Linaendana na mada.
Ziko dini zimesaidia sana katika juhudi za kuleta maendeleo katika nchi hii.
Baadhi ya dini zimeweza kujenga taasisi nyingi za msingi katika jamii, kama Shule, Vyuo, Viwanda, Hospitali, Barabara, Vyanzo vya Umeme, na kujumuisha wanachi katika kuboresha shughuli za Kilimo, Ufugaji, Uvuvi, Ujenzi, nk.
Ziko dini zilizo dunisha maendeleo ya jamii kila zilipoweka kambi za kidini na kuifanya jamii zilizowakaribisha kiwa nyuma katika maendeleo.
Ziko baadhi ya dini wanaabudu usiku na haijulikani wanachokifanya kwa jamii inayowazunguka, kila kitu kwao ni siri siri.
Ziko dini zinazoongozwa na akina Nabii Tito. Kazi yake ni kuhimiza Ulevi, Uvivu, Uzinzi, Starehe nk.
Unaposema madhara ya dini inabidi uzitaje hizo dini na madhara yake katika jamii.
Na sio kujumlisha kila dini
Hayo yote unayozungumza yapo kwenye nchi tofauti duniani, na zina maendeleo kuliko nchi yoyote ya Africa.
Nakupa mfano, Saudi Arabia, Dominated by Islam (japo sio islamic state). Hii nchi wana rasilimali moja tu ya mafuta, wapo hatua milioni 300 kuliko tanzania yenye Almasi, yenye Dhahabu, yenye Uranium, Yenye Wild life, yenye Gas, yenye Tanzanite. Sasa nataka unambie, udini umeingiaje hapo kwenye rasilimali kiasi kwamba taifa haliendelei? Tuanze kuwatizama ma CEO wa kampuni zinazojishughulisha na izo rasilimali na watu waliozunguka sehemu husika wana dini gani kisha tuseme dini ndio tatizo?
Kwanini waafrika wenye dini ndio waonekane hawaendelei lakini wasiokuwa waafrika wenye dini wanaendelea?
Hivi wewe rais, majukumu yako unayajua kwa wananchi lakini huyakamilishi, tatizo linakuwa dini? au Tamaa zako?
Wewe umeenda chuo kusoma, kufika chuoni ukaona bora ujiuze, ujichubue uwe mweupe, tatizo ni dini?
Wewe unamuona mwenzako anapata mafanikio, unaanza kumuonea choyo na kumtia husda, tatizo ni dini?
Wewe ushaona mbunge wako umemtilia kura, kashinda, kila mwisho wa mwezi anapewa pesa za jimbo, anakwenda kufanya mambo yake binafsi badala ya kuzitumia jimboni, halafu uchaguzi mwengine umefika, unamtilia tena kura, tatizo ni dini?
Mungu amejaalia nchi ina neema, amekuja fulani anataka kufungua kiwanda kuzalisha bidhaa fulani, unamwambia humpi leseni mpaka akupe 10% share, tatizo ni dini?
yapo mengi, ila naomba unijibu moja moja.