Dar Waterfront and Kigamboni Tunnel Master Plan

Dar Waterfront and Kigamboni Tunnel Master Plan

Shoctopus

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
3,435
Reaction score
1,995
Assalamualaikum wana JF!

Moja kwa moja kwenye mada:
Mimi sio mkazi wa Kigamboni lakini nimefuatilia matatizo ya usafiri wa ferry boat kwa muda mrefu sioni jitihada za dhati za kutatua kero hii kikamilifu.

Mamlaka za Jiji la Dar es Salaam na Serikali kuu pamoja na wizara husika kwangu mimi ama hawana ubunifu au nia ya dhati ya kuondoa changamoto ya usafiri kwenda na kurudi kati ya city center na Kigamboni.

Nasikitika kusema kwamba hata daraja jipya la NSSF lilistahili kuwa pale ferry lakini bahati mbaya wahusika hawakuona hivyo, fedha nyingi zilitumika kwa ujenzi wake lakini tatizo la kivuko cha ferry liko pale pale! Ferry boat zinajaza watu wengi kupindukia na magari kiasi cha kuhatarisha maisha ya watu.

Bahati mbaya mamlaka husika nilizotaja hapo juu wakaona wajenge daraja lingine baharini! (Tanzanite bridge). Hapohapo wakaanzisha ujenzi wa mji mpya huko Kigamboni ambao nasikia umekwama! Sishangai! Kwa changamoto ya usafiri wa ferry boat na daraja la Kurasini/Kigamboni badala ya Kigamboni/CBD short cut, nani atahama Mbezi beach au Mikocheni kwenda Ndege village? Tena makazi ya hiyo village yenyewe ni kama makambi ya jeshi! (Yaani hii nayo ni topic pekee ya community planning disaster!)

Kwahiyo ukifanya hesabu za haraka kidogo za gharama za ujenzi wa madaraja ya Tanzanite na NSSF pamoja na hiyo Ndege village, fedha zake zingetosha kujenga underwater tunnel kati ya Kigamboni na CBD. Logic yake ni kwamba hii ni njia ya mkato (short cut) kwa wakazi wengi wa Kigamboni wanaotegemea usafiri wa daladala, kwa miguu na ferry boat zinazojaza kupindukia na kuhatarisha maisha yao kila siku.

Kuhusu tunnel yenyewe. Upande wa Kigamboni ingeanzia mbali kidogo penye nafasi ya kujenga lango la kuingia na kutoka kwa mgari hata kwa miguu.

Na upande wa pili tunnel ingetokezea Gymkhana area kwasababu hapajajaa majengo makubwa na kuna connection nzuri kwenda CBD, Mnazimoja, Salenda bridge nk. Vinginevyo hata Ikulu ingehama kupisha stesheni ya Kigamboni Tunnel. Na si vibaya jengo Hilo likaachwa kuwa sehemu ya stesheni na museum ili kuvutia utalii. (Hii nayo ni topic pekee ya historical sites preservation na strategic urban planning)

Baadhi yenu mtauliza maswali mengi kuhusu Ikulu na Gymkhana kuhamishwa nk. Kwanini Gymkhana isiende Kigamboni au mbele zaidi?
Na Ikulu si ipo Dodoma? Hamuoni kuwa mmepitwa na wakati kun'gan'gania pale ilipo kila siku panaingiliana na shughuli za wananchi kwa vin'gora na maofisi, mahakama, mahoteli, daladala na wapitanjia tu? Yaani utadhani kuna hatari fulani eneo lile! Kumbe ni ofisi na makazi ya Mkuu wa Nchi! Kwanini asitupishe? ( Hii nayo ni topic pekee ya kupunguza gharama za maintenance za Ikulu mbilimbili. Ni ufahari usio wa lazima.) Fedha itakayo patikana kwa kiingilio cha "Ikulu Museum" ingetumika kuiendeshea. Vile vile ikiwa na sehemu za kukodi kwa mikutano na huduma za restaurant nk.

