Dah! Mwanangu watakuwa wamemroga aisee

Dah! Mwanangu watakuwa wamemroga aisee

Saa 7 mchana

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2018
Posts
6,500
Reaction score
12,843
Habari zenu wajuzi wa mambo.

Kunamwana angu mmoja nimejuana nae toka 2016 kipindi hicho tulikua nafanya nae kazi pamoja mtaani. Tukaja potezana mimi nikaendelea na ishu zingine, yeye akawa anaendeleza harakati.

Year 2020 nikarudi tena kwenye harakati nilizokua nafanya nae. Mshikaji nilimkuta yupo nje ya reli mambo hayakua mazuri kwake, nikaona isiwetabu nikamuambia tu team up kama zamani. Ikiwa mimi nita-finance kila kitu iliturudi kwenye reli.

Vikao tukawa tunakaa tukiseti mipanga ya nini kifanye mara kadhaa ikiwemo kufungua ofisi na kupeana majukumu ya kila mmoja cha kufanya, ila changamoto iliyokua inaibuka nikuwa pale tu tunapoaachana jamaa alikua hapatikani kwenye simu na akipatikana hapokei sometimes mpaka wiki mbili zinapita jamaa ndio anakuja kupokea simu.

Baadae ya hapo the cycle continues, tunapanga Mipango time ya utekelezaji jamaa haipatikani kwenye simu na kutokupokea. Imekua ivyo since 2020 June - Dec duh nikaona mwana hayupo tayari nikaachana nae hii ilitoea baada ya jamaa kutokupokea simu zangu kwa miezi miwili mfurulizo.

2021 Jan nikawa nimepata ishu nyengine nikahamia mkoa nakuamia mkoa B.

Nimekaa mkoa B For 6 months, bila kucontact na mshikaji. Ila katikati ya mwezi wa 6 nikapata some really potential information ambazo zingeweza kutuboost kwenye ile mishe/harakati. Kwa kuwa yeye yupo mtaa na ofcourse hanamishe to date. Nikaona isiwe mbaya nika-share nae. Nae akasema kuwa iliishu tuipange nyema na inoge inapidi yeye aje mkoa B nilipo.

Bhana wewe napo ikawa ni ishu tena ikawa nakuja siku fulani, siku iyo ikifika jamaa hapokeii simu zinapita hata wiki 3 ndio anapokea.

Nikamtumia nauli, napo hali ikaendelea kuwa vile vile. Chakushangaza ni kuwa jamaa anaequipments za kufanyia harakati zenye thamani zaidi ya millioni 3.8 na vyote hivyo kaviweka ndani mimi sijainvest chochote ila strategies na porojo za kupata wateja tu.

I was wondering kwa kweli , kunasiku nilipata client nikamseti vizuri tu kuwa ofisi zetu zipo mkoa A , kuwa mteja afike mkoa aliopo mshikaji wakutane wa-close the deal. Ila story ikarudi kuwa ileile baada ya mi kumpa contact za mteja tu. Jamaa akawa hapatikani kwenye simu tena as usually. Jamaa Aliachia deal la zaidi ya 2m likapita I was like what!! I didn't believe what happened.

Mwezi huu nilifika mkoa A alipo mshikaji nakukutanana nae. Mshikaji nakutanana nae analia njaa tu yupo kijiwe cha betting akizichambua vyema odds za mechi mbali mbali za afrika na kimataifa, kweli hata out look yake ilikua hainanuru.

Nikamdadisi labda mshikaji anaishu nyengine, wapi hana daily nikushinda betting house. Nikafika hadi kwake equipments nikazikuta zipo tu yani zaidi ya 3.8m imelala ghetto. Mwamba hana habari yupo bize na betting af chakushangaza hata pesa ya betting nayo yakuunga unga.

Before sijaondoka mkoa A, kurudi mkoa B nikakaa vikao na mshikaji jinsi ya kupata chochote kwenye ujuzi tulio nao. Moja ya mkakati ilikua ni kuanzisha ofisi ya mfukoni na mambo mengine.

Jamaa nikamuachia pesa kidogo ya matumizi na vitu baadhi vyakufuatilia ikiwemo muhuri tu, huwezi amini simu azijapokelewa tena mpaka timu hii naandika uzi huu na ni wiki 2 sasa zimepita.

Ase nimeshindwa kuelewa kuwa huyu jamaa anashida gani.

Wataalum wenye analysis nzito za ulozi

Hii imekaaje inawezekana jamaa wakawa wamroga au ni wenge lake binafsi?
 
Duuh hata kama ni athari za betting lakini nafikiri huyu ana tatizo la kiroho anahitaji msaada wengi wanafanya betting lakn sio hadi kufikia kukataa kufanya kazi.

Bt waweza shirikisha hata wengine hiyo ishu.
 
Nafanya kazi na mtu kama huyo mzee jamaa hajawahi ku-keep promise yani ukitaka asije mwambie atoe ahadi ...hatakuja yani haji atakuwe kuna nini ... hata aambiwe kuna million haendi as long as ni ahadi ... hata enda.

