cheusimangala
JF-Expert Member
- Feb 27, 2010
- 2,585
- 499
Tujadili Dhana Ya Ubikira
Wenzetu Swaziland wanawapima wasichana wao kutambua kama ni bikra au la! Msichana akikutwa bikra anapewa cheti ambacho ndiyo kinamhalalisha kuolewa, msichana asiyekuwa na cheti haolewi ngó! Hivi mpango huu ukianzishwa bongo jamani hii michango ya harusi isiyoisha kila kukicha si itakuwa ndiyo baibai !
Baada ya kusoma hapo juu hebu soma habari hii niliyoikuta katika blog ya bwana MJengwa Maggid kisha tujadili kwa pajoma .
.............................................................
Siku sio nyingi nilibahatika kuongea na rafiki yangu mmoja ambaye ameoa nikamuhadithia kisa cha kijana mmoja aliyejikuta akilazimishwa kumuoa binti ambaye alikua na lengo la kumuonja tu na kumuacha pindi jua litakapochomoza lkn janja yake hiyo `ilibaunsi` kwani baba wa binti akiongozana na wazee wengine wa kichaga waliobeba mapanga yaliyomeremeta kama kioo kwa makali huku hasira kali zikionekana machoni mwao mithili ya kifaru aliyejeruhiwa walivamia chumba ambacho kijana huyo alikitumia ku ipopoa bkira ya binti huyo na ktk hali ya kutweta kwa hasira huku sauti yake ikionesha kutoruhusu masihara wala mzaha wa aina yeyote baba huyo wa binti alimwambia kijana,
"nyie fijana wa mkini wapaya sana,hujaona raha hadi umemrupuni pinti yangu ukaitoa pikira yake …"
Alisema hayo huku akionesha kwa kunyoosha panga ktk mashuka yaliyotapakaa damu kama ushahidi wa bikira hiyo ya bintiye iliyotolewa na kijana huyo aliyefika kijijini hapo akitokea dar pamoja na rafiki yake kwa lengo la kuwasalimia wazazi wa rafikie kisha mzee huyo wa kichaga akaendelea kuongea.
"papangu inaonesha umesoea kurupuni fipinti na kufiacha lkn huyu wangu utaoa aisee papaangu maana ni wewe umemtoa pikira na usipomuoa ukaniachia hapa hakuna atakayemuoa mbila pikira,sitaki cha mahari wala nini ninachotaka ni umuoe tu uende naye huko kwako dar".
Huku akiwa kajifunika na mashuka yaliyolowa damu kijana alijaribu kujitetea kwa kusema,
"lkn wazee wangu mimi nimepanga nikae hapa siku mbili tu kisha nirudi dar kuwahi kazini hivyo nipeni muda niweze kujiandaa wazee wangu".
Mjomba wa binti huyo aliyeonekana kuwa kijana miongoni mwa wanaume ktk kundi hilo lililofanya uvamizi akadakia kwa jazba.
"chalii acha kuongea upuuuh upuusi,hamna cha kujiandaa wala nini tena kwa taarifa yako tunachinja mbusi ya kiapo maana unaonekana mjanja mjanja lkn hiyo damu ya kiapo haina masihara chalii ukimkimbia tu huyu pinti au ukimuoa halafu ukawa na wanawake wengine au kumtesa utayaona makipu ya kiapo"
Mlolongo ulikua mrefu lkn kwa kifupi ni kwamba kijana huyo aliyekua na mchumba dar aliyemvalisha pete huku ikiwa imebakia miezi michache afunge ndoa na mchumbae huyo alijikuta akiwa hana jinsi bali kumuoa binti yule wa kichaga aliyefumaniwa naye kwa ndoa ya dharura iliyofanyika huko huko kijijini machame na kurudi dar akiwa na mke wake wa halali kabisa na sasa miaka imepita na wana watoto wawili.
Baada ya kumaliza kumuhadithia rafiki yangu kisa hiki akasema;
"dah!hata ingekua ni mimi nisingejuta kumuoa huyo binti maana asikwambie mtu bwana kuoa mwanamke bikira kuna raha zake maana mwenyewe unaanza kufungua kitu na box kikiwa cealed".
