Elections 2010 DC Igunga ni mkristo mkatoliki; Kwanini hajasema kitu?

Wajameni tuwe waangalifu kwenye jambo hili. Mwislamu kuolewa na mkristo hakummfanyi mwislamu kuwa automatically mkristo kwani hata huko kanisani zipo ndoa za mchanganyiko wa dini au madhehebu. Ili tuweze kuwa na uhakika kama kweli ni mkristo tulete vithibitisho kwamba alibatizwa (mahali, na mbatizaji wake) na jina lake la ubatizo. Kwa kifupi tutafute cheti chake cha ubatizo au watu wanaomjua fika kwamba ni mkristo na jina lake linafahamika. siyo hizi ngonjera za kusema kaolewa na mkatoliki kwa hiyo naye ni mkatoliki.

Kwa uelewa wangu huu katika kanisa katoliki hakuna ndoa inayoweza fungwa kanisani mpaka mtu awe mkatoliki kwa kufuata taratibu zote hivyo mama alibadili dini kumfata mzee kwa ubatizo, komnio na kipaimara then sakramenti ya ndoa upo hapo katoliki si kama madhehebu mengine ya kikristo au kiislamu mfumo wake mgumu sana. KUBALI TU MLIKURUPUKA KAMA MLIVYOZOEA
 
Super dupa crap!!!
Ukweli unabaki kuwa toka mwanzo kuvuliwa kwa hijabu/mtandio kulihusishwa na kwamba DC ni mwislamu na kwamba amekoseshwa sitiri ya kike kwa utaratibu wa kiislamu. Ni baada ya kujua kuwa kumbe DC si mwislamu swala ndio limekuwa hijabu/mtandio. Comments zako ninaonesha au double-standards au unafiki. Tukumbushane mambo kadhaa hapa: a) Bakwata haikuwa kutoa tamko juu ya kukamatwa kwa Magdalena Sakaya, kupigwa na kuumizwa kwa Josephine Mshumbusi na wengine wengi!! Hata hivo wanawake na watoto huko Pakistani, Somalia na Afghanistan wanauawa na kuteswa na fellow muslim brothers - Bakwata iliwahi kusema chochote?? Bakwata ingekuwa inazungumzia hijabu, isingejiingiza kwenye kushauri CDM isipigiwe kura. Hapa ndipo wenye upeo wa kufikiri wamekazia!!! Bakwata ingetoa tamko la namna mbadala ambayo mhalifu wa kike ashughulikiwe.


Kusema hijabu ni ya uislamu au sketi ni alama ya ukristo ni kukosa upeo wa ufahamu. Fikiri mbali kuliko mavazi na vitabu au alama za dini. All faiths are ideologies!!
Naomba nikumbushwe kidogo hapa, hivi wale wanao pigwa mawe mpaka kufa kule uarabuni kwa tuhuma za ugoni huwa wanavuliwa kwanza hizo hijabu?na mahakama ya kadhi imeisha anza hapa Bongo?
 
Ndugu, mimi nipo karibu na hiyo familia, nimesikitishwa sana na upotoshaji unaoendelea kwenye thread hii! Ukweli ni kuwa bi Fatma amezaliwa muislam, na kweli pia aliolewa na mkristo Kimaryo . MUHIMU HAPA KU-NOTE NI KUWA BI FATMA SI MKRISTO kwa dini na PIA WAMETENGANA NA HUYO MUME WAKE KITAMBO SASA, na hiyo imempa fursa ya kumrejea MOLA wake! Wale washambulizi wa CHADEMA walifanya hivyo wakijua kuwa ni muislamu, angekuwa dada yao wakikatoliki wasingethubutu!

Katika kumrejea mola wake wewe ulikuwa shahidi. Mbona maandiko hayana kitu kama hicho kwa kuwa alifanya uzinzi hadi akazaa watoto wanne makafiri!!!!
 
Watanzania wenzangu hii hata kama huyo mama ni Mkiristo ndio anaruhusiwa kuvuliwa nguo zake? Mpaka sehemu zake za mwili wake maeneo ya tumboni yanabaki wazi.
Mafundisho ya Ukiristo na ya Bwana yesu yanakubali mwanamke kudhalilishwa?

