DAWASA yatoa tahadhari upungufu wa maji Dar es Salaam na Pwani

DAWASA yatoa tahadhari upungufu wa maji Dar es Salaam na Pwani

DAWASA

Official Account
Joined
Oct 7, 2010
Posts
158
Reaction score
103
TAARIFA KWA WAKAZI WA DAR ES SALAAM NA PWANI
TAARIFA YA UPUNGUFU WA HUDUMA YA MAJI
6.12.2025

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawataarifu wateja na wananchi wanaohudumiwa na mtambo wa kuzalisha maji Ruvu Chini (Kuanzia maeneo ya Bagamoyo, Tegeta, Boko, Mbezi Beach, Mwenge, Kinondoni, Mwananyamala, Masaki hadi Ilala) kuwa kumekuwa na upungufu wa huduma ya maji katika maeneo mengi kutokana na uzalishaji wa Maji kushuka zaidi ya kiwango cha kawaida kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kushuka kwa kina cha Mto Ruvu iliyosababishwa na kuchelewa kwa Mvua.

Kwa mtambo wa Ruvu Juu katika maeneo ya kuanzia Kibaha, Kibamba, Kimara, Tabata, Kinyerezi, Pugu hadi Kisarawe hali ya uzalishaji maji inaendelea vizuri na huduma inawafikia wananchi.

Jitihada mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa kwa kushirikiana na Wizara ya Maji ikiwemo kusitisha matumizi ya Maji ya Mto Ruvu kwenye shughuli za Kilimo na kuyaelekeza katika matumizi ya Binadamu tu na kuongeza matumizi ya Visima ili kupunguza changamoto ya ki-huduma.

DAWASA itaendelea kutoa taarifa za kila wakati juu ya hali ya upatikanaji Maji kwa Wananchi ili waweze kujiandaa na shughuli muhimu za kiuchumi.

Tunawaomba Wananchi kuendelea kuhifadhi Maji yanayopatikana kwa matumizi muhimu
DAWASA inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza

Wasiliana nasi Kituo cha huduma kwa wateja 181 (bure) na 0735 202-121 (WhatsApp tu)

Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano.
181
Malipo Bila
WhatsApp Pekee 0735 202 121
Tutembelea kwenye tovuti yetu www.dawasa.go.tz
Barua Pepe
Mitandao ya kijamii
info@dawasa.go.tzdawasatz


1765020699634.png


 
Hapa nilipo leo ni wiki ya pili hakuna Maji.

Kuna wengine hapa hapa Dar na Pwani wanalalamika kuwa ni zaidi ya mwezi hakuna Maji. Arusha, Morogoro na miji mingine kama Dodoma hali ni hiyo hiyo.

Matukio kama haya ndiyo yanayopaswa kuwakumbusha Watumishi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kuwa siku zote Wanapaswa kusimamia Haki pamoja na misingi ya Utawala Bora maana wakisimamia hayo Wananchi watapata viongozi sahihi wenye akili, uwezo na majibu sahihi na ya kudumu ya changamoto zinazowakabili.

Vyombo vya Ulinzi na Usalama badala ha kuwalinda Wananchi na Maslahi yao, wanalinda kikundi kidogo cha Watu kinacholazimisha kuwatawala Wananchi bila ridhaa yao, tena kwa nguvu na hata kuwaua, kuwabaka, kuwapoteza, kuwafungulia kesi za uongo na kuwalawiti.

Matokeo yake ndo haya. Viongozi wanaolazimisha kuwatawala Wananchi hawaoni haja ya kuwajibika kweli kwa Wananchi. Hawaoni haja ya kutafuta suluhisho la kudumu juu ya Matatizo yanayowakabili wananchi maana wana uhakika wa kuiba chaguzi na kuwalazimisha wananchi kukubali chochote kwa mtutu wa bunduki. Wao wanachoangalia ni kujinufaisha binafsi na familia zao.

