Dar: Nyumba zaidi ya 500 zimezingirwa na Maji ya Mvua eneo la Kigogo

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,120
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule amesema Mvua zilizonyesha Novemba 12, 2023 zimesababisha uharibufu kwenye nyumba takriban 500 katika eneo la Kigogo kutokana na Maji kujaa kwenye Mto Msimbazi.

DC Mtambule amesema, nyumba za eneo hilo zimezingirwa na kiasi kikubwa cha Maji ambapo kwa sasa jitihada Mamlaka za Uokoaji ikiwemo Jeshi la Zimamoto ziko eneo la tukio kwaajili ya kushughulikia suala hilo.

Pia, Mvua hizo zilizonyesha kwa zaidi ya saa 10 katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam zimesababisha madhara kwenye Miundombinu muhimu ikiwa pamoja na Shule ya Msingi Michael Urio ambayo imezingirwa na Maji.
 
Wakiambiwa wasijenge kwenye mkondo wa maji hawaelewi
Wanataka viwanja vya laki tatu tatu😂wapambane na hali yao
Hakuna kutoa msaada,wahame huko mabondeni
 
Asili ya maeneo hayo ni bonde lenye ukanda wa maji...poleni ila muwe mnawaskiliza TMA..
 
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Saad Mtambule amesema Mvua zilizonyesha Novemba 12, 2023 zimesababisha uharibufu kwenye nyumba takriban 500 katika eneo la Kigogo kutokana na Maji kujaa kwenye Mto Msimbazi.

DC Mtambule amesema, nyumba za eneo hilo zimezingirwa na kiasi kikubwa cha Maji ambapo kwa sasa jitihada Mamlaka za Uokoaji ikiwemo Jeshi la Zimamoto ziko eneo la tukio kwaajili ya kushughulikia suala hilo.

Pia, Mvua hizo zilizonyesha kwa zaidi ya saa 10 katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam zimesababisha madhara kwenye Miundombinu muhimu ikiwa pamoja na Shule ya Msingi Michael Urio ambayo imezingirwa na Maji.
Weka picha ya hizo nyumba 500
 
Mkuu uzi wako una matumizi mabaya ya neno nyumba. Balada yake ulipaswa kutumia neno Makazi.

Elewa neno nyumba.
 
Back
Top Bottom