David Nkuba a.k.a Mac D hatunaye tena.

Lakini huyu Mac dizooo wa mbwembwe hizo si mwenye sifa zilizotajwa !

Kuna jambo hapa , Sisemi RIP hadi uje ufafanuzi muafaka !

Yani inachanganya kweli Mac Dee ni msanii lakin ni kweli huyo wa Dar Skendo hajawahi soma UDSM wala afanyi kazi UDSM sasa mtoa uzi kaandika halfu kasepa!
 
Nzi eh mac dee huyo ni nani na nyimbo gani alizozitoa hewani? Watu wengi Tunajua ni Huyu wa Dar skendo Holla wa pfunky produkshizo holla!

Hata mimi nimeshangaa kwa kuwa aliyefariki nilikuwa namfahamu fika. Na sijawahi kusikia alikuwa mwanamuziki,tena kwa jina la Mac Dee! Nimemuuliza mohamed Mtoi ili afafanue zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Ukituwekea picha twaweza mjua, wengine hapa hata picha haiji. RIP.
 
Wakuu nimeongea na mdogo wa marehemu ameniambia si mwanamuziki bali mtalaamu wa Ict. Marehemu nae alikuwa anajiita Mac D na moja kwa moja tafsiri ilienda kwa yule Mac dizo.
Poleni kwa usumbufu.
 
Nikiri kuwa katika kumfahamu kwangu kote David Mwenda Nkuba,sikuwahi kumjua kwa jina la MacDee.Alikuwa mtu mcheshi na kibonge fulani hivi mweusi.Alikuwa anafanya kazi Shule Kuu ya Sheria(zamani Kitivo cha Sheria) Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Alikuwa mtaalamu wa takirishi na programu zake.Ni rafiki wa kila mtu.Lala pema kaka Nkuba...
 
Wakuu nimeongea na mdogo wa marehemu ameniambia si mwanamuziki bali mtalaamu wa Ict. Marehemu nae alikuwa anajiita Mac D na moja kwa moja tafsiri ilienda kwa yule Mac dizo.
Poleni kwa usumbufu.

Ok. Lakini ulikuwa ukimfahamu huyo kaka mtu? Ungeongea kwanza na mtu anayemfahamu ili utoe taarifa sahihi.

Anyway,

R.I.P kaka Nkuba.
 
Nikiri kuwa katika kumfahamu kwangu kote David Mwenda Nkuba,sikuwahi kumjua kwa jina la MacDee.Alikuwa mtu mcheshi na kibonge fulani hivi mweusi.Alikuwa anafanya kazi Shule Kuu ya Sheria(zamani Kitivo cha Sheria) Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.Alikuwa mtaalamu wa takirishi na programu zake.Ni rafiki wa kila mtu.Lala pema kaka Nkuba...

Hakika wewe ulikuwa unamfahamu Nkuba. Jamaa alikuwa kibonge mweusi tii,lakini mtoto wake Melisa,mweupe pee. Pengine kwa vile mama Melisa naye ni mweupe pee.

R.I.P Nkuba.
 
Ok. Lakini ulikuwa ukimfahamu huyo kaka mtu? Ungeongea kwanza na mtu anayemfahamu ili utoe taarifa sahihi.

Anyway,

R.I.P kaka Nkuba.

Kweli Nzi huyu mtoi amekurupuka sana taarifa za kifo cha mtu inabidi azifanyie uhakiki then ndio azirushe hewani,maana amechanganya watu kote wanajua msanii mac dee(dar skendo) ndio kavuta,mtoi next time kua makini unaweza ukaua watu kwa mshtuko kwa kutoa taarifa zisizo na uhakika,ni kweli jamaa nkuba amefariki lakin heading uliyoweka live watu wanajua ni yule msanii coz watu hawajui majina yao halisi.
 
Sikujua kama Nkuba alikuwa mwanamuziki. Kama anayedhaniwa kuwa amefariki ni yule mwanamuziki aliyekuwa chini ya P-Funk,basi huyu ninayemzungumzia siye. Kwa maelezo ya mwanzisha uzi,nina uhakika marehemu siyo Mac Dee aliyekuwa chini ya P-Funk. Labda kama alikuwa mwanamuziki kwa jina lingine;ndiyo maana nimeanza kwa kusema "sikujua kama Nkuba alikuwa mwanamuziki".
Ninasema hivyo kwa kuwa mke wake ni ndugu yangu kwa mbali.

Ni kweli amefariki,lakini siyo leo,amefariki jana pamoja na mjomba wake mmoja. Walikuwa wakienda Kahama,Shinyanga kupeleka gari jipya (lilitoka kununuliwa Dar) la mjomba wake mmoja aliyekuwa akiumwa Dar.