Kauli hii aliyoitamka rafiki yangu haikua mara ya kwanza kuisikia,nimeshaisikia mara nyingi sana tena na ninajua inasehemu kubwa ktk mila zetu za "kale" ambazo kila binti alitakiwa aolewe akiwa "kitu na box bin cealed aka bikira".
Hata hivyo pamoja na kuwa kauli hii nimeisikia mara lukuki lkn baada ya kuongea na rafiki yangu huyu nilijikuta nikiitafakari kauli yake baada ya yeye kuniaga.
Mawzoni mwangu nilikubaliana na kauli yake kwa namna moja au nyingine kwani
1.kama kila binti ataweza kujichunga na kuolewa akiwa na bikira basi hata maambukizo ya magonjwa kama ukimwi yasingekuwa makubwa kama ilivyo leo.
2.mimba za mashuleni zilizopelekea kina mama wengi kukatiza masomo yao huku waliowatwika mimba hizo wakisonga mbele huku kila dakika wakisema"wanawake bwana akili zao ndogo sana"zisingekuwepo.
3.dhambi ya zinaa iliyo machukizo mbele za mungu ingepungua.
4.n.k.
Nikiendelea kuwaza nilitamani siku moja mungu akinijalia kuwa na binti na yeye aolewe akiwa kitu na box kwani mwanamke mwenye bikira huonekana eti ana "thamani"kuliko asiyekua nayo sbb bikira yake ni "uthibitisho" tosha kuwa ni mwanamke aliyejitunza na mwenye kulelewa vyema asiye mapepe.
Nikiendelea kuwaza nilitamani binti yangu aje kuolewa akiwa na bikira kwa sbb tofauti na zile nilizozoea kuzisikia,mie nilijiambia mawazoni;
"kama binti yangu ataolewa akiwa na bikira ina maana atakua amesoma vizuri bila kuyumbishwa na wanaume wanaolaghai watoto wa kike wakiwa mashuleni na hivyo atakua na "thamani"kwani atakua ameweza kupata elimu ambayo ndio ufunguo wa mafanikio wa maisha ya thamani na kikubwa kuwa mbali na maambukizi ya magonjwa kwani bora mimba italeta mjukuu".
Hata hivyo niliendelea kuwaza juu ya suala zima la bikira na mazingira mazima ya maisha tunayoishi leo.
Enzi za mabibi na mababu zetu elimu pekee iliyotolewa kwa mtoto wa kike ilikua ni juu ya "kumlea mume"kwa heshima woga na unyenyekevu ikiwa na topic kama jinsi ya kumpikia mume chakula kizuri,jinsi ya kumnawisha mume mikono kabla na baada ya kula,jinsi ilivyo mwiko kumuacha mume kupeleka maji ya kuoga bafuni mwenyewe na jinsi ya kumuogesha kwa kisahani na maji yenye maua waridi na langilangi,elimu iliyomuandaa binti kuishi maisha ya kumilikiwa na mume na kumpandikizia imani kuwa ktk maisha yake hayo mwanaume ndiye bora na mwenye uwezo wa kufanya yote makubwa na yenye manufaaa hivyo aheshimiwe na kuogopwa kwani akikupa talaka "hutaweza" kuyafanya aliyokua akikufanyia.
Niliendelea kuwaza zaidi kuwa labda iliwezekana enzi hizo za mabibi na mababu mabinti wengi wakaolewa wakiwa bikira sbb waliolewa wakiwa wadogo sana baada tu ya kuvunja ungo huku wengine wakiwa hawana hata manyonyo.
Leo hii maisha yamebadili mkondo,elimu haina mke wala mume,pesa inatafutwa na mke na mume,ule umri ambao zamani binti tayari alishaozwa ni umri ambao binti leo yuko katikati ya masomo yake yenye kumjengea imani kuwa"hakuna tofauti yeyote ktk ubongo wa mwanamke na mwanamume na kwamba analoweza kufanya baba hata mama anaweza"
Leo hii ni wanawake wachache wanataka kuolewa wakiwa hawana nyuma wala mbele na kwa maana hiyo mpaka mtu aolewe utakuta ana umri mara mbili ya ule aliotakiwa aolewe enzi ya bibi na babu na ilihali mwili wake ukitoa changamoto za kufanya mambo ya wakubwa na hivyo kushindwa kuvumilia na kujikuta akipoteza "kitu na box yake" kwa boy friend.
