Dhambi ya uwongo ndio kaburi la CHADEMA

Dhambi ya uwongo ndio kaburi la CHADEMA

Rationalizer

Member
Joined
Jul 12, 2013
Posts
46
Reaction score
19
nilijua chadema inashindana na vyama vingine kama vile udp, nccr-mageuzi, tlp, ccm na ccj na vingine vingi tu hapa nchini kwa kujinasibu kwamba ndicho chama pekee cha ukombzi kwa watanzania lakini hatimaye nikagundua kwamba chadema inashindana na uwongo ambao umeshaonesha dalili kwamba chadema inawahadaa watanzania ikiwa ndio mkakati wake wa kupendwa ili waaminiwe na kukabidhiwa dola.

ilianza kwa kutotii amri za mamlaka ya nchi huku ikifanya fujo, kusababisha mauaji ikipaza sauti haraka milithili ya mwanamke aliyemkaba mumeo kooni lakini eti anapiga kelele kuomba msaada akidai ananiua, ameniumiza, niokoeni na maneno mengine chungu mzima lakini mwishowe watu wanapojitokeza wanagundua mwanaume ndio kakabwa. Ndivyo ilivyo kwa chadema kuhadaa watanzania ni ulimwengu mzima kwamba wananyanyaswa na polisi, wanatishiwa kuuwawa, wanaibiwa kura na kadhalika na baada ya kugundua kwamba watanzania wameshawastukia, sasa wanatumia uwongo bila kujua kwamba ndio kaburi lao.

gazeti la chadema katika moja ya makala zake za leo iliyoandikwa na aliyejiita mwandishi wetu wakati jana huyu huyu mwandishi wa chadema ambaye mwongo, mzandiki na mvivu wa kufikiria tena anaejua kuwagawa watanzania kikabila, kidini na hasa kisiasa aliyeandika kwa kuwaaminisha watanzania kwenye mtandao wa jamii forum kwamba mh. Ole medeye (mb) ambaye pia ni naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi amewaagiza malaigwanani wakawaambie kinamama na vijana eti wawapinge wachaga kutokana na fujo za lema ambaye ni mchaga na wasimchague mgombea yeyote ambaye si mmasai katika uchaguzi wa kesho jumapili kata nne za mkoa wa arusha lakini habati nzuri kwa kimasai kuna msemo usemao "meeppoo esipata ngujit" ikimaanisha kwamba majani hata yawe marefu namna gani lakini hayawezi kuficha ukweli.

nasikitika kwamba watu wengi wamechangia mtandaoni tena kwa kumuunga mkono mpuuzi aliyeendika uwongo mtupu lakini niwasihii watanzania tusiwe wepesei wa kuhukumu bila kuchunguza hasa kwa vyanzo mbali mbali uhalali wa kile tunachodhani ni muhimu kuchangia mawazo.

Mwandishi alitaka kuwaaminisha watanzania kwamba malaigwanani walidanganywa wahudhurie mkutano wa kimila lakini eti ajenda ikabadilishwa na kuwa mkutano wa siasa kiasi cha kulazimu malaigwananani wampinge mh. Ole medeye. Alitaka pia kuwaaminisha kwamba wamasai ni wabaguzi na hawawathamini watzania wengine.

kwa kifupi, mimi nilihudhuria mkutano ule na si technical kama mwandishi alivyodanganya kwani wazee wale si wanafunzi wa technical bali eneo linaitwa oreteti loongaik ambayo ni sehemu maalum kwaajili ya mikutano ya mila za kimasai tangu enzi za mababu na si kila mtu anaweza kuingia bali ni wazee maarufu na viongozi wa rika mbali mbali za kimasai ndio tu wanaingia pale tena si kama sokoni bali kwa ratiba maalum kama bungeni vile.

nathubuti kusema mwandishi huyu wa chadema ni mwongo kwani ule ni mkutano wa kimila ambao mh. Ole medeye alihudhuria kwa haki zote za kimila na si kama mbunge wala naibu waziri, bali ni laigwanani kama malaigwanani wengine hasa ukizingatia arusha huezi kuwa kiongozi wa kisiasa tena kwa ngazi ya ubunge bila kusimikwa cheo cha kimila ambayo ndio msingi wa hekima. Mwandishi ni mwongo kwasababu ole medeye hakuuliza swali wala kuchangia mada yoyote iwe ya kimila wala ya kisiasa hivyo basi ni dhahiri kwamba mwandishi wa makala ile ndio anawagawa watanzania kwa ubaguzi wa rangi, ukabila, ukanda, kidini na hasa kisiasa kwa makala yake ya uwongo bila kujua watanzania popote walipo hawapendi kutenganishwa kwa misingi hiyo.

