Dereva chukua tahadhari kwa sasa

Dereva chukua tahadhari kwa sasa

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
15,202
Reaction score
25,378
Hali inazidi kuwa mbaya hasa katika suala la rushwa, hapa Mbezi -Inter Chick kuna askari usalama barabarani wana tochi na wanazikamata gari hovyo.

Week ya nenda kwa usalama ikiwa inavuta kasi hawa jamaa nao hawalazi damu wakiwa barabarani, badala ya kutoa elimu wao wanatumia opportunity na kufanya yao.

Inavyoonekana hata madereva wanaokamatwa hawajui sheria za mwendo kasi wawapo mjini, hata sehemu nyingi hakuna vibao vya speed limit, ndipo inapelekea shida na kulipa fake fine zisizofika hazina.

Nawasilisha
 
Ni mfumo mbaya uliokuwepo muda mrefu.
Wananchi hatupewi elimu katika mambo mengi ili hao wanajiita serikali watunyonye mpaka damu kwa kisingizio kuwa hatufuati sheria.Nchi hii ina kila aina ya uchafu na umefumbiwa macho sababu ni familia ya kambale yani baba ana ndevu,mtoto ana ndevu na mama ana ndevu.
Kwa hiyo wote walewale.
Tubadilishe utawala huu wa kambale oktoba 25.
 
Cha ajabu wana tochi sehemu ambayo hata haistaili yaani ni kichekesho na hawana soni, sijui tumeumbwaje hasa hawa traffic.
 
Hawa maaskari wa usalama barabaran ni hovyo yanapenda rushwa ni balaa
 
Sasa wenye pikipiki ndio utawaonea huruma.Wanakamatwa ovyo kisa juzi walikuwa mstari wa mbele kumshabikia Lowassa
 
kama mtu ulisomee udriver hautakiwi kukimbia above 50km/h. apo police they are right
 
kisheria unapoingia mjini au ukiwa mjini speed limit ni 50km/h
 
Pale Interchick kuna kibao kinachokuamuru kwenda 50kmph, kama hukukiona ni uzembe wako na hustahili kuwa dereva. Nakushauri fanya safari ndefu kwenda mikoa ya bara ndo utajua vizuri matumizi ya hivyo vibao TODAYS
 
Last edited by a moderator:
ile ni highway hamna kibao cha speed limit

Kwa hiyo unadhani highway haina speed limit? mahali popote ambapo barabara kuu imepita kwenye makazi ya watu spidi ni 50km/hr. Haijalishi ni highway au laa.
 
Ha ha ha.. Tunalalamika askari kuchukua rushwa lakini mara nyingi sisi raia tunafanya makosa ya kizembe sana... Hivi dereva unalalamika hujapewa elimu kuhusiana na sheria za barabarani, leseni uliipataje..? Unategemea askari ndo akupe elimu..? Turudi shule madereva wote.. Tuzijue sheria za usalama ili tuzifuate na kuepuka kutoa rushwa..
 
Comrade, nashukuru kwa ushauri wako, ila naweza kukupa pole maana nina ufahamu kuhusu hii kitu uliyonipa ushauri, kwa ufupi mkoa ambao cjafika ni manyara na rukwa sasa sitaelewa unaongelea barabara ipi hapa Tanzania.
Pale Interchick kuna kibao kinachokuamuru kwenda 50kmph, kama hukukiona ni uzembe wako na hustahili kuwa dereva. Nakushauri fanya safari ndefu kwenda mikoa ya bara ndo utajua vizuri matumizi ya hivyo vibao TODAYS
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom