Dk. Benson Bana: Kikwete yataje makundi ya CCM

Dk. Benson Bana: Kikwete yataje makundi ya CCM

n00b

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2008
Posts
1,013
Reaction score
2,684
na Betty Kangonga | Tanzania Daima | Novemba 13, 2012


MHADHIRI wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Benson Bana, amesema kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, ameshindwa kuwa muwazi katika kuainisha makundi yaliyoko ndani ya chama hicho.

Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Dk. Bana alisema Rais Kikwete alipaswa kuwa muwazi kwa kuyataja makundi yanayoonekana kukivuruga chama hicho badala ya kutumia diplomasia zaidi.

Dk. Bana ambaye ni Mwenyekiti Mwenza wa Mapango wa Utafiti wa Elimu ya Demokrasia (REDET), alisema kuwa hotuba aliyoitoa Rais Kikwete ni nzuri, lakini ina upungufu kutokana na kushindwa kuyataja makundi yanayosigana.

Alisema kuwa kama kweli Rais Kikwete alikuwa na nia ya kutaka kuondoa makundi hayo, alipaswa kuyataja hadharani kuliko kuyaficha hatua inayoonyesha kuwa ameshindwa kukabiliana nayo.

"Kama kweli alikuwa na nia ya kutaka kuyamaliza makundi yaliyopo ndani ya chama chake alipaswa kuyataja kwa kuwa ni kiongozi wa juu wa chama hicho angeagiza Kamati ya Maadili kuyaita makundi hayo ili kuyapa onyo," alifafanua.

Bana aliongeza kuwa hatua hiyo ingesaidia makundi hayo kuogopa na kupunguza kasi inayokifanya chama kuwa na mvurugano.

Kuhusu suala la rushwa, alisema kuwa bado Rais ameshindwa kuwa wazi katika kudhibiti hali hiyo isijirudie na badala yake amekuwa akikemea pasipo kuchukua hatua madhubuti.

Msomi huyo alisisitiza kuwa kama hakuna mkakati maalumu wa kudhibiti rushwa ndani ya chama hicho, upo uwezekano wa kusambaratika jambo; linaloweza kusababisha taifa kuyumba.

"Lakini hotuba yake ni nzuri ameweza kuwajengea wanachama wake kuzidi kujihami kutokana na kuweka wazi kuwa wanazidi kusimamia na kutekeleza sera katika serikali yake," alisema.

Dk. Bana pia alipongeza hatua ya kuchaguliwa kwa Philip Mangula kuwa Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, akisema kuwa hatua hiyo inaweza kukisaidia chama hicho kurudi katika nidhamu yake kama ilivyokuwa zamani.

"Kumrejesha Mangula ni kurudisha nidhamu ndani ya chama hicho ambayo ilishaanza kupotea hatua iliyokuwa ikipoteza imani kwa wananchi," alisema.
 
Ukweli ni kwamba.Ndugu Bana haamini hiki alichoongea,ifike wakati waandishi wawe wanaangalia na watu wa kuwahoji,yaani unafunga safari kwenda kupata maoni juu ya hotuba ya JK kwa ndugu Bana?
 
Hivi Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam kina msomi Dr Bana pekee? Pia hakuna vyuo vingine vyenye wasomi? Kila siku Bana tuuuuu! Inaboa sana, tunataka mchanganyiko wa mawazo, sio mawazo ya mtu mmoja tu!
 
Kamanda kwani hiyo njia aliyotumia haiwezi mfikia JK hadi kwa contact za moja kwa moja?

Mkuu nadhani unaelewa kuwa Bana ndio mshauri mtaalamu wa kisiasa wa Kikwete sasa kwa nini asimpe huo ushauri moja kwa moja?
 
Mkuu nadhani unaelewa kuwa Bana ndio mshauri mtaalamu wa kisiasa wa Kikwete sasa kwa nini asimpe huo ushauri moja kwa moja?

Kamanda kuletwa kwa habari katika vyombo vingine vya habari haina maana kuwa ujumbe haujafikishwa moja kwa moja kwa mkuu waa kaya.

Habari kama hii inatupa mwangaza wa aina ya washauri waliopo na kama Mkuu wa kaya jeuri/msikivu ama pia anasikiza ushauri. Ingeenda moja kwa moja hii scoop tungeikosa. Ndio hasa nilikuwa nikiimaanisha.
 
Kamanda kuletwa kwa habari katika vyombo vingine vya habari haina maana kuwa ujumbe haujafikishwa moja kwa moja kwa mkuu waa kaya.

Habari kama hii inatupa mwangaza wa aina ya washauri waliopo na kama Mkuu wa kaya jeuri/msikivu ama pia anasikiza ushauri. Ingeenda moja kwa moja hii scoop tungeikosa. Ndio hasa nilikuwa nikiimaanisha.

Pamoja sana
 
Kamanda kuletwa kwa habari katika vyombo vingine vya habari haina maana kuwa ujumbe haujafikishwa moja kwa moja kwa mkuu waa kaya.

Habari kama hii inatupa mwangaza wa aina ya washauri waliopo na kama Mkuu wa kaya jeuri/msikivu ama pia anasikiza ushauri. Ingeenda moja kwa moja hii scoop tungeikosa. Ndio hasa nilikuwa nikiimaanisha.

Mkuu wa Kaya alivyo kichwa Maji atasema "Ni Upepo tu, na utapita"
 
Ukweli ni kwamba.Ndugu Bana haamini hiki alichoongea,ifike wakati waandishi wawe wanaangalia na watu wa kuwahoji,yaani unafunga safari kwenda kupata maoni juu ya hotuba ya JK kwa ndugu Bana?
AKUUNGA mkono mkuu. Bana siyo mtu wa kuhoji kuhusu mambo ya MAGAMBA kwa sababu nye ni GAMBA gumu
 
Bana pamoja na kumsifia JK siku zote naona hawajamkumbuka kwenye teuzi yeyote ile
 
political analysts wa kwetu wananjaa na uoga ukilinganisha na wa ulaya..wanahali fulani ya kutojiamini.Bana huyuhuyu ukikuta anachambua mambo ya Zimbabwe au Congo utampenda..jembe lililopo ni Baregu ambaye pamoja na kubaniwa ajira yake chuo kikuu hakubadili misimamo yake ya kuichambua serikali ya mafisadi
 
hivi sikuwahi kukataza comment za huyu m.weh* kuwekwa humu jamvini?
 
Nadhani kila mtu mwenye akili timamu anafahamu jinsi CCM ambavyo imegawanyika kwa makundi. Sasa wanapotuongopea ya kwamba kwenye uchaguzi wao watu wameshinda kwa 100% na JK kashinda kwa 99.2% wanafikiri ya kwamba inawasaidia kuongopa kwa jamii ya kwamba chama chao hakina mgawanyiko au? wakati hata huyo mwenyekiti wao kila siku katika hotuba zake za chama analalamika kuhusu mpasuko uliopo katika chama chao. Au wanataka kutuambia ya kwamba ile mipasuko yao ya chama chao imeshakuwa solved? wasitake kuwafanya Watanzania ni wajinga. Mi nadhani wamejidhihirisha kwa jinsi gani nia waongo na wanafiki.
 
Back
Top Bottom