Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,473
- 13,624
Kuhamia Dodoma kuna faida ya uongozi wa serikali kujiona kuwa wanalo jukumu la kuitazama nchi nzima kwa mapana yake na sio kuishia kuishi maisha ya ufahari yaliyozoeleka hapa Dar.
Tanzania inayo mikoa mingi ambayo bado haijafunguka katika suala la uwekezaji. Pia ni gharama ndogo sana kwa watu kutoka kona ya nchi kama kule Rukwa, Mtwara na Kagera, kuweza kufika Dodoma na kupata huduma za kiserikali kuliko kufunga safari ndefu ya kulitafuta jiji la Dar.
Dodoma panafikika kiurahisi zaidi kulinganisha na Dar. Halafu keki ya taifa ni lazima iwafikie wengi kwa maana ya mtawanyiko wa rasilimali unaotenda haki kwa kila anayejivunia kuitwa mtanzania.
Tanzania inayo mikoa mingi ambayo bado haijafunguka katika suala la uwekezaji. Pia ni gharama ndogo sana kwa watu kutoka kona ya nchi kama kule Rukwa, Mtwara na Kagera, kuweza kufika Dodoma na kupata huduma za kiserikali kuliko kufunga safari ndefu ya kulitafuta jiji la Dar.
Dodoma panafikika kiurahisi zaidi kulinganisha na Dar. Halafu keki ya taifa ni lazima iwafikie wengi kwa maana ya mtawanyiko wa rasilimali unaotenda haki kwa kila anayejivunia kuitwa mtanzania.