Kwa mujibu wa mpekuzi wetu ambaye kazi yake ni kufuatilia mambo ya watu, Diamond alifikia hatua ya kumtandika hadi akamharibu uso kisa kikielezwa ni wivu wa kimapenzi.
Chanzo kiliendelea kutambaa na mistari kuwa ilitokea purukushani kubwa ambapo Wema aligeuka bondia Mbwana Matumla kwa kupangua makonde ya Francis Miyeyusho kama alivyofanya wiki iliyopita pale Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
Ilidaiwa kuwa staa huyo wa filamu hakufua dafu kwani Diamond alipeleka konde moja matata kama lile la Miyeyusho kwa Matumla hivyo kumwachia michoro ya makofi usoni huku akimsababishia mrembo huyo kutosikia vizuri hadi sasa.