nnunu
JF-Expert Member
- Mar 4, 2011
- 654
- 230
Habari?,
Samahani naomba niambiwe tiba ya vipele kwenye ngozi kwa mtoto au doctor bingwa zaidi wa magonjwa ya ngozi kwa watoto.
Nimezunguka kwa madoctor wengi sana hapa ,mfano agakhan,tmj,tumaini,Dr hammeir,Dr ndodi na amepimwa vipimo mbalimbali hajaonesha kama ana tatizo lolote.
Kwenye suala la usafi namfanyia usafi wa hali ya juu sana,hajawahi kurudia kuvaa nguo,nguo zake ni matilio ya pamba,anaoga mara 2 asbh na jion,vitu vyake vya kuchezea nasafisha kila wiki, chakula chake namwandalia mwenyewe mara nyingi.
Baadhi ya ma DR walishauri asipewe sukari,soda,juise za viwandani vyote hivyo nimezingatia,juise nampa niliyotengeneza mwenyewe bila kuweka sukari,ila uji wake namwekea asali ilihakikishwa na mtaalam wa asali kuwa ni asali nzuri, na chakula chake anapewa visivyokobolewa hata unga wa uji natengeneza mwenyewe kwa usalama zaid.
Kwa bahati nzuri muda mwingi nipo naye kwasababu ni mjasiriamali so muda wa kuwa pamoja nawe naupata bila tatizo. Japo hapati homa, wala haumwi umwi, shule anaenda bila tatizo na darasani anafanya vizuri sana, tatizo NGOZI YAKE SIYO NYORORO MUDAMWINGI ANA VIPELE VIDOGO VIDOGO VYA JOTO, havimwashi wala kumuuma, nimempaka mafuta ya nazi nilitengeneza mwenyewe,haijasaidia, sasa hivi nampaka vaseline ya watoto na kumwogeshea sabuni ya mbuni, niliacha kutumia johnson baby nilipoona haimsaidii.
Doctor wa mara ya mwisho alisema suluhisho ni kuishi naye sehemu za baridi kwa sababu joto la Dar linamwathili, ila mvua ikinyesha siku 3 au zaidi na joto likipingua anakuwa na ngozi nzuri mpaka inapendeza,kuna kipindi nilisafiri naye kwenda lushoto alikuwa na ngozi nzuri kupita kiasi kwa sababu kule kuna baridi sana,niliporudi naye Dar vipele vikarudi tena,pia joto likiongezeka vipele vinaanza tena.
Sijawahi kumpaka dawa za cream kwa kuhofia kuharibu kinga yake ya ngozi.Kama dawa ni kuishi naye sehemu ya baridi ,je hakuna dawa ya kutibu tatizo hili?, na mwisho wa tatizo hili ni miaka mingap?? ana miaka 5 sasa.
Nampenda sana mwanangu napenda kumwona akiwa na ngozi isiyo na kipele kama zilivyo ngozi za watoto wengine pamoja na ngozi zetu sisi wazazi wake, tafadhali naomba msaada wenu.
Pia samahani kwa kuandika ndefu inaweza kuwachosha ,nisamehe katika hili nia yangu ni kutoa maelezo ya kutosha.
Asanteni.
Samahani naomba niambiwe tiba ya vipele kwenye ngozi kwa mtoto au doctor bingwa zaidi wa magonjwa ya ngozi kwa watoto.
Nimezunguka kwa madoctor wengi sana hapa ,mfano agakhan,tmj,tumaini,Dr hammeir,Dr ndodi na amepimwa vipimo mbalimbali hajaonesha kama ana tatizo lolote.
Kwenye suala la usafi namfanyia usafi wa hali ya juu sana,hajawahi kurudia kuvaa nguo,nguo zake ni matilio ya pamba,anaoga mara 2 asbh na jion,vitu vyake vya kuchezea nasafisha kila wiki, chakula chake namwandalia mwenyewe mara nyingi.
Baadhi ya ma DR walishauri asipewe sukari,soda,juise za viwandani vyote hivyo nimezingatia,juise nampa niliyotengeneza mwenyewe bila kuweka sukari,ila uji wake namwekea asali ilihakikishwa na mtaalam wa asali kuwa ni asali nzuri, na chakula chake anapewa visivyokobolewa hata unga wa uji natengeneza mwenyewe kwa usalama zaid.
Kwa bahati nzuri muda mwingi nipo naye kwasababu ni mjasiriamali so muda wa kuwa pamoja nawe naupata bila tatizo. Japo hapati homa, wala haumwi umwi, shule anaenda bila tatizo na darasani anafanya vizuri sana, tatizo NGOZI YAKE SIYO NYORORO MUDAMWINGI ANA VIPELE VIDOGO VIDOGO VYA JOTO, havimwashi wala kumuuma, nimempaka mafuta ya nazi nilitengeneza mwenyewe,haijasaidia, sasa hivi nampaka vaseline ya watoto na kumwogeshea sabuni ya mbuni, niliacha kutumia johnson baby nilipoona haimsaidii.
Doctor wa mara ya mwisho alisema suluhisho ni kuishi naye sehemu za baridi kwa sababu joto la Dar linamwathili, ila mvua ikinyesha siku 3 au zaidi na joto likipingua anakuwa na ngozi nzuri mpaka inapendeza,kuna kipindi nilisafiri naye kwenda lushoto alikuwa na ngozi nzuri kupita kiasi kwa sababu kule kuna baridi sana,niliporudi naye Dar vipele vikarudi tena,pia joto likiongezeka vipele vinaanza tena.
Sijawahi kumpaka dawa za cream kwa kuhofia kuharibu kinga yake ya ngozi.Kama dawa ni kuishi naye sehemu ya baridi ,je hakuna dawa ya kutibu tatizo hili?, na mwisho wa tatizo hili ni miaka mingap?? ana miaka 5 sasa.
Nampenda sana mwanangu napenda kumwona akiwa na ngozi isiyo na kipele kama zilivyo ngozi za watoto wengine pamoja na ngozi zetu sisi wazazi wake, tafadhali naomba msaada wenu.
Pia samahani kwa kuandika ndefu inaweza kuwachosha ,nisamehe katika hili nia yangu ni kutoa maelezo ya kutosha.
Asanteni.