Hoja ya msingi ni kwanini Dc akatoa ofisini kwenda field bila ulinzi wa Polisi, kiasi cha kuwekwa chini ya ulinzi wa raia citizen arrest. Yaani tunapoteza muda kumtetea mfuga Nguruwe, Bakwata mmetungusha sana
 
Suala la dini ni iman ya mtu,anaweza kuwa ameolewa na mkristo ila bado ana imani ya kiislamu,hilo ni suala la undani sana kwa mtu,ila kama kweli anafuga nguruwe je anastahili kuvaa hijabu????nadhani bakwata walitakiwa kumshitaki mama fatma kimario kabla ya kiikandamiza chadema,kwani yawezekana bi fatma anaudhalilisha uislamu kwa kuvaa vazi hilo hata wakati akifagia banda la mifugo yake.hapa bakwata tuombeni radhi waislamuuu.
 
Katika gazeti la Mwanahalisi toleo la juma kuanzia tarehe 28.9.2011, Saed Kubenea amefichua kuwa Fatuma Kimario anayetumiwa na CCM kwa kupata kura kwa udini huko Igunga siyo Muislam. Kubenea amefichua kuwa Fatuma amefunga ndoa na mkirsto na wanawatoto wawili wakristo mmoja wao ni Vivian na mmoja wao anafunga ndoa ya kikristo mwezi wa kumi mwaka huu. Habari zaidi mwanahalisi la leo.
 
Ni aibu kwa kibonde vilevile msimsahau,sheria za kiislamu zinasema once umeolewa au kuish na mtu bila kupitia sharia za ndoa wewe si muislam!uislam sio jina wala kuvaa hijab njaa itawaua maustaadh wetu akina kilemile
 
Wala sio Kubenea na mwanahalisi, ilishatolewa JF mapema tu kuwa huyu mama si mwislam, labda mwanahalisi waliiona humu wakaifatilia kwa undani zaidi. Kwahiyo hapo afichui chochote, zaidi ya kuhabalisha wasiojua kama wewe.
 
Wala sio Kubenea na mwanahalisi, ilishatolewa JF mapema tu kuwa huyu mama si mwislam, labda mwanahalisi waliiona humu wakaifatilia kwa undani zaidi. Kwahiyo hapo afichui chochote, zaidi ya kuhabalisha wasiojua kama wewe.

Alipoandika kafichua inamaana si kwa wana jf tu wapo ndugu zetu kule ngerengere ambao awajui hata jf ni nini kwa hiyo aijalish kubenea kaitoa wapi taarifa kwa hata hapa jf ni chanzo cha habari pia. Suala la kusema hata hapa jf limeshaongelewa si wote wanajf.
 
Wala sio Kubenea na mwanahalisi, ilishatolewa JF mapema tu kuwa huyu mama si mwislam, labda mwanahalisi waliiona humu wakaifatilia kwa undani zaidi. Kwahiyo hapo afichui chochote, zaidi ya kuhabalisha wasiojua kama wewe.

Mkuu ametoa details nyingi nzuri, mie nimetoa machache tu. Ameongea pia na watalaam wa ndoa za kislamu na uislam waliotoa tafsiri ya ndoa ya kiislam na muislam ni nani. Huyo DC kwa ufafanuzi uliotolewa si mwislam na wala hana ndoa ya kiislamu. CCM naona wanatapatapa sana, hata choo cha binadamu wanajipaka ilimradi wapate kura.
 
Vipi bakwata bado Wana la kusema.?na ule mda walotoa cdm kuomba radhi umepita?
 
Thanks, but we new it long time ago....ni hayo tu
Wameona aibu baada ya Prof. Abdala Safari kuwashushua, ila wa kulaumiwa ni CCM, ndio sumu katika nchi yetu, wala siyo Bakwata wao wanatumiwa tu kama alivyotumiwa DC Fatuma
 
Vipi bakwata bado Wana la kusema.?na ule mda walotoa cdm kuomba radhi umepita?
Wameona aibu baada ya Prof. Abdala Safari kuwashushua, ila wa kulaumiwa ni CCM, ndio sumu katika nchi yetu, wala siyo Bakwata wao wanatumiwa tu kama alivyotumiwa DC Fatuma
 
Kwenye status ya baba ubaya facebook ameandika kuwa DC kumbe anafuga nguruwe nyumbani kwake mbezi sasa bakwata inabidi watuombe radhi ikithibitika
 
Jaman haya majina yanawaponza! Wenzetu hawakujua km huyu mm alisha asi! Polen sana mkajipange upya na mjifunze, sio kutumiwa km zile karatas lain wakat wa kupiga kubwa!
 
Inawezekana, maana Kubenea ana jina la kiislamu lakini anatumikia maadui wa Uislamu. Munafiq ni mbaya kuliko twanghut!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom