Hivi mkuu wa Trafiki tuseme ndiyo hajui kinachotokea siku za Jumatatu kila wiki, mara 52 kwa mwaka katika barabara ya Buguruni-Kwa Nyerere?
Invyoelekea usalama au uchafuzi barabarani katika barabara hiyo wameamua hii ndio siku ya kuwakamua madereva na makonda wa daladala.
Kwa hiyo daladala hizo kwa kutambua hili na kuona serikali imelala na haiwashughulukii wachawi wao zimeamua kutokuganya kazi siku hiyo isipokuwa kwa chache ambayo inayumkinika ni za maaskari wenyewe au za jamaa wa maaskari.
Matokeo yake ni kwamba:
. Wagonjwa barabara hiyo wanaoelekea hospitali za Amana, Magomeni, Mwananyamala na kadhalika wanateseka kupita kiasi,
. Wafanyakazi mbalimbali wanachelewa kazini.
. Walimu wanachelewa madarasani,
Madaktari, manesi na wafanyakazi wengine wa hosopitali wanachelewa mahospitalini,
. Maelfu ya wanafunzi wanachelewa shule,
. mamia ya wafanyabiashara wanaingia hasara kutokana na kuchelewa kuwahi masokoni, migahawani na magengeni na wengine hasara kutokana na kuoza kwa bidhaa zao njiani,
Kwa hakika haya ndiyo maudhi mwananchi wa kawaida anayetumia barabara ya Buguruni-Kwanyerere anayopata kila Jumatatu hapa jiijini.
Ni vyema mkuu wa trafiki na wizara husika ikalishughulikia jambo hili kabla hali haijawa mbaya zaidi.
Invyoelekea usalama au uchafuzi barabarani katika barabara hiyo wameamua hii ndio siku ya kuwakamua madereva na makonda wa daladala.
Kwa hiyo daladala hizo kwa kutambua hili na kuona serikali imelala na haiwashughulukii wachawi wao zimeamua kutokuganya kazi siku hiyo isipokuwa kwa chache ambayo inayumkinika ni za maaskari wenyewe au za jamaa wa maaskari.
Matokeo yake ni kwamba:
. Wagonjwa barabara hiyo wanaoelekea hospitali za Amana, Magomeni, Mwananyamala na kadhalika wanateseka kupita kiasi,
. Wafanyakazi mbalimbali wanachelewa kazini.
. Walimu wanachelewa madarasani,
Madaktari, manesi na wafanyakazi wengine wa hosopitali wanachelewa mahospitalini,
. Maelfu ya wanafunzi wanachelewa shule,
. mamia ya wafanyabiashara wanaingia hasara kutokana na kuchelewa kuwahi masokoni, migahawani na magengeni na wengine hasara kutokana na kuoza kwa bidhaa zao njiani,
Kwa hakika haya ndiyo maudhi mwananchi wa kawaida anayetumia barabara ya Buguruni-Kwanyerere anayopata kila Jumatatu hapa jiijini.
Ni vyema mkuu wa trafiki na wizara husika ikalishughulikia jambo hili kabla hali haijawa mbaya zaidi.