DC nusura amsweke rumande padre

DC nusura amsweke rumande padre

Paroko Msaidizi wa Kanisa Katoliki parokia ya Chumbageni, Padre James Kabosa ameponea chupuchupu kuswekwa ndani na Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego kwa madai ya utovu wa nidhamu.
Chanzo: Nipashe Jumapili

Mkulu alikwisha sema "...ukuu wa Wilaya hausomewi...", ni kuteua kwa vigezo unavyo ona vinafaa, iwe dini, ndugu hata ch*pi, bora anapewa kazi maalumu atekeleze! Huyu Halima anatekeleza maagizo ya bosi wake!
 
Kama mtu aliteuliwa kwenye post fulani kwa vile yeye ni dini fulani na ana maelekezo maalumu juu ya mtazamo wa dini fulani toka kwa boss, tusitegemee jipya hapo.

Hongera baba Askofu kwa kuchukua hatua na kuinuka toka ofisini kwako japo najua una majukumu makubwa ya kiofisi na kulishughurikia hilo, nadhani huyo mkuu wa wilaya amejua na hatarudia tena kufanya mchezo wa kihuni juu ya kanisa na bila shaka ataomba ahamishiwe kwingine.

Wateule wa rais badilikeni, mkiendekeza udini hapa kwetu mwisho mtaumia ninyi wenyewe na kuabika, tumikieni watanzania wote bila kuangalia imani zao nk.

Anasema alipomfuka Padre hakujua kuwa ni kiongozi wa dini, hii inamanisha kwake ni halali kuwafukuza raia wengine, ni mbaguzi na huyu kwa serikali makini anasitahili kufukuzwa kazi.
 
fikra ngumu;

mahali popoote duniani ambapo kanisa limestawi jamii husika lazima iwe maskini wa kutupwaaa. Rejea kisa cha askofu oscar romero wa amerika ya kusini ambako kanisa limeshika hatamu na akaanzisha " liberation theology " lakini alipingwa hadi na papa kutoka vatican....kanisa halikutaka jamii ile ikombolewee, alikufa katika mazingira ya kutatanishaa sanaaa.. !

Kanisa pia halitaki jamii ya ki tanzania ikombolewe na umaskini !

acha fix kama avatar yako utaikomboa jamii bila elimu???au kwa kuwajaza ujinga badala ya kuwajengea uwezo??
 
FIKRA NGUMU;

Mahali popoote duniani ambapo kanisa limestawi jamii husika lazima iwe maskini wa kutupwaaa. Rejea kisa cha Askofu Oscar Romero wa Amerika ya kusini ambako kanisa limeshika hatamu na akaanzisha " Liberation Theology " lakini alipingwa hadi na Papa kutoka Vatican....Kanisa halikutaka jamii ile ikombolewee, Alikufa katika mazingira ya kutatanishaa sanaaa.. !

Kanisa pia halitaki jamii ya Ki Tanzania ikombolewe na Umaskini !


I doubt your reasoning capacity, jaribu kufanya analysis kwa utulivu sana - maeneo kama mtwara, lindi, tanga na yale unayoyafahamu wewe then angalia na hicho ulichokiandika, usichukue sample ya maeneo kama dar ambayo hao walioendelea unaowazungumzia ni wahindi na waarabu, take your fellow africans uone. Tuache ushabiki usio na maana, shame shame shame on you
 


Kuhusu chanzo cha tukio hilo, Kiule alisema ni kutokana na mgogoro wa ardhi wa eneo la wazi lililogawanywa na diwani wa kata ya Nguvumali, Selemani Mhina (sele boss) CCM, lililopo mbele ya kanisa la Kigango cha Majani Mapana kinyume cha sheria za ardhi.

Alisema kanisa katoliki lilishaomba eneo hilo zaidi ya mara mbili kwa Jiji la Tanga na kujibiwa kuwa ni eneo la wazi na lakini lilitolewa kwa wafanyabiashara kwa madai kuwa ni agizo la mkuu wa wilaya ili kujenga mashine za kusaga nafaka.

Kwa upande wa padre Kabosa alikiri kupatwa na kadhia hiyo lakini alidai kuwa tayari suala hilo linashughulikiwa na viongozi wakuu wa kanisa hilo kwa hatua zaidi za kurejesha amani na mshikamano ulioonekana kukosekana.
Naye Mkuu wa wilaya, Dendego alipotakiwa kuelezea shutuma hizo alikiri ujio wa padre Kabosa ofisini kwake na kutofautiana kimazungumzo lakini alidai kuwa alimuamuru kuondoka ofisini hapo kwa kuwa hakumtambua kama ni kiongozi wa dini.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya alikanusha tuhuma za kueneza udini na kwamba hilo halikufanyika kwa ajili ya udini bali ni moja ya matokeo ya kiutendaji.

Alimtupia lawama na kumtaja diwani Mhina kuwa ndiye anayechochea mgogoro huo kwa kueneza udini kuwa yeye anawapendelea waislamu jambo ambalo ni hatari.


Chanzo: Nipashe Jumapili

haya bi halima ufalme ni wako
 
FIKRA NGUMU;

Mahali popoote duniani ambapo kanisa limestawi jamii husika lazima iwe maskini wa kutupwaaa. Rejea kisa cha Askofu Oscar Romero wa Amerika ya kusini ambako kanisa limeshika hatamu na akaanzisha " Liberation Theology " lakini alipingwa hadi na Papa kutoka Vatican....Kanisa halikutaka jamii ile ikombolewee, Alikufa katika mazingira ya kutatanishaa sanaaa.. !

Kanisa pia halitaki jamii ya Ki Tanzania ikombolewe na Umaskini !

Sina hakika na haya ubayoyasema. Ningekubaliana na wewe kama ungesema kuwa sehemu za wakatoriki jamii ni maskini lakini kwa lutheran ni kinyume. Hata hivyo hatuwezi kuupuuza mchango wa wakaroriki kstika elimu ya tanzania
 
Back
Top Bottom