DC ataka walimu watesaji kukamatwa

DC ataka walimu watesaji kukamatwa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,286
Reaction score
10,831
MKUU wa Wilaya ya Njombe, Ruth Msafiri, ameagiza kukamatwa kwa walimu watakaobainika kuwafanyia vitendo vya kikatili wanafunzi ikiwa hatua ya kukomesha vitendo hivyo vinavyoendelea nchini.

Msafiri alisema hayo jana mjini hapa wakati msafara wa kijinsia wa kutokomeza ukatili ulipofika mkoani Njombe kwa ajili ya kutoa elimu ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Alisema serikali haipingi adhabu ya viboko lakini si kutoa adhabu hiyo kupitiliza na kusababisha ulemavu na maumivu kwa wanafunzi.

Mkuu huyo wa wilaya alisema suala la ukatili wa kijinsia ni mapambano makubwa nchini, hivyo jitihada zinahitajika kwa wananchi, wadau na mashirika yasiyo ya kiserikali kuhakikisha wanaunganisha nguvu ili kuondokana na vitendo hivyo.

Alivitaka vyombo vya usalama kuacha kufanya ukatili kwa kuchelewesha kesi za vitendo vya unyanyasaji na kusababisha ukatili wa kihisia kwa waathirika wa matukio hayo.

“Vyombo vya usalama mnachelewesha kesi kwa sababu mnaomba rushwa. Nawaomba msiwe kikwazo cha kupatikana kwa haki ya wahanga (waathirika) wa vitendo vya ukatili,” alisema.

Akizungumza kuhusu msaada wa kisheria unaotolewa na Shirika la Legal Serivces Facility, Joseph Magazi alisema wameweka nguvu katika kuisaidia jamii katika matatizo ya kisheria kwa kuwawezesha wasaidizi wa kisheria katika mikoa na wilaya kutoa elimu husika.

"Tumejipanga kushirikiana na serikali katika kuhakikisha tunaifikia jamii katika kutoa elimu itakayowezesha wenye matatizo mbalimbali ya kisheria kupata msaada na kuyatatua matatizo yao," alisema
 
Vipi upande wa pili,wale walimu wanaofanya kazi zao kwa weledi,ana neno juu yao?
 
Tatueni kwanza changamoto zinawakabili Waalimu ndo mje na matamko ya namna hiyo, hakuna Mwalimu anaetoka kwake akiwa na lengo la kuumiza watoto. Mkiweka Mazingira Bora shuleni hata hivyo viboko havitahitajika.. Japo Ni kweli Kuna Waalimu wengine Vimeo..!!
 
Walimu nao wapunguze kiherehere cha kuchapa chapa wanafunzi, mtoto akizingua we achana nae ni hasara kwa wazazi wake na Taifa.

Dunia itamfunza.
 
Aanze na Askari watesaji,wadhalilishaji,na wanaofanya kazi kwa misingi ya ukanjanja then ahamie kwa walimu huo ndio uadilifu .
 
Back
Top Bottom