Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya ni majiji yanayojengwa holela, si salama kwa kuishi na yaliyokosa mvu

Manelezu

JF-Expert Member
Feb 6, 2015
1,908
2,774
Miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya imejengwa bila kufuata ramani na idadi kubwa ya wakazi katika majiji haya wanaishi kwenye maeneo yasiyopimwa. Miji yote hii haina maeneo makubwa ya wazi ya kupumzika watu ?City Parks?. Mwaka 1985 Botha aliwahi kusema ?Pretoria has been made by the white mind for the white man? hii ilionyesha kwamba watu weusi si watu wanaoweza kuwa na mipango mizuri na endelevu. Kwa wale waliobahatika kutembelea nchi za wenzetu miji yao imepangwa vizuri na ni mipango ya mda mrefu sana. Maeneo kama bonde la msimbazi lilitakiwa lisijengwe toka zamani, kwanini tulishindwa kusimamia?

Jiji la Mwanza limejengwa holela milimani halina hata mvuto, Tuseme maeneo haya ya milimani yamejengwa holela bila idara ya mipango miji kuzuia ujenzi holela. Kulingana na report za UN-Habitat watu wanaendelea kuongezeka mijini na ndio yatakuwa makazi ya watu wengi , tunaomba serikali iunde chombo maalumu cha wataalam kitakachosimamia mipango miji na tuwe na bajeti ya kutosha kupima maeneo mengi zaidi ili watu wajenge maeneo yaliyopimwa.
 
Miji mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya imejengwa bila kufuata ramani na idadi kubwa ya wakazi katika majiji haya wanaishi kwenye maeneo yasiyopimwa. Miji yote hii haina maeneo makubwa ya wazi ya kupumzika watu ?City Parks?. Mwaka 1985 Botha aliwahi kusema ?Pretoria has been made by the white mind for the white man? hii ilionyesha kwamba watu weusi si watu wanaoweza kuwa na mipango mizuri na endelevu. Kwa wale waliobahatika kutembelea nchi za wenzetu miji yao imepangwa vizuri na ni mipango ya mda mrefu sana. Maeneo kama bonde la msimbazi lilitakiwa lisijengwe toka zamani, kwanini tulishindwa kusimamia?

Jiji la Mwanza limejengwa holela milimani halina hata mvuto, Tuseme maeneo haya ya milimani yamejengwa holela bila idara ya mipango miji kuzuia ujenzi holela. Kulingana na report za UN-Habitat watu wanaendelea kuongezeka mijini na ndio yatakuwa makazi ya watu wengi , tunaomba serikali iunde chombo maalumu cha wataalam kitakachosimamia mipango miji na tuwe na bajeti ya kutosha kupima maeneo mengi zaidi ili watu wajenge maeneo yaliyopimwa.

Umeandika point ndugu! Hata mimi napendekeza kuunda "Mamlaka za ukuzaji Miji/ Majiji kila mkoa kwa halimashauri zimefeli.
 
lukuvi keshasema kila mwenyekiti wa mtaa atapewa nakala ya mpango wa makazi katika eneo lake. labda itasaisia!
 
Mleta mada wewe unaishi mkoa gani uliopangwa vizuri?

Itakua Dodoma, angalau umepangiliwa. Lakini pia Mtwara nao huwez kujenga nyumba ya kudumu pasipopimwa, labda ujenge ya udongo ili iwe rahisi kuvunja.
 
ivi brasil milimani kule kwenye mji mkuu wao reo kumepimwa????? nadhani kwa mwanza nimaboresho tu yanahitajika!!! kule milimani kupatikane barabara za lami ama za mawe kupanda na kushuka huko milimani na huduma muhim za kijamii!! kwa dar - es salaam nikubomoatu!!! hamna namna nyingine
 
Arusha ndio inatia kinyaa,yani manispaa kulipopimwa ni njiro tu.Cha ajabu zaidi uko mianzini mataa ukipanda tu juu kidogo unakutana na nyumba za tope!!!
 
Hata Kama katibu mtendaji au katibu kata atapewa lakini ianzie na uwepo wa mamlaka husiki na hizo master plan na elimu kwa raia ni muhimu.
 
Brazil inatuhusu vp sisi? Vunja zote zile za milimani zitasababisha maporomoko
ivi brasil milimani kule kwenye mji mkuu wao reo kumepimwa????? nadhani kwa mwanza nimaboresho tu yanahitajika!!! kule milimani kupatikane barabara za lami ama za mawe kupanda na kushuka huko milimani na huduma muhim za kijamii!! kwa dar - es salaam nikubomoatu!!! hamna namna nyingine
 
ivi brasil milimani kule kwenye mji mkuu wao reo kumepimwa????? nadhani kwa mwanza nimaboresho tu yanahitajika!!! kule milimani kupatikane barabara za lami ama za mawe kupanda na kushuka huko milimani na huduma muhim za kijamii!! kwa dar - es salaam nikubomoatu!!! hamna namna nyingine

Mji mkuu wa Brazil sio reo mkuu ni Sao Paulo
 
Arusha ndio inatia kinyaa,yani manispaa kulipopimwa ni njiro tu.Cha ajabu zaidi uko mianzini mataa ukipanda tu juu kidogo unakutana na nyumba za tope!!!
Mkuu miji yetu kinyaa. .I wonder we call them cities
 
Back
Top Bottom