Kuwenui wabunifu zaidi, hakuna soko la samaki la "kimataifa" pale, ni uchafu mtupu!
Mkifanya nilivyosema hapa juu na kushirikisha wataalamu haswa wa waterfront planning and development, eneo lile litakuwa kivutio cha kimataifa kweli! (Kama Rais SSH na msafara wake walifika au wangefika Pier 39, San Francisco alipokwenda California wangejua ninachosema.)

Kwahiyo mamlaka za Jiji la Dar es Salaam na Serikali kuu pamoja na wizara na wadau husika wakae pamoja na kuunda chombo kitakachohusika na project ya "DAR WATERFRONT REDEVELOPMENT AND KIGAMBONI TUNNEL, MASTER PLAN".

Nashauri alternative approaches kama ifuatavyo:

1. Apatikane msanifu ujenzi maarufu wa kimataifa kutoka Israel, USA, UK, au Canada, awe mshauri mkuu wa project. Ingawa sio lazima, vema akisaidiana na wataalamu wetu kama wapo.

2. Tutangaze 'project design competition' kwa level ya kimataifa na zawadi nono ili tupate proposal kadhaa toka wataalamu wa kimataifa. Kwa njia hii tutapata mawazo na solution kadha wa kadha zitakazopanua uelewa wa wataalamu wetu katika miradi ya aina hii. Hatuwezi kuwaachia akina Amos Makala na Jiji tu kwenye project kama hii, wataleta Coco beach ingine!

3. Tukiwa serious mradi huu utapata support ya wawekezaji wa ndani na nje ya Tz kwasababu utafungua new business opportunities kwa hoteli na biashara nyingine na kupanua ajira. Uboreshaji wa mazingira utavutia watalii na shughuli au fulsa mpya za kiuchumi Kigamboni na maeneo yote ya jiji.

Tumejaza magorofa marefu pale waterfront yoote, mengi ni maofisi ya Serikali iliyohamia Dodoma! Wakati wangeachia maeneo yote haya yangegeuzwa kuwa sehemu za biashara na vivutio vya utalii!

Kama ilivyo tuna Ikulu mbilimbili, na wizara za serikali nazo zina ofisi mbilimbili Dom na Dar, Za nini? Kiuhalisia Tz tuna makao makuu mawili ya Serikali! Huu ni ubadhirifu wa fedha za walipakodi! Kwanini tuendelee kukamuana matozo wakati vyanzo mbadala vya mapato tunavichezea?

Mamlaka husika za Jiji na Serikali pitieni ramani ya mwambao wote wa bahari kuanzia stesheni ya boti za Zanzibar mpaka Gymkhana na (Aga Khan hospital) na orodha ya majengo yenu eneo lote la waterfront yatakayopisha mradi huu. Kama vipi muyapige 'X' kabisa! Yaani yaingizwe kwenye redevelopment plan hii. Vinginevyo tutaendelea kudanganyana kwamba Dar ni jiji la kisasa wakati sivyo.

Najua Aga Khan hospital ni private property, sio rahisi kuhamishwa, lakini ni rahisi kuigeuza hoteli ikabaki kuwa yao ili wapewe eneo jingine wajenge hospitali kubwa kama inavyosemekana walikuwa waijenge Arusha.

Msongamano wa watu kwenye ferry boat hauleti picha nzuri na salama ya Jiji la kisasa!

Soko la samaki la feri halina hadhi ya muonekano, usafi, na mazingira kimataifa badala yake linaharibu mandhari ya eneo lote!

Kule n'gambo Kivukoni college zamani si ilikuwa hoteli? Isogezwe mbele kupisha project hii eneo hilo.

Ikulu haitakiwi kuwepo pale ni pafinyu na inaingiliana na traffic circulation eneo lile. Lakini ni hatari kwa wapitanjia kutokana na ulinzi wake na misafara kwenda na kurudi ya wakubwa.

