijuka? Inawezekana huyu mama hajui chochote ndio maana mnamuengua hadharani!
Akina muhongo wanajua siri nzito ndo maana mnawaweka kipolo ili wasiwaumbue na nyie. Rais kama utapata nafas nyingne toa hutoba nyingne itakayojibu maswali juu ya mabilion ya fedha kwenye taifa lako, na kutoa mwanya wa uwajibikaji kuchukuwa nafas yake, sio kuongea kana kwamba na wewe ni mwizi hivyo unaogopa utakachoamua wezi watasema mbona na wewe rais tulikuwa pamoja!
Na haki unayoisema ichukuwe nafas sio kumuumiza mlaji unamuacha aliyepika chakuka chenye sumu.
Na swala la uchunguz kwa mambo ambayo yako wazi ni kuwaibia wananchi. Na serikali yako rais imetia fora kwa kuunda tume kisha hizo tume hata hazitusaidii. Kama unadhani nakuonea kuiponda hotuba yako njoo kitaa usikie..