DCI Manumba: Tumejiandaa

DCI Manumba: Tumejiandaa

Wakati wa Jeshi la Polisi la Tanzania likisema linafuatilia taarifa za vitisho za kundi la Al-Shabaab la Somalia za kushambulia, Mtanzania mmoja, Vedasto Nsanzugwanko ambaye alijeruhiwa kwenye shambulio la Kenya ameelezea yaliyomkuta.


Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba alisema jana kuwa wameanza kufuatilia kwa undani taarifa zilizozagaa katika mitandao ya kijamii kwamba kundi la Al-Shabaab linajipanga kuishambulia Tanzania na Uganda.


DCI Manumba alikiri kusikia taarifa hizo na kusema kuwa Jeshi la Polisi limeanza kufanya uchunguzi wa kina: "Siwezi kukueleza ni uchunguzi wa aina gani tutakaofanya, hiyo ni siri yetu."


Hata hivyo, Msemaji wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), Meja Eric Komba alisema kuwa kuna uwezekano taarifa hizo zikapikwa na wajanja wachache kwa ajili ya kuwajengea hofu wananchi.


"Taarifa za kwenye mitandao wakati mwingine ni uzushi mtupu… kuna kipindi ziliwekwa taarifa za uongo zinazohusu jeshi hili," alisema.


Alipotakiwa kutoa msimamo wa jeshi hilo iwapo taarifa hizo zitakuwa na ukweli alisema, "Jeshi tuko tayari kwa jambo lolote."

source: DCI Manumba: Tumejiandaa - Kitaifa - mwananchi.co.tz

My take: Ni kwa neema za Mungu tuu ndio mpaka leo hatushambuliwi lakini si kwa uimara wa jeshi la polisi.

Picha chini ni askari maalumu wa kupambana na ugaidi. picha ya kwanza akimpa escort mtuhumiwa wa ugaidi.
Picha ya pili askari wetu shupavu akidhibiti uhalifu.
attachment.php

Nimelipenda hilo bullet proof jacket la huyo askari wa pili hapo chini. Aliyebuni anitafute nimpe tuzo.
 
Polisi yetu imekuwa kama chama cha siasa.
Na yeye anataka watu watambue uwepo wake.
 
Kiongozi!

Serikali hovyo, inazaa watendaji hovyo kabisa. Hivi huyo anaye sema tumejiandaa anajua anacho kisema au ni ili mradi waTanzania wasikie kwamba kiongozi wa Taasisi flani ya serikali amesema?

hivi pale Ubungo terminal kuna usalama gani kama watu wanaamua kufanya yaliyo tokea Nairobi? Ni maeneo gani hapa Tanzania ambayo yanakusanya watu wengi, panafanyika ukaguzi kiasi kwamba ana sema tumejiandaa? Kama vibaka waliwahi kuingiza na kutapeli watu pale Magogoni bila kizuizi, unategemea nini kwenye maeneo ya kawaida?!!

Asilete mzaha na hili jambo kabisa. Labda kama wamejiandaa kwa upande wa Magogoni, lakini huku kwetu dud pishana kila siku, sijaona lolote la kuwazuia hao maharamia.

hao wanamgambo tulio nao kweli watamudu?
 
Mnaoubisha kauli za Majeshi yetu kujipanga subilini tarehe 10/10/2013 muone si mmeisha ambiwa na viongozi wenu mfanye mazoezi kama al shababu walivyoanza?Mimi naunga mkono kabisa kuwa majeshi nyetu yako vizuri sana na tuko salama sana.Mashabiki wa Chadema,CUF na NCCR watakiona kilichomnyoa Kanga manyoa siku hiyo waliyopanga kuleta vurugu nchini kwetu.Jeshi fanyeni kazi yenu CCM na Watanzania tunatambua umuhimu wenu.VIVA TANZANIA.
 
Jamani mm natoa ushauri hivi kwann vijana wa jkt wasiende kulinda pale magogoni
 
Back
Top Bottom