Hospitali za Ocean road na Aga Khan zihame ili pawe na Sea front hotels and restaurants za kimataifa. Tutumie ocean view kwa WATALII badala ya WAGONJWA. Yaani mnataka watalii nao waende Coco beach!

Hii ni mifano tu ya jinsi ya kubadili sura ya jiji na maeneo haya ili yaendane na matumizi bora na sahihi ya fukwe zetu.

ULINZI, USAFI, USTAARABU NA UKARIMU.
Mambo haya manne yafanyiwe kazi ili sura ya Jiji la Dar ipande hadhi kimataifa. Solution mojawapo ni kupunguza kabisa msongamano CBD kwa kuboresha usafiri kwenda na kurudi toka maeneo yote pamoja na Kigamboni.

Zamani tulikuwa na taa za barabarani kuwezesha watu kwenda mjini kuvijnjari usiku. Sasahivi ni hatari kuwa town na fukweni usiku. Kwanza maeneo yote ni maofisi ya Serikali, mahakama na mahospitali. Usiku kuko giza na kimya kama makaburini au makanisani!

Tuwe wabunifu na wakarimu kwa fikra mbadala. Jeshi la polisi liboreshwe kifikra ili wenyeji na wageni wajisikie huru na salama jijini usiku na mchana. Mtake msitake panyarodi ni matokeo ya police failure, full stop!

KWAHIYO TUSEME: "KAZI IANZE"!
 
Ushauri mzuri ila hao uliowapa sidhani kama watakuelewa. Sio karne hii labda ijayo ya vitukuu vyetu. Kuhamisha Ikulu? Ocean Road hospt?
Ufujaji wa pesa imekuwani style ya maisha ya wanaotungoza.
Kujenga na kubomoa ndo zetu.
Wacha tozo ziendelee
 
Una mawazo mazuri sana lakini humu humu watakuja kukupinga kabla hata ujumbe haujafika kwa wahusika.
Lol
 
Hebu jengeni mabwawa watu wafanye kilimo cha umwagiliaji
Wekezeni pesa zaidi kwenye sekta
Ya kilimo.....
Watu wazalishe,export ya mazao ifanyike
Haya mambo kujenga ma tunnel,blhblh syo lazima sana

Ova
 
Good idea ila vilaza wetu sioni wakifanya hiyo kitu
 
Pale ni njia ya meli za ukubwa tofauti, hilo daraja ujenzi wake labda liwe la kufunga na kufungua pindi meli kubwa zikija.
Sasa ghalama yake siyo ya nchi hii.
Vitu vyote ulivyosema vihamishwe (ikiwemo ikulu) hapa kigamboni kuna uspecial gani kwani?
Kuna kipi cha kuifanya serikali iharibu hela kiasi hicho?
 
Ili muione daslama yenu kama ulaya wekezeni nguvu za maendeleo mikoani na vijijini...vinginevyo hakuna jipya
 
Hebu jengeni mabwawa watu wafanye kilimo cha umwagiliaji
Wekezeni pesa zaidi kwenye sekta
Ya kilimo.....
Watu wazalishe,export ya mazao ifanyike
Haya mambo kujenga ma tunnel,blhblh syo lazima sana

Ova
Ukiwa madarakani uwezo wa kufikiri unapungua ukitoka unaongezeka
 
Ideas zipo nyingi Sana shida wananchi hatushirikishwi juu ya matumizi ya kodi zetu tunashirikishwa kwenye ulipaji wa madeni tu.
 
Kuna wataalam maisha yao baada ya shule wameishi ughaibuni wamekuja umri umeenda wakaingia kwenye system bahati ni bahati, pamoja na exposers na experiences za za ughaibuni lakini mambo bado kama nchi imefungwa 2015/2021
 
Inawezekana kujenga daraja jingine la kigamboni linaanzia pembeni mwa bahari usawa wa busta ya NBC posta ya zamani linaendelea kupanda juu linaenda kushukia lango la kuingia chuo cha Mwalimu Nyerere. Meli zote zinapita Chini magari juu.
 
