Sababu zipi sio "za ki ujinga" za kumpiga mwanamke?...sipendi domestic violence ya aina yeyote..
tena sababu zenyewe zikiwa za ki ujinga kama 'txt'...
Gee ujasiri ni jambo moja na utendaji wa vyombo husika ni jambo lingine.
mara nyingi sana kesi kama hii ukifika kituo cha polisi unaambiwa rudi mkayamlizie nyumbani...na hili limewajengea wengi mazoea kuwa ntamdunda na tukifika polisi tutarudishwa nyumbani tuje tumalizane.
Sasa hapo ndo itategemea kama unajua kukomaa ukomae na bondia wako. Lakini kwa mtazamo wangu domestic violence zimelelewa sana na vyombo vya dola kwa upande mwingine.
Sababu zipi sio "za ki ujinga" za kumpiga mwanamke?
Root problem Gaijin, mara nyingi tuna nyanyaswa na kuonewa kwa kutofhamu nini ni haki na nini ni wajibu wetu kisheria. wangapi wana uthubutu wa kumwambia polisi nipe kauli yako kwa maandishi??? kwanza chochote anachosema utashangaa wengi wetu tunakubali tu kwa kumwogopa.Tatizo nilionalo ni kuwa mbali ya kuwa hakuna ujasiri lakini hata hao wenye nao hawajui haki zao kisheria
Polisi kama hataki kufungua kesi yako kwa aliyekupiga na kukwambia "kayamalizeni nyumbani" mwambie nipe maneno hayo kwa maandishi
Ukirudi nyumbani ukigeuka bondia au ukitafuta watu wa kukodi kumpiga, uwe na maandishi yaliyokuruhusu kufanya hivyo.
Sheria ipo lakini tunawaachia watu wazifinyange finyange na kutukosesha haki zetu
Root problem Gaijin, mara nyingi tuna nyanyaswa na kuonewa kwa kutofhamu nini ni haki na nini ni wajibu wetu kisheria. wangapi wana uthubutu wa kumwambia polisi nipe kauli yako kwa maandishi??? kwanza chochote anachosema utashangaa wengi wetu tunakubali tu kwa kumwogopa.
Ndugu yangu wanapenda kuandikwa hao,tena muda mwingine wanapiga kabisa na cm jamni kuna hiki mbona hamjaandika?I hope amechukua hatua muafaka. Kwa sababu kupigwa na kutolewa magazetini namna hii ni udhalilishaji wa aina yake
Hilo ni tatizo sugu kabisa. Na inachosikitisha hata wale uliodhani wana uelewa kama hapa JF wanakuja na hadithi ndeefu za kukuvunja moyo.
Kuna wengine wanasema ni "haki yake" na wengine ni "ishara ya mapenzi". ....Baada ya majibu kama haya mwanamke mwengine likimfika ataona hata aibu kuhadithia seuze kwenda kwenye vyombo vya sheria.
Wale waliowahi kuwafunguwa mashitaka utakuta wanaona haya kuhadithia kwa sababu jamii itawaona "wanoko"
Tunahitaji major changes kwenye jamii yetu kwa kweli
hii ndio hasa reflection ya jamii yetu. mtu anashabaikia kabisa jambo ambalo ni kinyume na haki. sasa wenzangu na miye kule kwetu ambako hata uelewa wa mambo ya msingi haupo ndo utegemee maajabu?
Gee hapo kwenye kufungua mashtaka na baadae kuona haya kuthibitisha kesi yako nimeshuhudia mara nyingi sana, watu wanaogopa jamii na kusahau stahili zao. kwa mfano mashauri ya kubakwa, incest n.k. mtu anakana kabisa siku ya kesi kuwa hapana hayo aliyoyaeleza mwanzoni si ridhaa yake. utamfanyaje sasa?? si shauri litupwe tu maana shahidi mkuu wa jamuhuri ndo huyo kaigeuka!!!
Hii jamii ilivyo kama huna moyo wa chuma hufungui mashitaka na haijalishi kama hao watu wamesoma au hawajasoma. Wewe ulofungua mashitaka ndo utaonekana mhalifu
Mimi nilimfungulia mtu mashitaka, watu walotuzunguka (ambao wote walikuwa exposed na wana elimu ya kutosha) walinisema mpaka basi ATI "nataka kumharibia maisha"!!
Kwa hiyo ni kupiga moyo konde tu, as long as unajua ni haki yako usikubali mtu mwengine kukukatisha tamaa. Haki haiji tu hivi hivi
kwani yeye anapokupiga au kukutendea kinyume na sheria anakuwa amefanya nini?? aisee mimi hii kichwa yangu mbovu hii hata mia mbili kama ni haki yangu nakupeleka kwa polisi ndo ije kuniudunda hadi na mi alama ya vidole juu?? mimi sijali nani anasema nini juu yangu so long as najua ninachofanya "ndicho ninachopaswa" kufanya !!! kwanini niumie kwa kukuridhisha tu?? people strain for just no good reasons wallah....
halafu kun ahili la kuambiwa ukifika kituoni eti hakuna gari la kumhamishia mtuhumiwa kituo husika cha polisi (kama hapo ni police post), yaani jamani hili suala ni pana tu na vikwazo ni vingi
Mkuu unakulaga chakula cha Nguruwe nini maana naona njix zako kama za pork hivi au macho yangu ila samahani kama nimeingilia maisha yako!!Safi sana mwanamke asie sikia ni kumzabua tu vibao
Sasa Bee kama hakuna gari la kumhamishia wewe uloenda kushtaki ufanyeje?
Nchi imeoza hii, hakuna hata sehemu moja yenye afuweni. Na sio kuwa kikija chama kipya madarakani ndo tutapata unafuu! Hatupati kwa sababu mentality zetu wengi kama zimeingia maji. Wewe mtu keshakupiga kisha unaambiwa ukamalizane nae nyumbani. Akikuuwa kabisa jee?!
Unapiga simu polisi kuna wahalifu pahala unaambiwa hatuna usafiri, hatuwezi kuja
Kuipata haki yako Tanzania ni ngumu mno, maana hata hivyo vyama vyama vya kupigania haki navyo vimelala havina msaada.
Hili walau wangelisemea kidogo. Wanafanya kama mtu kupigwa ni "a good thing"
maisha ya mastaa wetu hayo.