CARLOS MAJURA
Senior Member
- Mar 7, 2013
- 192
- 69
Kama vile ni njama za kumkomoa mbunge wa UKerewe, hakimu wa wilaya hiyo haonekani ofisini ikwa ni baada tu ya kumfutia dhamana mbunge huyo. Kwa mujibu wa taarifa ambazo zimethibitishwa na watu mbali mbali (wakiwemo watumishi wa mahakama wilayani ukerewe) hakimu huyo alionekana akipanda meli kuelekea Mwanza siku ya tarehe 7.11.2013, ikiwa ni siku moja baadaya kumfutia dhamana mbunge Machemli. Taarifa ambayo imetolewa na katibu wa chadema wilaya ya Ukerewe Bw Poul Mfumu inasema kuwa wao walikamilisha masharti ya dhamana tangu ijumaa na walipokwenda mahakamani waliambiwa hakimu amesafiri na jalada la kesi halionekani, hivyo warudi siku ya Jumatatu. Hata hivyo leo waliporudi mahakamani hadithi imekuwa ile ile kwamba hakimu yuko safari. Katika sura hii sasa watu tunaanza kujiuliza Je, hivi sasa siasa zimeingia ndani ya Vyumba vya Mahakama?