Pale ni njia ya meli za ukubwa tofauti, hilo daraja ujenzi wake labda liwe la kufunga na kufungua pindi meli kubwa zikija.
Sasa ghalama yake siyo ya nchi hii.
Vitu vyote ulivyosema vihamishwe (ikiwemo ikulu) hapa kigamboni kuna uspecial gani kwani?
Kuna kipi cha kuifanya serikali iharibu hela kiasi hicho?
Linainuka kuanzia NBC garden na kushuka lango la kuingia kambi ya jeshi stand ya zamani ya magari meli zote urefu wowote zinapita Chini ya daraja. La kufungua hapa umeme wetu hautabiriki pili system za kufungua zikifeli means meli hazitoki au kuingia ni mbaya kwa uchumi tutalimwa faini na wamiliki
 
Pale ni njia ya meli za ukubwa tofauti, hilo daraja ujenzi wake labda liwe la kufunga na kufungua pindi meli kubwa zikija.
Sasa ghalama yake siyo ya nchi hii.
Vitu vyote ulivyosema vihamishwe (ikiwemo ikulu) hapa kigamboni kuna uspecial gani kwani?
Kuna kipi cha kuifanya serikali iharibu hela kiasi hicho?
TUNNEL sio daraja.
 
Wazo zuri. Tunnel inaweza kujengwa na kutokea Gymkhana bila kuhamishs chochote.
 
Hoja zako ni nzuri, zinaonesha you have a privilege of being exposed to developed countries, lakini zinaacha mianya ya kuboresha mfano
Kwanza, daraja la Nyerere ni bora pale lilipojengwa kuanzia Vijibweni kuja Kurasini ili kuleta dispersion ya wanaotoka Kigamboni wote wasishukie Kivukoni au Gymkhana kama unavyopendekeza maana italeta unnecessary congestion. Mfano mtu anayetaka kuelekea Posta anatenganishwa vizuri na yule aendaye Kariakoo.
Pili suala la waterfront management, hizi hoteli za ufukweni zilizopo bado hazitumiki to capacity. Hata Kama tunapanga miaka 50 ijayo. Mfano zile twin towers na Mwalimu Nyerere Foundation towers could attract hotel investment if demand is there and it's worth doing so, but even occupancy rate is very low.
Tatu, Aga Khan labda umesahau pia Ocean Road hospitals kuwa relocated. Hapa unachamganya mambo, unaposema lengo ni kuvutia utalii lakini hujatambua kuhusu medical tourism. Unajua India wana advanced medical tourism na players kwa Tanzanian market ni akina Apollo hospital?
Tano, nchi haina ikulu mbili za Dar na Dom tu...ambazo unaita ni ufahari. Nchi ina ikulu ndogo katika kila makao makuu ya mkoa. Unapobadilisha matumizi ya ikulu ya Dar unazalisha hitajio la kujenga ikulu nyingine.
Sita, try to have a big picture of Dar, it is not only restricted to Ilala CBD.
Thank you.
 
Ushauri mzuri ila hao uliowapa sidhani kama watakuelewa. Sio karne hii labda ijayo ya vitukuu vyetu. Kuhamisha Ikulu? Ocean Road hospt?
Ufujaji wa pesa imekuwani style ya maisha ya wanaotungoza.
Kujenga na kubomoa ndo zetu.
Wacha tozo ziendelee
CCM inatuchelewesha sana na bado tunaikumbatia, watanzania ni wazito sana kupenda maendeleo kwani tumezoea maisha ya babu zetu ya robo kilo na robo mkate.
 
CCM inatuchelewesha sana na bado tunaikumbatia, watanzania ni wazito sana kupenda maendeleo kwani tumezoea maisha ya babu zetu ya robo kilo na robo mkate.
Acheni kauli zenu za uchungu. Kwani mangapi ccm inaendelea kuyafanya? Ina maana hamuyaoni. Mbona inafanya makubwa tu
 
Back
Top Bottom