masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 18,409
- 14,116
Dk 45 ya leo ilikuwa ina bore.
ITV inabidi wajifunze kuweka watu wenye uelewa mkubwa zaidi ili kuwaweka kiti moto wasomi kama Prof Mukandala katika kipindi cha dk 45 ya leo.
Muulizaji maswali kipindi cha leo si msomi, hivyo maswali yake hayakuwa ya kina na naweza kusema general questions.
Maswali ya kitoto kama wahadhiri kuwa na uhusiano na wanafunzi, wanafunzi na mikopo, hostel za wanafunzi, haya yote yangeweza kujibiwa na karani wa wizara elimu ya juu.
Maswali.mazito juu ya uhusiano wa elimu ya juu na sera ya viwanda sikuyasikia.
Maswala ya matumizi na mafanikio ya utafiti wa wasomi wetu sikusikia.
Matumizi mabaya ya maeneo ya kisomi(Academic Areas) na kuyageuza kuwa ya biashara, kama Mlimani City, hayakuulizwa kisawasawa.
Uwekezaji kitaifa katika elimu ya juu, R&D yaani utafiti katika teknolojia, matazamio katika eneo hilo kiujumla ~hakuna kabisa!
ITV, leo mmempa Prof Lwekaza Mukandala, a walkover!
ITV inabidi wajifunze kuweka watu wenye uelewa mkubwa zaidi ili kuwaweka kiti moto wasomi kama Prof Mukandala katika kipindi cha dk 45 ya leo.
Muulizaji maswali kipindi cha leo si msomi, hivyo maswali yake hayakuwa ya kina na naweza kusema general questions.
Maswali ya kitoto kama wahadhiri kuwa na uhusiano na wanafunzi, wanafunzi na mikopo, hostel za wanafunzi, haya yote yangeweza kujibiwa na karani wa wizara elimu ya juu.
Maswali.mazito juu ya uhusiano wa elimu ya juu na sera ya viwanda sikuyasikia.
Maswala ya matumizi na mafanikio ya utafiti wa wasomi wetu sikusikia.
Matumizi mabaya ya maeneo ya kisomi(Academic Areas) na kuyageuza kuwa ya biashara, kama Mlimani City, hayakuulizwa kisawasawa.
Uwekezaji kitaifa katika elimu ya juu, R&D yaani utafiti katika teknolojia, matazamio katika eneo hilo kiujumla ~hakuna kabisa!
ITV, leo mmempa Prof Lwekaza Mukandala, a walkover!