Daniel Adrian
JF-Expert Member
- Jan 1, 2019
- 311
- 322
Ndugu zangu habari za saa hizi.
Nimetimiza miezi sita sasa sina kazi. Nimetumia taaluma yangu kutafuta kazi lakini jitihada zangu hazizalishi matumaini. Shida ni kwamba sipo peke yangu nina mtoto ananitegemea.
Nimeamua nijiajiri kama dalali wa nyumba na viwanja. Kiukweli sijawahi kufanya hii kazi lakini waswahili wana msemo wao unasema 'njaa ni mwalimu'. Nipo tayari kupokea maelekezo ya mambo yote ninayopaswa kuyajua kabla ya kufanya hii kazi.
Lakini ikiwa pia kuna dalali anahitaji mtu wa kumsaidia au kushirikiana nae nipo tayari ili nipate uzoefu ninaouhitaji.
Kwa sasa nipo Temeke lakini naweza kufanya kazi hii katika wilaya yoyote ile Dar es salaam.
Madalali wazoefu na wabobezi kwenye hii kazi naombeni muongozo wenu (au hata kampani mkipenda) ili nami niijue hii kazi. Namie mkono wangu uende kinywani badala ya kichwani au shavuni.
Natanguliza shukrani kwa wote watakaonisaidia kwa dhati kabisa.
Nimetimiza miezi sita sasa sina kazi. Nimetumia taaluma yangu kutafuta kazi lakini jitihada zangu hazizalishi matumaini. Shida ni kwamba sipo peke yangu nina mtoto ananitegemea.
Nimeamua nijiajiri kama dalali wa nyumba na viwanja. Kiukweli sijawahi kufanya hii kazi lakini waswahili wana msemo wao unasema 'njaa ni mwalimu'. Nipo tayari kupokea maelekezo ya mambo yote ninayopaswa kuyajua kabla ya kufanya hii kazi.
Lakini ikiwa pia kuna dalali anahitaji mtu wa kumsaidia au kushirikiana nae nipo tayari ili nipate uzoefu ninaouhitaji.
Kwa sasa nipo Temeke lakini naweza kufanya kazi hii katika wilaya yoyote ile Dar es salaam.
Madalali wazoefu na wabobezi kwenye hii kazi naombeni muongozo wenu (au hata kampani mkipenda) ili nami niijue hii kazi. Namie mkono wangu uende kinywani badala ya kichwani au shavuni.
Natanguliza shukrani kwa wote watakaonisaidia kwa dhati kabisa.