Deleted Files/Folders Katika Computer, Hupelekwa Wapi?


Limit ya kuhifadhi data ipo kama hautafuta mafaili. Kwa ufahamu wako, Hdd za sasa hivi ni kubwa mno, hakuna 5gb tena!

Hard disk lifespan yake ni wastani wa miaka 5.
kwa hivyo usinunue hard disk used kamwe.

hard disks zina motor ambazo zinazunguka kama mara 5400, 7200, 15000 kwa dakika. Hivyo baada ya muda zinachoka.

kuna aina mpya ya storage inaitwa SSD. Solid state disk. inatumia technology ya flash disk kutunza data, ndo nzuri kwa sasa, haichoki mapema na inahimili mikimiki, haitumii motor

kuwa slow kwa computer yako haisababishwi na kujazwa vitu Kwenye computer.! No! Unless imejaa sana.

inasababishwa na program zinazojaza RAM yako na zile zinazo ifanya processor iwe bize muda mrefu.

Huwa zinaingia pamoja na program unazoweka. nyingi zina autostart. Nyingi ni za kidaku... huku zikijinadi kuwa zinafanya auto-update. ukweli ni kuwa zinapeleka information kadhaa kwa walio zitengeneza na hata kwengineko.... watch out!!!!
 

Hapo kwenye red, ni sawa usemayo lakini ni watu wangapi wanaweza kununua a brand new computer/Lap Top or the like kwa maisha haya ya kibongo?

Nimeshuhudia hapa hapa jamvini baadhi ya members wakitafuta used Lap top za kununua kwa bei ya Tshs. Laki tatu! Pamoja na hayo bado kuna tatizo kubwa la uelewa katika tasnia nzima ya IT kwa maana tu hata ile elementary knowledge hasa kwa wale wa mwaka 47;

Kuna member mmoja hapa ktk uzi huu amesema kuwa anafanya PhD. kuhusu suala lililoulizwa hapa; sina hakika kama alikuwa anatania au la! Kapotelea wapi sijui.
 
Mkuu malizia basi hzo asilimia 2 alizobakisha

umeona pekundu hapo chini? Haikwepi kuandika data katika sector hiyo... except inategemea na mzigo ulionao computer kwa muda huo(processes), position of the hard disk head and the closest free space iliyopo.. hata kama itakuwa ndo hiyo ambayo imefutwa hiyo hiyo sekunde

Lol! Unapofuta file haliondoki katika sector lilipohifadhiwa, kinachobadilika ni entry tu, OS yako inabadili anuani kutoka say "my documents" kwenda "trash",

hivyo sector ya hdd lilipohifadhiwa hilo file inakuwa bado na kitu kilekile kama kilivyohifadhiwa kuondoa anuani tu. Hivyo basi, uki-empty recycle bin yako unafuta hata hiyo anuani ya pili "recycle bin"

hivyo inakuwa ngumu kulitrace file lako kiurahisi, lakini si kwamba file limetoweka kabisa, linabaki palepale kwenye sector ileile, na computer ita-asign jina maalum katika file lako,

computer itakwepa kwa kadri iwezekanavyo kuandika data nyingine katika sector hiyo,
hivyo katika muda huo ukitumia software maalum inalocate file lako na inaweza kulirejesha kwa kulipa anuani nyingine!
 
Siko mbali sana na wengine waliochangia hapa; labda tu kwa ufupi: User anapoamua ku-delete file, computer uondoa table contents ktk location ya file, kimsingi pale ktk location uingia a blank card ya file husika.

Sababu hasa ya kufanya hivyo, ni kwamba computer ingetumia a lot of time & power kwenda kila location na kufuta file. Pia wakati mwingine kuruhusu file au folder kuwa recovered.

Mkuu Iselamagazi, computer haiwezi kujaa deleted files kamwe; hii ni kwa sababu Operating System (O/S) marks the location of that deleted file 'free' - hivyo file lingine linaweza kuwa copied to that free location.

In general, deleted files don't go anywhere. They remain on the disk exactly as they were until they happen to get overwritten. When they are deleted, a link to it is simply removed from the file system structure.
 

mkuu, maelezo unayosema ni rahisi ndio magumu zaidi, yaani no mtiririko wala collocation na hiyo mifano ni irrelevant kabisa naomba huyo uliempa 98% umpe 100% na wewe ujipe 05% kwani umetuchanganya zaidi!
 

Lol! nimekusoma mkuu. To what i know ni kwamba computer itaandika katika un-used sectors kwanza na zikijaa ndiyo inaanzakuandika over used sectors! Nadhani nahitaji kujikumbusha kidogo. Pamoja sana.
 

na akili sana wewe. Mi nilishndwa kuyaweka haya mawz yang kt maandsh kama ulivyofnya wewe kwa maana ya kila m2 kukelewa
 
Last edited by a moderator:
mkuu okaoni, ameuliza kuwa Deleted SMS ktk mobile phones nazo uishia wapi? Naona jibu bado halijatoka. Mwenye ufahamu alete hapa.
 
Last edited by a moderator:

ni kweli kabisa alichosema Mlamoto hapo juu..hdd ina limit yake (size) pale tu endapo hutafuta kila unachoingiza sababu hdd itafanya allocation ya data kwa empty addresses zote (ndo hiyo hdd size) ambapo yatakuwa yanaweza kuwa accessed then ili uongeze data zingine ni lazima hdd ifute reference path ya data iliyopo ndani tayari na kuifanya iwe empty address ili data ingine ije ipewe adress hii..

na lile file lililokuwepo kurudishwa nyuma huko mahali ambapo only specified program inayoweza kulifikia(recivery program) ndo itaweza kuliaccess na kuipa adress ingine (kama hdd yako bado ina free space)..

na kama nilivyosema awali kadri unavyozidi kuweka na kufuta mafaili ndivyo unavyozidi kupoteza uwezekano wa kuyapata mafaili ya mwanzo kuwa deleted sababu yanazidi kwenda mbali zaidi na hapo ndipo utatakiwa kuwa na program zenye nguvu zaidi ya kurecover ili iweze kuyafikia...

So hdd haitajaa kama utakuwa unaweka mafaili na kuyafuta ila tu utaongeza uwezekano wa hdd kufa endapo utakuwa uanfanya hiyo weka toa mara nyingi zaidi ya matumizi ya kawaida ya pc ..

mfano we kila baada ya dakika moja una copy file to hdd the una lifuta then uancopy then futa...yaani we ikiwa kazi ndo hiyo tu hdd yako haitadumu kama mtu yule anayefanya hivyo katika matumizi ya kawaida...
 
Ukifikiria kwa kina sana naweza ungana na wale jamaa aliyewahi kusema kuwa anaweza Kibadili kihifadhi kumbukumbu na kuweza kuhifadhi mafaili bila ukomo.

Kwa kuwa mafaili yaliyo futwa huwa tu yameondolewa ktk ukurasa wa mbele wa Tarakirishi yako. Kwa nini tusiweze kuhifadhi mafaili hayo badala ya kuyaficha?

Ni wazo langu tu
 

Move sio sahihi kwa kuwa hakuna movement yoyote ya files inayotokea file zipo pale pale kwenye HD, ni kwamba Operating system inaficha file mtumiaji asione na pili inaweka alama kwenye HD kuwa lile eneo la file ni ruksa kuhifadhiwa kitu chochote kama ikihitajika.

Pia ni muhimu kidogo kuelewa kuwa faili sio lazima lihifadhiwe zima sehemu moja kwenye HD kipande kinaweza kuwa mwanzo kipande kingine katikati na kingine mwisho hii inaitwa fragmentation na ina faida na hasara zake.

Pia nimeona kuna comments za unaweza kuiua drive ukicopy sana or something hili halina ukweli practically, so usiogope kuitumia computer yako kivyovyote vile ila hakikisha unabackup files za muhimu (hasa online au kwenye DVD) maana HD zinaweza kufa muda wowote bila sababu.
 
Mkuu Kang, I like your comment!
 
Last edited by a moderator:
mkuu, maelezo unayosema ni rahisi ndio magumu zaidi, yaani no mtiririko wala collocation na hiyo mifano ni irrelevant kabisa naomba huyo uliempa 98% umpe 100% na wewe ujipe 05% kwani umetuchanganya zaidi!

Pole tunatofautiana! . Hata darasani uelewa unakuwa hivyo! wengi wamenielewa na watanielewa. Ukweli ndio huo! punguza jazba!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…