DART inatarajia kupokea shehena ya mabasi 99 ya mwendokasi

DART inatarajia kupokea shehena ya mabasi 99 ya mwendokasi

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
20,725
Reaction score
31,305
Samia hasubiri kuapishwa, tayari kaanza kutekeleza ilani, mpaka 2030 hii nchi itakuwa ulaya ndogo.

Serikali kupitia Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), inatarajia kupokea shehena ya mabasi 99 ya mfumo wa mabasi yaendayo haraka (BRT) kutoka kwa mtengenezaji, kampuni ya Golden Dragon, kabla ya uzinduzi rasmi wa awamu ya pili ya huduma hiyo.

Mradi wa Awamu ya Pili wa BRT una urefu wa kilomita 20.3, umejengwa kwa gharama ya dola za Marekani milioni 159.32 (sawa na Sh bilioni 285.1) na kampuni ya China ya Sinohydro Construction Limited, na unatarajiwa kuanza rasmi kutoa huduma kamili ifikapo Septemba 1, 2025.

Mkurugenzi Mtendaji wa DART, Dkt. Athuman Kihamnia, aliieleza The Citizen siku ya Ijumaa, Julai 18, 2025, kuwa mabasi hayo yenye urefu wa mita 18 tayari yamekamilika na yamewasilishwa katika Bandari ya Glovis Precious iliyopo Jiji la Xiamen, China, tayari kwa kusafirishwa kuelekea Dar es Salaam. Mabasi mengine 101 yanatarajiwa kusafirishwa kufikia Agosti 15.
 

Attachments

  • Screenshot_20250719-192940.jpg
    Screenshot_20250719-192940.jpg
    607.5 KB · Views: 22
Tatizo lenu chawa ni kutumia nguvu nyingi kuelezea vitu ambavyo kitaalamu,kisayansi,na hata kwa macho ya kawaida huwezi mwambia mtu timamu akakiona unachokisema.

Yaani unachukua mbwa,unamuweka pembe bandia halafu unapiga kelele kuwa umenunua mbuzi aliyenona,kwa akili zako zenye ufinyu wa madini unaamini na kuhisi watu wanasapoti,kuona na kuelewa upuuzi unaojaribu washawishi kuwa wanaona.

Niseme tu huu ni ukosefu wa akili kiwango cha hatari sana. Wakati kama huu ambao kila raia anashuhudia mambo ya hovyo wewe unakuja hapa jukwaani kuandika uzi ambao ni dhahiri una maudhui ya kinafiki yenye lengo la kupotosha na sio kutoa taarifa sahihi au kusema ukweli.

Huu ni ujinga sana aisee, mimi nataka watu kama wewe mleta uzi ikibidi mambo yatakapo kaa sawa muwajibishwe kisheria na kupewa adhabu kali sana ambayo itajumuisha viboko visivyopungua 30 siku unayoingia na siku unayotoka kutumikia adhabu yako ya kifungo cha miezi 6 kwa kosa la kudhalilisha hadhi ya uraia wako, kufedhehesha na kudhihaki uzalendo na uhaini dhidi ya jamii ya watanganyika.
 
Back
Top Bottom