DC Karagwe atoa agizo la kukamatwa kwa viongozi Muleba waliouza ardhi kinyemela kwa raia wa Rwanda

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,564
21,586
Mkuu wa wilaya ya Karagwe iliyoko mkoani Kagera Mhandisi Richard Ruyango ameliagiza jeshi la polisi kuwakamata na kuwafikisha Mahakamani viongozi wa kata Ngenge ambao ni pamoja na diwani wa kata hiyo Ezekiel Kaganda, Mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Binoni Josephat Shimikile na mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Kishuro Julius Domician ambao kwa pamoja wanakabiliwa na tuhuma ya kuuza kinyemela ardhi ya kijiji hicho kwa raia toka nchi jirani wanaoingia hapa nchini na mifugo yao ambayo imekuwa ikifanya uharibifu mkubwa wa mazao kwenye mashamba ya wakulima.

Mkuu huyo wa wilaya ametoa agizo hilo alipofanya ziara katika kijiji cha Kishuro baada ya kusikiliza kero za wananchi ambao wameonyesha kutoridhishwa na uongozi wa serikali ya kijiji hicho ambao umerushiwa tuhuma nyingi ambazo ni pamoja na ubadhilifu wa mali za kijiji na kupokea mifugo iliyoondolewa kwenye hifadhi ya misitu na mapori ya akiba kufuatia operesheni iliyoendeshwa mkoani kagera hivi karibuni ambayo baadhi yao wananchi wameikamata.

Mkuu huyo wa wilaya pia amestushwa na hatua ya mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Binoni ya kuanzisha kinyemela kijiji cha Rukindo kwa ajili ya makazi ya raia toka nchi jirani ya Rwanda ambacho hakina usajili.

Kwa upande wao viongozi waliotuhumiwa wamekana tuhuma zilizoelekezwa kwao na wananchi, naye mkuu wa jeshi la polisi wa wilaya ya Muleba, Lazaro Mwanyasi ameahidi kuwachukulia hatua viongozi watakaowanyanyasa wananchi walioeleza kero za viongozi wao mbele ya mkuu wa wilaya.

Chanzo:
ITV
 
Mkuu wa wilaya ya Karagwe iliyoko mkoani Kagera Mhandisi Richard Ruyango ameliagiza jeshi la polisi kuwakamata na kuwafikisha Mahakamani viongozi wa kata Ngenge ambao ni pamoja na diwani wa kata hiyo Ezekiel Kaganda, Mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Binoni Josephat Shimikile na mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Kishuro Julius Domician ambao kwa pamoja wanakabiliwa na tuhuma ya kuuza kinyemela ardhi ya kijiji hicho kwa raia toka nchi jirani wanaoingia hapa nchini na mifugo yao ambayo imekuwa ikifanya uharibifu mkubwa wa mazao kwenye mashamba ya wakulima.

Mkuu huyo wa wilaya ametoa agizo hilo alipofanya ziara katika kijiji cha Kishuro baada ya kusikiliza kero za wananchi ambao wameonyesha kutoridhishwa na uongozi wa serikali ya kijiji hicho ambao umerushiwa tuhuma nyingi ambazo ni pamoja na ubadhilifu wa mali za kijiji na kupokea mifugo iliyoondolewa kwenye hifadhi ya misitu na mapori ya akiba kufuatia operesheni iliyoendeshwa mkoani kagera hivi karibuni ambayo baadhi yao wananchi wameikamata.

Mkuu huyo wa wilaya pia amestushwa na hatua ya mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Binoni ya kuanzisha kinyemela kijiji cha Rukindo kwa ajili ya makazi ya raia toka nchi jirani ya Rwanda ambacho hakina usajili.

Kwa upande wao viongozi waliotuhumiwa wamekana tuhuma zilizoelekezwa kwao na wananchi, naye mkuu wa jeshi la polisi wa wilaya ya Muleba, Lazaro Mwanyasi ameahidi kuwachukulia hatua viongozi watakaowanyanyasa wananchi walioeleza kero za viongozi wao mbele ya mkuu wa wilaya.

Chanzo:
ITV

Karagwe RAIA Wa kigeni ni vigumu sana kuwaondoa maana kuna vijiji kama Kibimba ( Kata ya mabira) , makazi ( mabira) , omukagando ( mabira), Businde, maeneo hayo yamekaliwa na wageni kwa 90%, wengine wapo Tangu Uhuru wanakaribisha ndugu zao hivyo kuwatoa inakuwa ngumu, eneo hilo ni LA watu kutoka Rwanda , pia hata Wilaya za Misenyi & Ngara wahamiaji ni wengi tu , ukizingatia uingiaji nchini kwetu ni rahisi sana.
 
Karagwe RAIA Wa kigeni ni vigumu sana kuwaondoa maana kuna vijiji kama Kibimba ( Kata ya mabira) , makazi ( mabira) , omukagando ( mabira), Businde, maeneo hayo yamekaliwa na wageni kwa 90%, wengine wapo Tangu Uhuru wanakaribisha ndugu zao hivyo kuwatoa inakuwa ngumu, eneo hilo ni LA watu kutoka Rwanda , pia hata Wilaya za Misenyi & Ngara wahamiaji ni wengi tu , ukizingatia uingiaji nchini kwetu ni rahisi sana.
Ni kweli mkuu,kuna Mabira na Bushangal (r)o huko ni hatari kwa wahamiaji. Nakumbuka miaka fulani wakati nasoma kule kuna kijiji walichukua raia karibia wote na kuwarudisha Rwanda.
 
Back
Top Bottom