Dini inanikosesha mke

Dini inanikosesha mke

Roho Mbaya

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2012
Posts
777
Reaction score
677
Mimi ni kijana mwenye umri miaka ishirini na nane 28, nimetokea kumpenda binti dini ya Kisilaam ni takribani miaka minne hivi sasa, amekuwa akishindwa kuniweka wazi kama ananipenda,ingawa ukaribu wangu mimi na yeye ndani ya miaka hiyo minne umewaaminisha watu kuwa tupo kwenye mahusiano.

Kutokana na hali hiyo nikamtangazia kumuoa lakini amekuwa akinikatalia ombi langu la kuolewa na mimi kisa tofauti ya dini, kuwa mimi ni mkiristo ingawa mpaka muda huu tayari nipo nae kwenye mahusiano ya kimapenzi.

Tatizo nikimugusia swala la kumuoa yeye anaingiza kigezo cha dini, naombeni ushauri wenu, kweli binti nampenda na yeye ananipenda ila kosa hii dini inanikosesha mke.
 
Ni ngumu sana kwa mkiristo kubadili dini na kuwa muislamu, ila ni rahisi sana yy kuja upende wako!
 
Kwan yeye anakataa kama yeye au kuna shinikizo la wazazi/ ndugu? Kama ni yeye anaongea anapenda mgegedo tu kwako na mengineyo.... Ila kuwa makini asikuchezee dudu afu akuache....vinginevyo tafta mkiristo mwenzio
 
Khaa!! Wajina Kumbe ulikwisha olewa na dini sasa huyo unamtaka wa nini? Vitu vingine vya kujitakia tu
 
Soon nitakua na kesi hiyo..sasa nakaa kimya nipate majibu hapahapa kabla hata ya mtihani
 
Back
Top Bottom