Iwe Boss awe nani haendi ... ukitaka atokee msiweke AHADI nyie semeni tu bila ya ahadi ... mkithibutu kuweka AHADI haji atakama atatishiwa kufukuzwa kazi.
 
Habari zenu wajuzi wa mambo.

Kunamwana angu mmoja nimejuana nae toka 2016 kipindi hicho tulikua nafanya nae kazi pamoja mtaani. Tukaja potezana mimi nikaendelea na ishu zingine, yeye akawa anaendeleza harakati.
Inasikitisha sana kwakweli, ila nimefurahishwa na jinsi unavyojitahidi kumpambania kijana mwenzio. That's so manly and impressive. Vijana tunatakiwa kuwa hivi.

Inaonyesha una nia ya dhati kabisa kumsaidia rafikiyo ila kwa mujibu wa maelekezo yako ni wazi kabisa huyo ndugu tayari kashaanguka kwenye Negative/Dark Realm ukute ni mtoto wa kwanza kwao au kuna possibilities ya potential za ndugu zake wakubwa kazibeba yeye ndio maana anaandamwa namna hiyo.

Mimi ningeshauri kua umchukue huyo mtu ukae nae au muishi sehemu moja kisha fanya utaratibu wa kumkomboa na kumrudisha katika msitari. Tafadhali usiwasikilize watakao kushauri uwende kwa fulani sijui akusaidie. Usithubutu kuondoa giza kwa kutumia giza lenyewe washa taaa!!!
 
Nafanya kazi na mtu kama huyo mzee jamaa hajawahi ku-keep promise yani ukitaka asije mwambie atoe ahadi ...hatakuja yani haji atakuwe kuna nini ... hata aambiwe kuna million haendi as long as ni ahadi ... hata enda
Iwe Boss awe nani haendi ... ukitaka atokee msiweke AHADI nyie semeni tu bila ya ahadi ... mkithibutu kuweka AHADI haji atakama atatishiwa kufukuzwa kazi
Kumbe watu kama hawa wapo wengi
 
Mbona inaonekana wewe ndo umelogwa? Kwanini ulazimishe kuteam up na mtu hahitaji ushirika?
Ni kwamba huyo mtu anayeelezea Conscious mind na subconscious mind yake vimewekewa uzio kwa kutumia Dark spells so hazina ushirikiano cha msingi ni kuondoa huo ukingo kwenye mind yake (I call it Clearing cookies and caches)
 
Kuna watu wanasumbuliwa na kukosa "motivation" from within, anakuwa haoni purpose ya maisha yake. Anaona hata nikifanya hiki sawa, hata nisipofanya pia sawa. Hapangi chochote kuhusu future yake anakua yupo yupo tu.

Ataenda hivyo hivyo then ataingia kwenye depression, anahitaji msaada it's more psychological.

Sijui kuhusu kulogwa lakini hii hali inaweza kumtokea mtu ambaye amekuta na disappointment kubwa katika kipindi fulani cha maisha yake. Unahitaji kumpush kwa maneno ya kumtia moyo na kumtia nguvu, Pole yake.
 
Kuna watu wanasumbuliwa na kukosa "motivation" from within, anakuwa haoni purpose ya maisha yake. Anaona hata nikifanya hiki sawa, hata nisipofanya pia sawa. Hapangi chochote kuhusu future yake anakua yupo yupo tu.

Ataenda hivyo hivyo then ataingia kwenye depression, anahitaji msaada it's more psychological.

Sijui kuhusu kulogwa lakini hii hali inaweza kumtokea mtu ambaye amekuta na disappointment kubwa katika kipindi fulani cha maisha yake. Unahitaji kumpush kwa maneno ya kumtia moyo na kumtia nguvu, Pole yake.
Weweeee....

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Wewe hujajua tu, huyo ameona mchango wako wewe si mkubwa kama wake, kiasi wewe utakuwa kama unamu-exploit tu, mashine zake atajua mwenyewe cha kuzifanyia. Hata mimi kuna watu wa design yako huwa wananisumbua sana, mara ooh, ile gari imekaa tu sijui ilete wapi tufanye nini, wakati naona kabisa itaenda kufa au kunitia hasara ya matengenezo, si bora ikae tu..., acheni kusumbua watu bhana..
 
Kuna watu wanasumbuliwa na kukosa "motivation" from within, anakuwa haoni purpose ya maisha yake. Anaona hata nikifanya hiki sawa, hata nisipofanya pia sawa. Hapangi chochote kuhusu future yake anakua yupo yupo tu.

Ataenda hivyo hivyo then ataingia kwenye depression, anahitaji msaada it's more psychological.

Sijui kuhusu kulogwa lakini hii hali inaweza kumtokea mtu ambaye amekuta na disappointment kubwa katika kipindi fulani cha maisha yake. Unahitaji kumpush kwa maneno ya kumtia moyo na kumtia nguvu, Pole yake.
Hilo darsa la saikologia inabidi nimshitukize na liwe na session moja tu. Mana akipewa ahadi ya darsa lazima akache, au session ya pili isitokee kamwe.
 
Back
Top Bottom