King junior
Member
- Apr 8, 2011
- 63
- 12
Nionavyo mimi " Wananchi wamepunguza imani na CCM kutokana na udhalimu na ufisadi unaofanywa kila leo na chama tawala hadi serikalini.
Kiukweli hamsomi alama za nyakati, na hambadiliki kutokana na wakati, mmekuwa mkiimba nyimbo zile zile tangu Uhuru ambazo wananchi wengi tumezichoka. Hata mnachokifanya sasa ni danganya toto, kwani kitendo cha 'KUVUA GAMBA' kwa ninavyojua ni kuacha mabaya na kutenda mema yaani kama kitu kinazaliwa upya.
Kimsingi hamtambui kuwa kansa hukaa kwenye damu na si kwenye gamba kama mnavyofikiri, tatizo sio viongozi, bali ni system yenu mbaya. Mlipaswa kukaa pamoja kuondoa tofauti zenu, ndio muanze mchakato wa kulivua hilo gamba lenu. Hao mnaowatoa wana makundi, wanaoingia NEC wana makundi pia, hivyo mtarudi palepale.
Mnapaswa kubadili nyimbo, mjisafishe wenyewe kwanza, muwe mstari wa mbele kupiga vita ufisadi ndani ya chama na serikalini na si kuongoza nchi kirafiki kama ilivyo sasa, la sivyo mtakuwa mnafagia uchafu, harafu mnarudisha uchafu" Ni hayo tu, 'MUNGU IBARIKI TZ, MUNGU IBARIKI AFRIKA.'
Kiukweli hamsomi alama za nyakati, na hambadiliki kutokana na wakati, mmekuwa mkiimba nyimbo zile zile tangu Uhuru ambazo wananchi wengi tumezichoka. Hata mnachokifanya sasa ni danganya toto, kwani kitendo cha 'KUVUA GAMBA' kwa ninavyojua ni kuacha mabaya na kutenda mema yaani kama kitu kinazaliwa upya.
Kimsingi hamtambui kuwa kansa hukaa kwenye damu na si kwenye gamba kama mnavyofikiri, tatizo sio viongozi, bali ni system yenu mbaya. Mlipaswa kukaa pamoja kuondoa tofauti zenu, ndio muanze mchakato wa kulivua hilo gamba lenu. Hao mnaowatoa wana makundi, wanaoingia NEC wana makundi pia, hivyo mtarudi palepale.
Mnapaswa kubadili nyimbo, mjisafishe wenyewe kwanza, muwe mstari wa mbele kupiga vita ufisadi ndani ya chama na serikalini na si kuongoza nchi kirafiki kama ilivyo sasa, la sivyo mtakuwa mnafagia uchafu, harafu mnarudisha uchafu" Ni hayo tu, 'MUNGU IBARIKI TZ, MUNGU IBARIKI AFRIKA.'