Hata hivyo bado sielewi ni kwa nini mwanamke asiye na bikira apungue "thamani" na nilipoamua kuwaza kama mwanaume nilijiambia kuwa;
"ningekua mwanaume ningemdhamini mwanamke iwapo.."
1.ana mapenzi ya dhati kwangu
2.ana upendo na heshima kwake na kwa watu wengine wa aina zote.
3.mcha mungu.
4.mchapa kazi,mwenye uchu wa maendeleo na mwenye akili za kuzaliwa ktk kupambanua mambo.
5.mrembo kulingana na macho yangu.
Sbb kama nitathamini tu wale wenye bikira na kuwaona eti ndio waliojitunza,je wale wanawake ambao;
*aliolewa akiwa na bikira yake lkn mumewe akafariki baada ya wiki moja lkn bikira ilishatolewa na marehemu mumewe.?
*walibakwa na bikira zao kutolewa bila hiyari yao.?
*hana bikira ana sifa kama nilizotaja hapo juu?
*anayo bikira ni kitu na box lkn mvivu,hana akili za kuzaliwa,hana muamko wa maendeleo na havutii machoni mwangu?
Nilishawahi kusikia eti kuna makabila walikua wanawashona watoto wao ktk sehemu za siri ili tu wasijekupoteza bikira zao na kuiletea familia aibu,jambo ambalo ni unyama na lenye madhara makubwa.
Wapo eti mabinti ambao kwa kuogopa kupoteza bikira zao waliamua kufanya mapenzi kinyume ya maumbile huku sehemu za mbele zikiwa zimehifadhiwa kwa ajili ya atakayeoa tu ili siku ya harusi "ndoa ijibu".
Wapo ambao nasikia walinunua dawa zinazoweza kurudisha bikira na siku walipoolewa wakakutwa ni kitu na box wakati mji mzima unajua kua huyo binti alikua hatari kwa waume za watu lkn mume alimthamini kuliko hata yule aliyepoteza ubikira wake kwa mwanaume mmjoa tu.
Kitu kingine ambacho sielewi kuhusu hili suala la bikira,ni kwanini wanaume wao ni sawa kupoteza "ubikira wao" na thamani yao isipungue,tena ndio "inapanda"kadiri wanavyozidi kuipoteza maana utasikia wakiambiana"aah sema mzee watotoz naona umetoka kubangua" na wala hataitwa changudoa wala baba huruma wala maharage ya mbeya au fagio la city na wala hatakosa mke tena unaweza kumsikia akisema mwanamke atakayemuoa sharti awe bikira lkn sisi ukiwa"mamaa wa mababaz"utaitwa malaya,changudoa,jamvi la wageni mama teresa mama huruma na hakuna atakayetaka kukuoa.
Kwanini kama wanaume wanapenda kuoa wanawake wenye bikira na wao wasiutunze ubikira wao ili waje waoe wakiwa bikira na mke awe bikira,lkn la!wao ndio wa kwanza kwenda kuwarubuni wadogo zetu wa kike mashuleni na hata kuwarubuni wanawake wenye kujiheshimu na wenye misimamo kwa lugha tamu tamu na hata kwa uchumba hewa ilimradi tu wawaonje,tena wengine hujifanya hadi walokole wanapomuwinda binti wa kilokole.
Lingine ambalo sielewi,utakuta eti mwanaume anajisifia kwamba mie mke wangu nilimuoa na bikira lkn anaisaliti ndoa yake na wanawake wengine,sasa kama bikira ina thamani kuubwa kiasi hicho mbona haijatosha kuwatuliza wanaume hawa wasizisaliti ndoa zao!?
naielewa sababu ya kidini ila kuhusu hili lkn mbali ya kidini Sielewi kama huu ni ubaguzi wa kijinsia au ukandamizaji,imani tata au mawazo potofu maana ningefurahi kujua kama wapo wanaume wenye kujiheshimu kwa kuutunza ubikira wao ili aoe akiwa yuko"kitu na box cealed aka bwanaharusi bikira" kwani wengi ninaowajua wanasema eti wananoa misumeno huko na huku ili wakioa kitu kiwe kikali waweze kumridhisha mamaa.