Katika karne hii ya 21, wakati wenzetu wakifikiria kwenda kuishi sayari nyingine, na Mataifa mengine ambayo yapo Jangwani kama Israel hawana mgao wa Maji, hapa Tanganyika Samia, familia yake, ndugu zake na chama chake wanawaibia wananchi, wanalazimisha kuwatawala kwa nguvu huku Wananchi wakipata shida ya mgao wa Maji.

Cha ajabu zaidi Vyombo vya Ulinzi na Usalama vinatumika kumlinda huyu mtu Samia na genge lake ili azidi kufanikisha mateso ya Watanganyika.

20251206_132608.jpg
 
TAARIFA KWA WAKAZI WA DAR ES SALAAM NA PWANI
TAARIFA YA UPUNGUFU WA HUDUMA YA MAJI
6.12.2025

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawataarifu wateja na wananchi wanaohudumiwa na mtambo wa kuzalisha maji Ruvu Chini (Kuanzia maeneo ya Bagamoyo, Tegeta, Boko, Mbezi Beach, Mwenge, Kinondoni, Mwananyamala, Masaki hadi Ilala) kuwa kumekuwa na upungufu wa huduma ya maji katika maeneo mengi kutokana na uzalishaji wa Maji kushuka zaidi ya kiwango cha kawaida kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kushuka kwa kina cha Mto Ruvu iliyosababishwa na kuchelewa kwa Mvua.

Kwa mtambo wa Ruvu Juu katika maeneo ya kuanzia Kibaha, Kibamba, Kimara, Tabata, Kinyerezi, Pugu hadi Kisarawe hali ya uzalishaji maji inaendelea vizuri na huduma inawafikia wananchi.

Jitihada mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa kwa kushirikiana na Wizara ya Maji ikiwemo kusitisha matumizi ya Maji ya Mto Ruvu kwenye shughuli za Kilimo na kuyaelekeza katika matumizi ya Binadamu tu na kuongeza matumizi ya Visima ili kupunguza changamoto ya ki-huduma.

DAWASA itaendelea kutoa taarifa za kila wakati juu ya hali ya upatikanaji Maji kwa Wananchi ili waweze kujiandaa na shughuli muhimu za kiuchumi.

Tunawaomba Wananchi kuendelea kuhifadhi Maji yanayopatikana kwa matumizi muhimu
DAWASA inaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza

Wasiliana nasi Kituo cha huduma kwa wateja 181 (bure) na 0735 202-121 (WhatsApp tu)

Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano.
181
Malipo Bila
WhatsApp Pekee 0735 202 121
Tutembelea kwenye tovuti yetu www.dawasa.go.tz
Barua Pepe
Mitandao ya kijamii
info@dawasa.go.tzdawasatz


Wapumbaf.
Na ile master plan yao nzuri nzuri ya kujenga dam kuukinga mto Ruvu, walisema itakuwa sijui maeneo ya Morogoro, sijui eneo gani nishasahau ni muda sasa!

Kazi ni kuhondomola tu hela za nchi na kukimbilia kuendeleza miradi ya kizima moto isiyo na uhakika kama hiyo!

Unategemea waterflaw ya msimu kwa karne hii ya mabadiliko ya tabia nchi kweli!

Dawasa hampo serious, Mungu tena!
 
Kila mwaka shida ni mto Ruvu, kila mwaka case ni hiyo..
Hakuna mtu wakufikiri solution nyingine kuacha na kutegemea mto Ruvu miaka na miaka?
chanzo sio mto ruvu chanzo ni ujinga!
mwanza wana lake victoria mpaka jijini unashuka feli unaingia katikati ya mji,
lakini nao wana mgao wa maji

huoni kua mnaongozwa na akili mgando hapo
 
E Mungu mim naomba huu mto ruvu maji yakauke ili wakose visingizio vya kijinga hawa matapeli
 
Back
Top Bottom