DC amkwida diwani katika chakula

Tunata kiongozi anayejiheshimu na kujithamini katka safu ya uongozi wa nchi hii. Kiongozi unapovunjiwa heshima inabidi uonyeshe kujithamini kwako kuchukua hatua kwa yule aliyekuvunjia heshima na wananchi unaowaongoza waone kweli umejithamini kwa kuchukua hatua.

Kuna namna nyingi za kuonyesha kujithamini mara unapovunjiwa heshima. Nasikitika kusema kuwa Diwani Sipemba hakujithamini kwa kitendo chake cha kutochukua hatua baada ya kudalilishwa, kwa kifupi , diwani kakubali kudhalilishwa pamoja na wale waliomchagua.
 
hivi chakula huko Kahama ni adimu sana ??

Nashauri hii tabia ya kupanga foleni ife hasa kwa upande wa kupata chakula na Mpesya tafadhari sana usituaibishe watu wa Mbeya hasira za kubwagwa na Sugu usizihamishie Kahama
...Haaaa haaaa haaaaaa ukizingatia ulikuwa ubwabwa mh!!! roho zinakimbia bhana!
 
Diwani alivunja utaratibu. Kuna itifaki alikuwa akiifanya mkuu wa wilaya hivyo diwani angesubiri wakati wake ufike. Inakuwa kama waligombea chakula!

Ni kweli ila itifaki ikivunjwa busara inatakiwa itumike hasa mtu mzima anapokuwa katika mstari inabidi umpotezee alafu unampa elimu, hata hivyo diwani yule nae amekomaa kisiasa hajasusa msosi akaugonga bila zengwe pale DC alipomtoa mikononi mwa police
 
Benson Mpesya akapimwe akili,akumbuke kuwa kuna siku atakwenda kufanya kazi kata ya diwani aliyemdhalilisha,na yeye kama dc hana watu diwani ana watu,akumbuke yaliyotaka kumpata Makamu wa Raisi tunduma hadi akaokolewa na Ernest Silinde David.
 
...Haaaa haaaa haaaaaa ukizingatia ulikuwa ubwabwa mh!!! roho zinakimbia bhana!

Huko ndipo unalimwa kama msimu ni mzuri kilo moja huwa inashuka mpaka Tsh.500 (mia tano), hapa nadhani kuna dhana kama ile ya utotoni chakula cha nje ya nyumbani ni kitamu maana mtoto kimepikwa kile kile nyumbani kula ni issue lakini akienda kwa ajirani anakula mpaka basi
 
Dah ubwabwa wa ccm inaonyesha mtamu sana
 
kwikwiwiwwwwwwwwwwwwwwwwwww hii haikuwa nzuri hata kidogo.anyway kama hakufwata itifaki asingetumia nguvu zote hizo na kumdhalilisha namna hiyo angemsema baadae chakula ni kitu kidogo sana. au kilikuwa hakitoshi?

halafu DC anakagua mstari wa chakula kujua nani kala nani yupo nani hayupo??????? hii ni aibu hana wasaidizi hana kazi zingine.?

na wewe diwani hata kama njaa yako imezidi imezalilishwa bado wala?
je angekuwa wa ccm angemfanya hivi? hapa mwisho nauliza tu.
 

haya maandishi yako hayana mvuto kusoma, japo habari yenyewe ni nzuri huku janvini
 
haya maandishi yako hayana mvuto kusoma, japo habari yenyewe ni nzuri huku janvini

1.hujalazimishwa kusoma

2.unaweza kuweka mvuto kwa kufanyia editing kadri upendavyo wewe

3. hoja yako ni ya kipuuzi.
 
Jamani kateuliwa kuwa mkuu wa wilaya?aaaaarrrgh hii nchi vip?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…