Wenzetu Swaziland wanawapima wasichana wao kutambua kama ni bikra au la! Msichana akikutwa bikra anapewa cheti ambacho ndiyo kinamhalalisha kuolewa, msichana asiyekuwa na cheti haolewi ngó! Hivi mpango huu ukianzishwa bongo jamani hii michango ya harusi isiyoisha kila kukicha si itakuwa ndiyo baibai !
Baada ya kusoma hapo juu hebu soma habari hii niliyoikuta katika blog ya bwana MJengwa Maggid kisha tujadili kwa pajoma .
.............................................................
Siku sio nyingi nilibahatika kuongea na rafiki yangu mmoja ambaye ameoa nikamuhadithia kisa cha kijana mmoja aliyejikuta akilazimishwa kumuoa binti ambaye alikua na lengo la kumuonja tu na kumuacha pindi jua litakapochomoza lkn janja yake hiyo `ilibaunsi` kwani baba wa binti akiongozana na wazee wengine wa kichaga waliobeba mapanga yaliyomeremeta kama kioo kwa makali huku hasira kali zikionekana machoni mwao mithili ya kifaru aliyejeruhiwa walivamia chumba ambacho kijana huyo alikitumia ku ipopoa bkira ya binti huyo na ktk hali ya kutweta kwa hasira huku sauti yake ikionesha kutoruhusu masihara wala mzaha wa aina yeyote baba huyo wa binti alimwambia kijana,
"nyie fijana wa mkini wapaya sana,hujaona raha hadi umemrupuni pinti yangu ukaitoa pikira yake …"
Alisema hayo huku akionesha kwa kunyoosha panga ktk mashuka yaliyotapakaa damu kama ushahidi wa bikira hiyo ya bintiye iliyotolewa na kijana huyo aliyefika kijijini hapo akitokea dar pamoja na rafiki yake kwa lengo la kuwasalimia wazazi wa rafikie kisha mzee huyo wa kichaga akaendelea kuongea.
"papangu inaonesha umesoea kurupuni fipinti na kufiacha lkn huyu wangu utaoa aisee papaangu maana ni wewe umemtoa pikira na usipomuoa ukaniachia hapa hakuna atakayemuoa mbila pikira,sitaki cha mahari wala nini ninachotaka ni umuoe tu uende naye huko kwako dar".
Huku akiwa kajifunika na mashuka yaliyolowa damu kijana alijaribu kujitetea kwa kusema,
"lkn wazee wangu mimi nimepanga nikae hapa siku mbili tu kisha nirudi dar kuwahi kazini hivyo nipeni muda niweze kujiandaa wazee wangu".
Mjomba wa binti huyo aliyeonekana kuwa kijana miongoni mwa wanaume ktk kundi hilo lililofanya uvamizi akadakia kwa jazba.
"chalii acha kuongea upuuuh upuusi,hamna cha kujiandaa wala nini tena kwa taarifa yako tunachinja mbusi ya kiapo maana unaonekana mjanja mjanja lkn hiyo damu ya kiapo haina masihara chalii ukimkimbia tu huyu pinti au ukimuoa halafu ukawa na wanawake wengine au kumtesa utayaona makipu ya kiapo"
Mlolongo ulikua mrefu lkn kwa kifupi ni kwamba kijana huyo aliyekua na mchumba dar aliyemvalisha pete huku ikiwa imebakia miezi michache afunge ndoa na mchumbae huyo alijikuta akiwa hana jinsi bali kumuoa binti yule wa kichaga aliyefumaniwa naye kwa ndoa ya dharura iliyofanyika huko huko kijijini machame na kurudi dar akiwa na mke wake wa halali kabisa na sasa miaka imepita na wana watoto wawili.
Baada ya kumaliza kumuhadithia rafiki yangu kisa hiki akasema;
"dah!hata ingekua ni mimi nisingejuta kumuoa huyo binti maana asikwambie mtu bwana kuoa mwanamke bikira kuna raha zake maana mwenyewe unaanza kufungua kitu na box kikiwa cealed".
Kauli hii aliyoitamka rafiki yangu haikua mara ya kwanza kuisikia,nimeshaisikia mara nyingi sana tena na ninajua inasehemu kubwa ktk mila zetu za "kale" ambazo kila binti alitakiwa aolewe akiwa "kitu na box bin cealed aka bikira".
Hata hivyo pamoja na kuwa kauli hii nimeisikia mara lukuki lkn baada ya kuongea na rafiki yangu huyu nilijikuta nikiitafakari kauli yake baada ya yeye kuniaga.
Mawzoni mwangu nilikubaliana na kauli yake kwa namna moja au nyingine kwani
1.kama kila binti ataweza kujichunga na kuolewa akiwa na bikira basi hata maambukizo ya magonjwa kama ukimwi yasingekuwa makubwa kama ilivyo leo.
2.mimba za mashuleni zilizopelekea kina mama wengi kukatiza masomo yao huku waliowatwika mimba hizo wakisonga mbele huku kila dakika wakisema"wanawake bwana akili zao ndogo sana"zisingekuwepo.
3.dhambi ya zinaa iliyo machukizo mbele za mungu ingepungua.
4.n.k.
Nikiendelea kuwaza nilitamani siku moja mungu akinijalia kuwa na binti na yeye aolewe akiwa kitu na box kwani mwanamke mwenye bikira huonekana eti ana "thamani"kuliko asiyekua nayo sbb bikira yake ni "uthibitisho" tosha kuwa ni mwanamke aliyejitunza na mwenye kulelewa vyema asiye mapepe.
Nikiendelea kuwaza nilitamani binti yangu aje kuolewa akiwa na bikira kwa sbb tofauti na zile nilizozoea kuzisikia,mie nilijiambia mawazoni;
"kama binti yangu ataolewa akiwa na bikira ina maana atakua amesoma vizuri bila kuyumbishwa na wanaume wanaolaghai watoto wa kike wakiwa mashuleni na hivyo atakua na "thamani"kwani atakua ameweza kupata elimu ambayo ndio ufunguo wa mafanikio wa maisha ya thamani na kikubwa kuwa mbali na maambukizi ya magonjwa kwani bora mimba italeta mjukuu".
Hata hivyo niliendelea kuwaza juu ya suala zima la bikira na mazingira mazima ya maisha tunayoishi leo.
Enzi za mabibi na mababu zetu elimu pekee iliyotolewa kwa mtoto wa kike ilikua ni juu ya "kumlea mume"kwa heshima woga na unyenyekevu ikiwa na topic kama jinsi ya kumpikia mume chakula kizuri,jinsi ya kumnawisha mume mikono kabla na baada ya kula,jinsi ilivyo mwiko kumuacha mume kupeleka maji ya kuoga bafuni mwenyewe na jinsi ya kumuogesha kwa kisahani na maji yenye maua waridi na langilangi,elimu iliyomuandaa binti kuishi maisha ya kumilikiwa na mume na kumpandikizia imani kuwa ktk maisha yake hayo mwanaume ndiye bora na mwenye uwezo wa kufanya yote makubwa na yenye manufaaa hivyo aheshimiwe na kuogopwa kwani akikupa talaka "hutaweza" kuyafanya aliyokua akikufanyia.
Niliendelea kuwaza zaidi kuwa labda iliwezekana enzi hizo za mabibi na mababu mabinti wengi wakaolewa wakiwa bikira sbb waliolewa wakiwa wadogo sana baada tu ya kuvunja ungo huku wengine wakiwa hawana hata manyonyo.
Leo hii maisha yamebadili mkondo,elimu haina mke wala mume,pesa inatafutwa na mke na mume,ule umri ambao zamani binti tayari alishaozwa ni umri ambao binti leo yuko katikati ya masomo yake yenye kumjengea imani kuwa"hakuna tofauti yeyote ktk ubongo wa mwanamke na mwanamume na kwamba analoweza kufanya baba hata mama anaweza"
Leo hii ni wanawake wachache wanataka kuolewa wakiwa hawana nyuma wala mbele na kwa maana hiyo mpaka mtu aolewe utakuta ana umri mara mbili ya ule aliotakiwa aolewe enzi ya bibi na babu na ilihali mwili wake ukitoa changamoto za kufanya mambo ya wakubwa na hivyo kushindwa kuvumilia na kujikuta akipoteza "kitu na box yake" kwa boy friend.
