DAR LUX yadhalilisha abiria wake

Najimunisa DUME LA MBEGU. Barabara toka ikiwa ya vumbi kampuni ilitupenda na kutupa huduma safi mpaka imewekwa lami nayo imeendelea kutoa huduma!!
Hatutatupa mbachao kwa msala upitao.
Ya nini kutema BigG kwa karanga za kuonjeshwa?
Basi endelea kupanda wewe ila mimi hunishawishi...
 
Dar Mwanza wanageuzaje? Au wakifika usiku asubuhi wanageuza au wakifika usiku huo huo wanageuza?
 
Hapa naona umetumia Biology na chemistry kwenye hitimisho lako.
Yaani gari ikipumzika siku moja halafu ndio ifanye safari inaondoa uwezekano wa kuanguka!?
Physics inakataa!!!!!


wewe kweli hujui basi linapokuwa mwanza au mwanza maana yake madereva pamoja na wahudumu wanapata muda wa kupumzika kwa ajili ya safari ya siku inayofuata. inamaana hujui hata kuwa basi halianguki ila linaangushwa? basi bila dereva linatembea? du!
 
Kitu kisichowezekana sababu safari ya Dar-Mwanza ni ndefu sana
 
Basi endelea kupanda wewe ila mimi hunishawishi...
Ulijaribu kutushawishi kuwa Mabasi ya Najmunisa ni mabaya nimekujibu sawasawa na kauli yako mbovu na nimekupa best reason ever.
Imekupasa uwe na adabu.
 
Dar lux bana wana huduma nzuri sana yaani kama wao hawajaza bus zingine zinangoja kwanza na hata ikijaza utakuta mabus mengine wanaomba agent wao akae kwenye ofisi za dar lux ili kama wakija na wakikuta dar lux imejaa basi ndo watakata kwenye bus lingine......mtoa mada hizo ni figisu zako tu
 
Kuna mabasi ya LIM SAFARI NI VIMEO KABISA USIJARIBU KABISA KUPANDA KILA KUKICHA YANALALA NJIANI
 
Kama unajamaa yako anafanya kazi hapo mdadisi atakuibia siri, mm nimewapa habari mchukue tafadhali na mamlaka husika ziwe alerted maana mnaona vyema kugawiwa pipi badala usalama wa maisha ktk safari
 
Basi au gari haliangushwi, narudia haliangushwi, bali LINAANGUKA.
Ili uliangushe umepaswa kuwa nje ya basi husika u apply force against the said object.
Unaonekana shuleni ulikuwa unakaba waalimu wewe.
Biniadamu anapaswa kulala masaa mangapi, wanaanza safari saa ngapi na wanatakiwa kulala ikifika saa ngapi.
Usitake kutuambukiza ujinga!!!
Umaanishe eti uingie kazini leo kesho upumzike kwa kuwa unafanya kazi kwenye kiwanda cha nondo!!! Hiyo ndiyo kazi yake, tena wako wawili, wanapokezana, hawapaswi kuendesha kupita 80kph.
Udundulizaji wa abiria ndio kigezo cha kulaza bus!! Kinyume chake linatakiwa lizunguke lilipe mkopo.
 
Vitu ambavyo sio realistic. Hata Dar-Kilimanjaro huwezi kwenda na kigeuza.
Kilimanjaro mbali sana, hata dar -same bado itakua ngumu!! Mleta mada sijui ni umbea tu au ana lengo zuri ila tatizo uandishi
 
Dar lux ni kampuni nzuri mmeanza kulipwa ili waonekane hovyo na kampuni zenu..,
 
hainiingii akilini yaani Basi iende siku hiyo hiyo nà kugeuza labda unamaanisha yale ya dar-moro
 
Huyu jamaa inaelekea wakati anaandika nae alikuwa amesinzia......!yani yeye amehadithiwa akabeba na kuleta hapa bila kuongezea za kwake....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…