Inasemekana mjomba aliyekuwa akiumwa ndiye aliyekuwa akiendesha gari,nafikiri ni maeneo ya Singida ama Manyoni ndiyo walipopata ajali baada ya tairi kupasuka. Nkuba na mjomba wake 1 ndiyo waliofariki (alikuwa na wajomba 2 katika safari). Mjomba aliyekuwa akiumwa,hajafariki.

Msiba upo pale UDSM,Ubungo Flats,eneo linaitwa Geti Maji. Ni geti la kuingilia UDSM kwa kutokea Ubungo. Mipango ya awali inasema marehemu Nkuba anaweza kuzikwa Kahama. Ingawa kwao kabisa ni Kahama. Kuna mtafuruku kidogo wa kindugu.

Bwana alitoa,bwana ametwaa. Jina lake lihidimiwe.

Pumzika kwa amani kaka Nkuba.

Jamani Nawasilisha Hili Jambo Ambalo ni Muhimu sana!! "Tyres do expire" Hakuna kitu cha hatari kama kununua gari from abroad na kutumia tyres hizo hizo kwa safari ya Mbali!! Ni hatari kupita maelezo!! Tyres zikikaa kwenye mazingira ya Maji (Idle kwa muda unaozidi miezi sita) huwa hazina tena uhalali wa safari!! Pia Tyre huwa zina expire zikishakaa zaidi ya Miaka sita!! Nawaombeni sana ndugu zangu ukinunua gari used, Jitahidi sana kubadilisha tyres! Usifanye safari ndefu hata kama zinaonekana kama mpya!!!!
 
Ninamfahamu sana Huyu ndugu alimaliza Usagara Secondary Mwaka 1992 FORM SIX!! Alikuwa mbele yangu mwaka Mmoja
 
Kwa wale wanaomfahu
David Nkuba aka Mc Dee
amefariki leo kwa ajali ya
gari ndogo maeneo ya
Shinyanga.

David alisoma Azania
Secondary, Usagara High
School, alipita pia UDSM
kidogo na baadae
akamalizia masomo yake
Chuo Kikuu cha Mysore,
India alikosemea Shahada
ya Uhandisi na kubobea
katika Ectronics na
Communications.

David ni Mwanataaluma
mzuri wa ICT amefanya
kazi makampuni mbali
mabli na mpaka mauti
inamkuta mwajiri wake ni
Chuo Kikuu cha DSM, kitivo
cha Informatics and Virtual
Eduaction.

Ameacha Mke na mtoto
mmoja Melisa.
Msiba upo nyumbani
kwake Chuo Kikuu,
unaingilia gate la Maji
kama unatokea Ubungo,
unaenda kushoto.
Tujitokeze kwa wingi
kumfariji mjane na mtoto
na kutoa msaada wowote
utakaohitajika
Bwana alitoa na bwana
ametwaa jina lake
lihimidiwe.

mac dee nimempigia simu sasa hivi yupo ok vp hii habariii
 
Mbona nimemsikia huyo Mc dee akihojiwa EATV sasa hivi, jamani?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Dah, nimesikitika sana.......... My bro wa kitaa enzi zileee

Mkuu namkumbuka enzi zile akiwa Azania na wakati tunakutana kitaa na zile mbwembwe zake, tukapoteana and then nikaona mkuu yuko India, we kept in touch although i never met him for more than 10 years

This is really sad

RIP Mkuu..... I always remember zile swagga za enzi zile, and every time i think of those days, i smile because you really was something

Miss ya Mac Dee (you kept the name to the end... one of the longest serving AKA of our time)
 
Wakuu nimeongea na mdogo wa marehemu ameniambia si mwanamuziki bali mtalaamu wa Ict. Marehemu nae alikuwa anajiita Mac D na moja kwa moja tafsiri ilienda kwa yule Mac dizo.
Poleni kwa usumbufu.
basi kamanda omba mods wabadili heding maana mac d mwenyewe atainua bango....
 
Wakuu nimeongea na mdogo wa marehemu ameniambia si mwanamuziki bali mtalaamu wa Ict. Marehemu nae alikuwa anajiita Mac D na moja kwa moja tafsiri ilienda kwa yule Mac dizo.
Poleni kwa usumbufu.
Omba mods wabadili title ya hii habari.......
 
Wakuu nimeongea na mdogo wa marehemu ameniambia si mwanamuziki bali mtalaamu wa Ict. Marehemu nae alikuwa anajiita Mac D na moja kwa moja tafsiri ilienda kwa yule Mac dizo.
Poleni kwa usumbufu.
ni kweli, ka-edit ile taarifa yako ya kwanza
 
Back
Top Bottom