Hata hivyo bado sielewi ni kwa nini mwanamke asiye na bikira apungue "thamani" na nilipoamua kuwaza kama mwanaume nilijiambia kuwa;
"ningekua mwanaume ningemdhamini mwanamke iwapo.."
1.ana mapenzi ya dhati kwangu
2.ana upendo na heshima kwake na kwa watu wengine wa aina zote.
3.mcha mungu.
4.mchapa kazi,mwenye uchu wa maendeleo na mwenye akili za kuzaliwa ktk kupambanua mambo.
5.mrembo kulingana na macho yangu.
Sbb kama nitathamini tu wale wenye bikira na kuwaona eti ndio waliojitunza,je wale wanawake ambao;
*aliolewa akiwa na bikira yake lkn mumewe akafariki baada ya wiki moja lkn bikira ilishatolewa na marehemu mumewe.?
*walibakwa na bikira zao kutolewa bila hiyari yao.?
*hana bikira ana sifa kama nilizotaja hapo juu?
*anayo bikira ni kitu na box lkn mvivu,hana akili za kuzaliwa,hana muamko wa maendeleo na havutii machoni mwangu?
Nilishawahi kusikia eti kuna makabila walikua wanawashona watoto wao ktk sehemu za siri ili tu wasijekupoteza bikira zao na kuiletea familia aibu,jambo ambalo ni unyama na lenye madhara makubwa.
Wapo eti mabinti ambao kwa kuogopa kupoteza bikira zao waliamua kufanya mapenzi kinyume ya maumbile huku sehemu za mbele zikiwa zimehifadhiwa kwa ajili ya atakayeoa tu ili siku ya harusi "ndoa ijibu".
Wapo ambao nasikia walinunua dawa zinazoweza kurudisha bikira na siku walipoolewa wakakutwa ni kitu na box wakati mji mzima unajua kua huyo binti alikua hatari kwa waume za watu lkn mume alimthamini kuliko hata yule aliyepoteza ubikira wake kwa mwanaume mmjoa tu.
Kitu kingine ambacho sielewi kuhusu hili suala la bikira,ni kwanini wanaume wao ni sawa kupoteza "ubikira wao" na thamani yao isipungue,tena ndio "inapanda"kadiri wanavyozidi kuipoteza maana utasikia wakiambiana"aah sema mzee watotoz naona umetoka kubangua" na wala hataitwa changudoa wala baba huruma wala maharage ya mbeya au fagio la city na wala hatakosa mke tena unaweza kumsikia akisema mwanamke atakayemuoa sharti awe bikira lkn sisi ukiwa"mamaa wa mababaz"utaitwa malaya,changudoa,jamvi la wageni mama teresa mama huruma na hakuna atakayetaka kukuoa.
Kwanini kama wanaume wanapenda kuoa wanawake wenye bikira na wao wasiutunze ubikira wao ili waje waoe wakiwa bikira na mke awe bikira,lkn la!wao ndio wa kwanza kwenda kuwarubuni wadogo zetu wa kike mashuleni na hata kuwarubuni wanawake wenye kujiheshimu na wenye misimamo kwa lugha tamu tamu na hata kwa uchumba hewa ilimradi tu wawaonje,tena wengine hujifanya hadi walokole wanapomuwinda binti wa kilokole.
Lingine ambalo sielewi,utakuta eti mwanaume anajisifia kwamba mie mke wangu nilimuoa na bikira lkn anaisaliti ndoa yake na wanawake wengine,sasa kama bikira ina thamani kuubwa kiasi hicho mbona haijatosha kuwatuliza wanaume hawa wasizisaliti ndoa zao!?
naielewa sababu ya kidini ila kuhusu hili lkn mbali ya kidini Sielewi kama huu ni ubaguzi wa kijinsia au ukandamizaji,imani tata au mawazo potofu maana ningefurahi kujua kama wapo wanaume wenye kujiheshimu kwa kuutunza ubikira wao ili aoe akiwa yuko"kitu na box cealed aka bwanaharusi bikira" kwani wengi ninaowajua wanasema eti wananoa misumeno huko na huku ili wakioa kitu kiwe kikali waweze kumridhisha mamaa.