Dar es salaam Dar es salaam....Tanzanians needs your Support!!!!

meddie

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
434
125
Hii ndio capital city yetu lakini inashagaza na kutuangusha sana;
  • Uchafu
  • Foleni; (mwendo wa kilomita 1 unakwenda masaa3). Watu tuliiii – kisa amani!!
  • Barabara mbovu na chafu……...tena ktk maeneo wanakoishi “so called civilized community”
  • Watu wanalipuliwa na kufa kwa mabomu -hakuna maelezo wala uwajibikaji. Watu tuliiii – kisa amani!!
  • Mgao wa umeme masaa 24!! Watu tuliiii – kisa amani!!
  • Vingora kila wakati!! Mnasimama masaa eti kiongozi anapita (hujui anatoka wapi na kwa lipi hasa!)


  • Ukiwa Dar utaona msafara wa magari asubuhi yakienda taratibu kuelekea mjini, jioni msafala unatoka mjini kuelekea Bunju, Mbezi, ruvu, mbagala kuu…. . Mjini wahindi na waarabu kibao lakini kwenye msululu wa magari jioni na asubuhi huwaoni! Hayo ni magari acha wanaofuata reli!! Haya ndiyo maisha siku neda siku rudi.


  • Ikija wakati wa uchaguzi utaona magari yamepambwa kijani, watu wamevaa t-shirt, kofia, kanga wanafuraha kama hawana akili mzuri!! Wanasikiliza mtu akiwaeleza upuuzi kana kwamba ukweli wa maisha yanayowakabili wameyasau/ama hawayaoni. Mkoa huu ndo CCM inajizolea kura kemkem!!!

  • Usiku utaona kila kona mabaa yamefurika hakuna pa kukaa, (utafikiri kuna sherehe furani)! Night activity ni watu kwenda baa tu hakuna jambo jingine!! Utasikia kuna baa mpya imefunguliwa twende…lakini ukifika bia ni ile ile!! Kwenye baa watu wanakaa kwa kustarehe utafikiri hawana hadha yeyote wala haja ya mabadiliko!!

  • Ni mji umesheheni elite wa nchi hii lakini unakosa mchango na msimamo wa dhati inapokuja swala la kuchukua hatua za kuleta mabadiliko ya kweli kisiasa/kiuongozi hapa nchini! Ebu linganisha Dar es Salaam na mikoa kama Arusha, Mbeya, mikoa ya kanda ya Ziwa. Wasomi wengi Dar wanakaa kwanza wanamsikiliza JK anasema nini na wao wanaanza kusupport …aakweli uvunjifu wa amani…aaa udini!!!!

Kwa kuzingatia umuhimu wa Dar es Salaam kama Capital city, kunahaja kubwa ya wana dar kubadilika na kuhamasika kwa ajili ya kuleta mabadiliko nchini. Najua CHADEMA wanayo support kutoka Dar es Salaam, lakini kama ingekuwa katika kiwango kikubwa kama inayotoka mikoani speed ya mabadiliko ingekuwa kubwa zaidi!

DAR ES SALAAM PLEASE COME UP AND COME FOR CHANGE WE NEED!

 
Wanamjua Mbowe na Vog lake la kifahari na club billcanas na wanajua Dr Slaa ana lipwa 7.5 milioni na kodi halipi,wanamjua Haliama Mdee na mambo yale,wanamjua mnyika na harakati za club ambiance! wanaona ni usaniii tu ni bora wafanye kazi zao!
 
wanamjua mbowe na vog lake la kifahari na club billcanas na wanajua dr slaa ana lipwa 7.5 milioni na kodi halipi,wanamjua haliama mdee na mambo yale,wanamjua mnyika na harakati za club ambiance! Wanaona ni usaniii tu ni bora wafanye kazi zao!

not clear!!
 
Wanamjua Mbowe na Vog lake la kifahari na club billcanas na wanajua Dr Slaa ana lipwa 7.5 milioni na kodi halipi,wanamjua Haliama Mdee na mambo yale,wanamjua mnyika na harakati za club ambiance! wanaona ni usaniii tu ni bora wafanye kazi zao!

nahisi na wewe unatoka dar
 
Strategically unapoongelea wakazi wa Dar unaongelea aina kuu tano, wapo wale wenye kazi zao nzuri tu katika private sector, wanalipwa vizuri sana, hawa wanatoka nyumbani saa kumi na nusu alfariji kurudi saa nne na nusu usiku, Tabaka la pili ni watu wanaofanya kazi serikalini, kwenye mawizara na idara mbalimbali, hawa kila wanapoondoka wanawaza kurudi nyumbani na makusanyo mazuri ama ya kuforge vikao, kuomba rushwa au hata kula madili ya kukwapua pesa za umma, Kundi la tatu ni la wafanyabiashara ndogondogo ambao kila siku wanakuwa busy kuwahi feli au kariakoo shimoni kununua mazao, hawa nao wanakuwa busy kuanzia saa kumi alajiri na kukamilika saa nne asubuhi, kundi la nne ni la commuters, madereva na makonda plus wapiga debe na mateja, hawa nao wanawazia hesabu ya tajiri na hela ya kununulia unga, hawa nao wapo busy kweli. Kundi la tano ni la ma opportunists, hawa wapo mission town, madalali wa kila aina wafanya biashara za kila aina, hawa wote wanawaza kujenga kuwa na usafiri na kama wanao basi kuuhudumia.

