ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Kuna mashirika yanapaswa kubadili mfumo wake wa Utendaji kazi. Katika kuwezesha wateja kulipia bili zao kwa wakati DAWASCO wametoa mifumo mbalimbali ya malipo ikiwemo M-Pesa, NMB Mobile nk lakini cha kusikitisha, unapojaribu kulipia bili yako ya maji kupitia mifumo hiyo pengine huduma haipatikani kabiosa, na unaweza kukata tamaaa hasa ukitumia NMB Mobile.Unapoomba maelekezo kutoka kwa watendaji wa Shirika hilo wanakuambia kulipia kupitia njia hizo mbadala kunachelewesha shirika kupokea malipo na haikuwezeshi kupata stakabadhi mpaka uende tena ofisini kwao. Hii ni urasimu usio wa lazima na unaisababishi Serikali kupoteza mapato mengi. Aidha, tofauti na wakusanya Kodi kama TRA ambao wanatewmbea na mashine za kukukatia risiti wanapofuatilia walipa kodi, kwa DAWASCO ni tofauti, msoma mita akija kwako kusoma mita pengine anakuwa hana rekodi kamili ya unachodaiwa (hana kumbuklumbu ya mita yako) na akija atakutaka wewe ndio umpe risiti uliyolipia mara ya mwisho ili ajiridhishe .Msomaji huyo akisoma na kubaini unadaiwa, anataka ukalipie Ofisini kwao ili upate risiti vinginevyo atakukatia maji ili ukilipa ndipo urejeshewe tena..huu ni upuuzi na kushindwa kutimiza wajibu..kwa nini mashirika kama DAWASCO yasiwe na utartibu wa wasoma mita kutumika kukusanya Bili moja kwa moja kwa wateja badala ya kuwasababishia wateja usumbufu usio na msingi wa kwenda kupanga foleni Ofisini??? Ni kiasi gani cha fedha zinazopotea kwa mteja ambae ametumia maji kwa kliwango kikubwa lakini badala yake akaishia kukatiwa maji na kuachwa tu ili arejeshewe baada ya kulipia bili?? DAWASCO hamuoni kuwa wapo wateja ambao wao shida sio kulipa bili bali wanakosa muda wa kufika Ofisini kwenu kulipa au kufuatilia risiti tu za malipo baada ya kulipa ??? Hamuoni unapoteza wateja na Serikali kupoteza mapato??..kwa nini wananchi wasijiunganishie maji kihuni kama ninyi hamna mkakati wa kuwafanya waheshimu sheria bila shuruti wana usumbufu ??