wamasai wangekuwa wabaguzi kama mwandishi alivyosema,basi wasingewakaribisha watanzania wengine bila kujali ukabila na wakawauzia ardhi na bado wanawauzia, wamasai wasingeoana na makabila mengine tu mengi ya kitanzania, wamasai wasingekuabali kushirikiana na watanzania wengine katika shughuli zote za kijamii, kiuchumi na kisiasa na wasinge wachagua viongozi wa kiasiasa mfano mh. Godbless lema na madiwani wote ambao si wamasai na waliondolewa na chadema hapa arusha. Mbona wamasai wamejaa kwenye dini na vyama vyote vya siasa hapa nchini?

mwandishi huyu ni tishio kwa usalama wa nchi, umoja na mshikamano wa watanzania hivyo anastahili kuwaomba radhi wamasai na watanzania kwa ujumla kwani akifanikiwa kuwagawa wamasai na wachaga, basi ataendeleo kuwagawa makabila mengine na nchi haitabaki sala. Kama chadema inamtumia mtu kama huyu ili kupata huruma ya kupigiwa kura, basi imenoa kwani uwongo ulioandikwa jana tarehe 12/07/2013 na leo ukaandikwa katika gazeti la mtanzania daima si tu itawafanya watanzania waione jamii forum na gazeti la tanzania daima kwamba ni vyanzo vya habari zisizofaniwa uchunguzi, bali pia itawafanya watanzania wasizisome habari mbali mbali katika vyanzo nilivyotaja.

Mwandishi huyu aogopwe si tu kama fujo za chadema, bali pia kama mauaji ya kimbari ya rwanda na burundi.

Mwisho, napenda kuwahakikishia watanzania kwamba huo ni uzushi na mwandishi apuuzwe kwani lengo lake ni kuwagawa watanzania kwa misingi ya ukabila, udini, ukanda ila namsihi awaache watanzania wamchague kiongozi yeyote wa kisiasa wanayemuona anawafaa ili kiongozi huyo asipotekeleza majukumu yake kama anavyoahidi katika kampeni zake basi waliomchagua wajilaumu wenyewe lakini isitokee kiongozi mwenye hekima na maadili kama mh. Ole medeye akapakaziwa uwongo kama huo.

Mungu wabariki watanzani, mungu ibariki tanzania, mungu ibariki africa !


 
Kawaida ya hilo gazeth, wala mimi si relai kwenye habari km hizo
 
Habari za magazeti ya cdm huwasiziamini kabisa kwani waandishi wake ni washabiki tu. Hawaandiki habari kwa ufasaha wake na kubalansi stori zao bali huandika kwa mlengo wnaotaka wao. Kifupi ni wakabila na wadini,hivyo na chama cha cdm ni cha kuogopwa kama ukoma. Pia cdm huitumia JF kama chombo chao cha propaganda,tazama habari zinzopewa kipaumbele humu niza cdm tu. Hata huu uzi hapa hautadumu. JF haiko tayari kuona cdm inasemwa negative,utashangaa humu ukumbini ni habari za cdm tupu na washabiki wake wanatoa kejeli kwa wengine na wanaachwa tu. Jamani haya ni majanga.
 
Kwani ni uongo mbona kwenye ile video ya kwenye yotube anaomekana waziri mzima anautubia kwa lugha ya komasai na tepats watu wa kutafsiri .nikweli anasema wachaga waondoke arusha je kwa wale ambao wameoa ama kuolewa na waarusha je nao wafukuzwe.
 
Pole sana mkuu , labda kwa faida yako tu ni kwamba kila hila iliyopangwa , inayopangwa au itakayopangwa itafichuliwa na wazalendo , mkutano wa kimila ? Why now ? Pole sana maana hakuna ambacho ccm itaambulia kesho , inauma sana lakini hiyo ndiyo hali halisi , damu mliyoimwaga Arusha itawagharimu milele .
 
Tanzania Daima ni gazeti la udaku.
 
Nashangaa sana watu, wanasema damu mlimwaga arusha itawagarimu, mimi si mwanachadema ila iwe cdm au ccm kila mtu aliyehusika kupanga anajijua mwenyewe na kila tone la damu itawasumbuwa mpaka kizazi chako, watu wengine wanaandika damu damu, kumbe yeye ndio muhusika tusubiri mungu yupo, hata usipokamatwa mungu atakuwajibisha kwa kumwaga damu za watu,wasio na hatia, na asilimia 95 ninaamin ni cdm ndio walifanya, damu zitawafuata mpaka watoto wenu,
 
Nilishasema hivi vyama viwili vitatufikisha pabaya sana

"To know the enemy is half the victory"
 
Hapo kwenye RED kama ulihudhuria mbona umejikita kupinga habari iliyochapishwa na gazeti la Tanzania Daima lakini haujaeleza hicho kikao kilizungumzia nini? na wakati na wewe ulikuwepo
 
]
Tanzania Daima ni gazeti la udaku.
[VIDEO]http://www.youtube.com/watch?v=70ffU1xIpN0[/VIDEO
Ni kwelii kaka unafaaa sanaa kuwa mnafiki.. Huyu madeye alishiriki kwenye kikao cha kimila kilichotangaza chuki dhidi ya wachagga na video ipo hapaa.. Ole Medeye; atangaza vita na wachaga asema watapigana kwa silaha zote kuwagoa Arusha - YouTube zaidi ya hapoo... Mnashiriki kujenga chuki za kikabila kwa mgongo wa propaganda za CCM.. HAYA YANA MWISHOO Ole Medeye; atangaza vita na wachaga asema watapigana kwa silaha zote kuwagoa Arusha - YouTube
 
TANZANIA DAIMA ni gazeti la UDAKU.
Ni kwelii kaka HATA HII VIDEO NI YA UDAKU..AHAHAHAHAHAHAAAAAA..... unafaaa sanaa kuwa mnafiki.. Huyu madeye alishiriki kwenye kikao cha kimila kilichotangaza chuki dhidi ya wachagga na video ipo hapaa.. Ole Medeye; atangaza vita na wachaga asema watapigana kwa silaha zote kuwagoa Arusha - YouTube zaidi ya hapoo... Mnashiriki kujenga chuki za kikabila kwa mgongo wa propaganda za CCM.. HAYA YANA MWISHOO Ole Medeye; atangaza vita na wachaga asema watapigana kwa silaha zote kuwagoa Arusha - YouTube
 
Mkutano wa kimila haujaanza leo au kipindi kihi cha uchaguzi bali ni mwendelezo wa mikutano ya kimila ambayo Ole Medeye na malaigwanani wenzake wamekuwa wakihudhuria na siku ukimuona Mh. Lowassa akiingia huko, najua hutachelewa kusema anasaka urais isipokuwa nikuambie Ndugu yangu na mtanzania mwenzangu kwamba Lowassa ni kiongozi wa Mila za Kimasai Africa Mashariki.

Wamasai wana taratibu za kuishi na hiyo imesaidiwa sana na mila na desturi zinazotenganisha rika kwa rika ili kujenga heshima katika jamii na kwa kuwa wewe huelewi na hujui kwamba huelewi na ukieleweshwa hutaki kuelewa basi akili yako inakimbilia uchaguzi ambao hata hivyo maamuzi yake yako kwa watanzania hasa wapiga kura wa kata husika.

Sijui ni bangi na viroba vinawaongoza sielewi. Hekima ni hulka ya mtu na si shuruti hvyo usisubiri somo la hekima darasani maana utapitwa na wakati.
 
Tanzania Daima ni gazeti la udaku.

Ktk magazeti hapa Tz ukichelewa kuamka mpaka saa nne haukuti kopi hata moja kwa wauza magazeti ni DAIMA 2weni wakweli haswa kesho.Ayo mengine hayauziki.
 
Hapa tulipofika sasa patamu.
CCM ipo radhi kulimaliza taifa hili kwa uchu wa madaraka.
 
Inaelekea wewe hujui technology inavyofanya kazi, hivi picha za kivita unazozionaga unadhani zote ni za kweli? Hebu tumia sehemu ndogo ya ubongo wako kufikiri kwa upana. Nikuulize, katika nchi inayotawala kwa misingi ya demokrasia na utawala bora kama Tanzania, Mh. Rais pekee ndio mwenye mamlaka ya kutangaza vita na mtu yeyote akifanya hivyo ni kosa la jinai na anastahili kuburuzwa mbele ye sheria?
Je Polisi wameenda likizo ili usema Ole Medeye katumia hiyo nafasi ya kutangaza vita? Huo ni uzushi kama ule wa jana katika jamii forum na leo katika gazeti la udaku la Mtanzania Daima.

Kwanza Mtanzania halisi hawezi kuwa hivyo mnavyofikiri kwa maana hiyo gezeti lenu mngeeliita MChadema News.
 
Back
Top Bottom