Chozy
Senior Member
- Aug 22, 2012
- 172
- 47
Siku za hivi karibuni niliweka uzi wa kutaka mchumba pale UCC (UDSM) lakini nikautoa baada ya kuona nasumbuliwa na wadau (pm) nikafanya maamuzi ya kumrudia mpenzi wangu tuliyebwagana mwezi Oct 2014 kutokana na ubabe wake katika maamuzi ya pamoja na kutaka kunitalawa kifkira na kiuchumi pia; nilifanya maamuzi ya kumrudia kwa kuhofia kuanza kuzoea penzi jipya alihali yeye tayar nimeshamzoea pamoja na madhaifu yake. Nilifika home kwao kwa muzungumzo zaidi na kisha kukubaliana twende kituo cha afya tupime HIV, tumefanya hivo na wote tupo salama sasa kilichoniumiza zaidi ni pale alipohitaji kumuona daktari kwa tatizo jingine, baada ya kuingia chumba cha daktar masaa yaliyoyoma na mm nikimsubiri ktk kiti cha wagonjwa nikapatwa na hofu kinachoendelea humo ndani kibaya zaidi wahudu wa mapokezi na chumba cha dawa walikuwa wakitizamana na kisha kunitizama mm nilipokaa alihali kuna kitu fulani walikuwa wanaashiria; badae akatoka nikalipa bill na kumrudisha home kwao na mm kusepa kwa hasira(Maumivu)
Msaada wana jf, kweli kwa mazingira haya palikuwa na usalama kweli!? Japo nimemuuliza akadai dk alikuwa anachukua maelezo.
Nawasilisha: utani, kejeli havitanisaidia plz.
Msaada wana jf, kweli kwa mazingira haya palikuwa na usalama kweli!? Japo nimemuuliza akadai dk alikuwa anachukua maelezo.
Nawasilisha: utani, kejeli havitanisaidia plz.