DC wa Lushoto Azidi Kuweka Watumishi Lupango

DC wa Lushoto Azidi Kuweka Watumishi Lupango

MTA1

Member
Joined
Jun 1, 2013
Posts
89
Reaction score
11
Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Bw. Mwanga amempeleka polisi mtumishi wa halmashauri Bw. Mohamedi Semkamba kwa kosa la kuchelewa kuondoa vifaa vya mwenge. DC alikasirishwa na kitendo cha Bw. Mohamedi kuchelewa kuchukua vifaa vya mwenge, ingawa Mohamedi alichelewa sehemu ya tukio kwa vile alikuwa anaokoa gari la serikali lililotaka kuungua moto. Mara alipofika pamoja na utetezi wote, DC aliita askari wa polisi na kutoa amri ya kumweka chini ya ulizni wa polisi hadi atapotoa amri nyingine.
DC huyu tangu afike Lushoto amekuwa ni mbabe anayependa kutukuzwa na wafanyakazi wote wa serikali wilayani Lushoto; tukio hili ji mwendelezo wa uvunjwaji wa UTAWALA BORA, SHERIA na matumizi mabaya ya madaraka kwa mfano ni yeye DC kwa ushirikiano na RC Chiku Galawa siku za karibuni walimweka lupango DMO kwa kosa la kunywa maji ya chupa mbele yao. wakidai ni kitendo cha dharau kwa viongozi wake. Pia DC amewahi kujaribu kumweka Lupango, DED na Mwanasheria wa Halmashauri ya Lushoto.
 
Ndo raha ya kuwa kiongozi wa ccm, unakuwa demi-god...
 
Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Bw. Mwanga amempeleka polisi mtumishi wa halmashauri Bw. Mohamedi Semkamba kwa kosa la kuchelewa kuondoa vifaa vya mwenge. DC alikasirishwa na kitendo cha Bw. Mohamedi kuchelewa kuchukua vifaa vya mwenge, ingawa Mohamedi alichelewa sehemu ya tukio kwa vile alikuwa anaokoa gari la serikali lililotaka kuungua moto. Mara alipofika pamoja na utetezi wote, DC aliita askari wa polisi na kutoa amri ya kumweka chini ya ulizni wa polisi hadi atapotoa amri nyingine.
DC huyu tangu afike Lushoto amekuwa ni mbabe anayependa kutukuzwa na wafanyakazi wote wa serikali wilayani Lushoto; tukio hili ji mwendelezo wa uvunjwaji wa UTAWALA BORA, SHERIA na matumizi mabaya ya madaraka kwa mfano ni yeye DC kwa ushirikiano na RC Chiku Galawa siku za karibuni walimweka lupango DMO kwa kosa la kunywa maji ya chupa mbele yao. wakidai ni kitendo cha dharau kwa viongozi wake. Pia DC amewahi kujaribu kumweka Lupango, DED na Mwanasheria wa Halmashauri ya Lushoto.
Dah........................,siku zake zinahesabika!
 
Kwa Lushoto mnyoshwe tu na ikiwezekana mchapwe hata viboko. Si ndo ninyi wanazi wa CCM? Nyie ni wale mnaorudisha harakati za ukombozi nyuma. Mkome na CCM yenu.
 
Kwani watu wa TANGA siku hizi yale mambo mambo wazee wameacha na wameokoka wote nini? Huyo kazi yake ndogo tu jitahidini muwaone wazee wa Tanga
 
hii ni kali - nizaidi ya enzi za Hitler au Mobutu!!!
 
WAKATI MWINGINE UNAWEZA KUNYANYASWA SIYO KWASABABU UNAONEWA, BALI NI KWASABABU UMEWAPA WATESI WAKO HIYO FURSA.. NI LAZIMA TUDAI UHURU WETU KWA NGUVU KWANI HAKUNA HATA SIKU MOJA WATAUTOA UHURU HUO KWA KUPENDA...rejea maandika ya martin luther king jr
 
Wewe naona unachuki binafsi,huyu dogo mimi namfahamu sana na kwa taarifa yako sio mkurupukaji,alishawahi kuwa askari magereza akaona haimlipi akaamua kutemana na ajira akawa anasimamia shughuli za kaka yake so ni muelewa na hana tatizo,nadhani kinachokuumiza wewe ni kwamba dogo anaumri mdogo na hata kuoa nadhani bado labda ndo anashughulikia hilo,sasa wewe wivu ni umri wako umehsaenda na hauwezi fikia aliko huyo dogo,naomba uache kijana achape kazi please
 
Hizi ni shutuma za CHADEMA ambao wameshindwa kuivunja ngome za CCM mkoani Tanga
 
Back
Top Bottom