Sasa watu hawa waliopigika kwa kuwa wakazi wa Dar wengi kuwashawishi kuacha shughuli zao ni vigumu sana na ndiyo maana nawapongeza sana CDM kwa kuuweka pending mji wa Dar, watu hawa doesn't care whos's in IKULU wanachofikiria wao ni kutafuta tu. Ndiyo maana wanabinuliwa na kugalagazwa na oleni na migao ya umeme bado wanasema hewala. Hawataki bugudha kwani wanahofia usalama wa vihamba vyao na engine walizo nazo zinazowatafunia mamilioni ya lita za mafuta kwa mwaka kwenye foleni baabarani.
 
Foleni kitu gan? Dar hatuangaiki na mambo ya watu! Kila mtu kivyake! Nyie huko mikoan as long as hamna cha kufanya, endeleeni tu kuandamana! Sisi tutatuwa tu tunasoma habari zenu!
 
Foleni kitu gan? Dar hatuangaiki na mambo ya watu! Kila mtu kivyake! Nyie huko mikoan as long as hamna cha kufanya, endeleeni tu kuandamana! Sisi tutatuwa tu tunasoma habari zenu!
Wanadanganya wajinga wa mikoani,dar watu wanatafuta pesa kwanza,porojo za CDM hawana time nazo
 
Hii ndio capital city yetu lakini inashagaza na kutuangusha sana;
  • Uchafu
  • Foleni; (mwendo wa kilomita 1 unakwenda masaa3). Watu tuliiii – kisa amani!!
  • Barabara mbovu na chafu……...tena ktk maeneo wanakoishi "so called civilized community"
  • Watu wanalipuliwa na kufa kwa mabomu -hakuna maelezo wala uwajibikaji. Watu tuliiii – kisa amani!!
  • Mgao wa umeme masaa 24!! Watu tuliiii – kisa amani!!
  • Vingora kila wakati!! Mnasimama masaa eti kiongozi anapita (hujui anatoka wapi na kwa lipi hasa!)


  • Ukiwa Dar utaona msafara wa magari asubuhi yakienda taratibu kuelekea mjini, jioni msafala unatoka mjini kuelekea Bunju, Mbezi, ruvu, mbagala kuu…. . Mjini wahindi na waarabu kibao lakini kwenye msululu wa magari jioni na asubuhi huwaoni! Hayo ni magari acha wanaofuata reli!! Haya ndiyo maisha siku neda siku rudi.


  • Ikija wakati wa uchaguzi utaona magari yamepambwa kijani, watu wamevaa t-shirt, kofia, kanga wanafuraha kama hawana akili mzuri!! Wanasikiliza mtu akiwaeleza upuuzi kana kwamba ukweli wa maisha yanayowakabili wameyasau/ama hawayaoni. Mkoa huu ndo CCM inajizolea kura kemkem!!!

  • Usiku utaona kila kona mabaa yamefurika hakuna pa kukaa, (utafikiri kuna sherehe furani)! Night activity ni watu kwenda baa tu hakuna jambo jingine!! Utasikia kuna baa mpya imefunguliwa twende…lakini ukifika bia ni ile ile!! Kwenye baa watu wanakaa kwa kustarehe utafikiri hawana hadha yeyote wala haja ya mabadiliko!!

  • Ni mji umesheheni elite wa nchi hii lakini unakosa mchango na msimamo wa dhati inapokuja swala la kuchukua hatua za kuleta mabadiliko ya kweli kisiasa/kiuongozi hapa nchini! Ebu linganisha Dar es Salaam na mikoa kama Arusha, Mbeya, mikoa ya kanda ya Ziwa. Wasomi wengi Dar wanakaa kwanza wanamsikiliza JK anasema nini na wao wanaanza kusupport …aakweli uvunjifu wa amani…aaa udini!!!!

Kwa kuzingatia umuhimu wa Dar es Salaam kama Capital city, kunahaja kubwa ya wana dar kubadilika na kuhamasika kwa ajili ya kuleta mabadiliko nchini. Najua CHADEMA wanayo support kutoka Dar es Salaam, lakini kama ingekuwa katika kiwango kikubwa kama inayotoka mikoani speed ya mabadiliko ingekuwa kubwa zaidi!

DAR ES SALAAM PLEASE COME UP AND COME FOR CHANGE WE NEED!
Mkuu hapo kwenye bold naona unajidangaya labda Dar es Salaam Kimara bonyokwa au Kimara temboni, wewe unadhani kwa nini CDM hawataki kuitisha maandamano Dar es Salaam? watu huku hawataki huu upuuzi
 
Back
Top Bottom