Sigara Kali
JF-Expert Member
- May 28, 2017
- 3,623
- 8,428
Salaam wana JF
Naomba kuuliza hivi nchi yetu hii ina dira yoyote ya maendeleo ambayo inaendelezwa na viongozi? Manake kila rais wa nchi hii akiingia madarakani anakuja na Sera na dira zake akiondoka zinakufa kifo cha mende chalii
1.Mkapa kaja na Uwazi na Ukweli akabinafsisha mashirika ya umma kaondoka madarakani hakuna kilichoeleweka nchi ikaendelea Kuwa maskini na Watanzania wakaendelea Kuwa maskini wa kutupwa
2.JK kaja na maisha Bora kwa kila mtanzania na akaja na Sera ya kilimo kwanza na matokea makubwa sasa( Big Results Now) kaondoka kaacha kilimo kipo mahututi,kaacha umaskini wa kutupwa ingawa baadhi ya Watanzania wajanja walinufaika na utawala wake ,BRN sijui iliishia wapi
3.JPM huyu kaja na sera ya Tanzania ya viwanda Lakini hadi sasa sioni kinachoendelea zaidi ya matukio mara kutumbua,mara kuteua mara Makinikia kushtukia 2020 hiyo hakuna la maana tutakalopata zaidi ya kuendelea na shida na umaskini wa kutupwa
Mnijuze nchi yetu hii ina mpango gani endelevu wa maendeleo manake kila anaekuja anakuja na taratibu zake ambazo kimsingi naona zinarudisha nyuma maendeleo.
Naomba kuuliza hivi nchi yetu hii ina dira yoyote ya maendeleo ambayo inaendelezwa na viongozi? Manake kila rais wa nchi hii akiingia madarakani anakuja na Sera na dira zake akiondoka zinakufa kifo cha mende chalii
1.Mkapa kaja na Uwazi na Ukweli akabinafsisha mashirika ya umma kaondoka madarakani hakuna kilichoeleweka nchi ikaendelea Kuwa maskini na Watanzania wakaendelea Kuwa maskini wa kutupwa
2.JK kaja na maisha Bora kwa kila mtanzania na akaja na Sera ya kilimo kwanza na matokea makubwa sasa( Big Results Now) kaondoka kaacha kilimo kipo mahututi,kaacha umaskini wa kutupwa ingawa baadhi ya Watanzania wajanja walinufaika na utawala wake ,BRN sijui iliishia wapi
3.JPM huyu kaja na sera ya Tanzania ya viwanda Lakini hadi sasa sioni kinachoendelea zaidi ya matukio mara kutumbua,mara kuteua mara Makinikia kushtukia 2020 hiyo hakuna la maana tutakalopata zaidi ya kuendelea na shida na umaskini wa kutupwa
Mnijuze nchi yetu hii ina mpango gani endelevu wa maendeleo manake kila anaekuja anakuja na taratibu zake ambazo kimsingi naona zinarudisha nyuma maendeleo.