Dada zangu kwa nini mnapenda kufanya udukuzi?

Chuda Kashara

JF-Expert Member
Sep 5, 2016
849
554
Wakuu wa baraza amani iwe nanyi.

Leo nawauliza swali hawa dada zetu, kwanini mnapenda kufanya udukuzi?
Wanatumia juhudi kubwa mno ili kupata kumjua mtu wanaokutana naye. Tuseme labda ni mfanyakazi mpya karipoti kazini, wafanyakazi wa kike watafanya juhudi na maarifa ya kila namna ili kumjua mgeni kwa undani zaidi kuliko wale wa kiume.
Lazima watataka kujua fulani anaishi wapi? anaishije, marital status yake, michepuko yake, vitu anavyotumia mfano, simu, gari, mavazi na ukikutana na makonkodi watajua hadi balance uliyonayo bank.Kwa muda mfupi sana wanafanikiwa kujua tabia za mgeni hata kama si za muhimu kwao.

Hili linakwenda sambamba na wanawake kuwa ni wateja wakubwa wa kazi za kipaparazi kama vile ununuzi wa magazeti ya udaku. Hata nyakati ninapoenda night club na rafiki zangu wa kike, tukishaingia ukumbini, mimi najitahidi kuangalia ulipo mlango wa dharura[Tahadhari kama fujo zikivuma], ilipo kaunta na mwishowe palipo na viti tupu vya kukalia. Lakini hawa rafiki zangu[KE] wataanza kuwatizama watu kujua wamevaaje, bonds zao ni za namna gani ili mradi tu kuhakikisha wanawajua watu.
Wakati wakijitahidi kuchunguza mienendo ya tabia za wengine, wao wanazidi kuwa more secretive.Ndio wanazidi kufanya maigizo zaidi ili kuficha rangi zao halisi kwa watu wengine.

Sasa nawauliza nyie kina Dada, ni nini lengo lenu hasa la kufanya udukuzi wa kujua tabia za watu wengine?
 
Sio wanawake tu zamani udukuz ulikua suna kwetu wanawake!!il a saivi nyie ndo mmetuzidi kwa umbea hadi mmefungua shirika la wambea duniani SHIWALADU!!! Pyeee
 
Wanawake nature yetu ni udukuzi sawa

Ila naamini mwenye udukuzi wa kiwango hicho ulichoelezea ni hawana shughuli za msingi za kufanya
Hata mimi nimehamaki kama wewe....wadukuzi wengine ni mameneja.
 
Bora udukuzi wa wanawake kuliko wa wanaume.

Yaan mwanaume akikuangalia tu(kama mgeni ni mwanamke) ujue keshakuvua nguo akilini na kuanza kutalii kwenye mwili wa mhusika.(kama huna hips utakavyochorwa humo sasa)
Wanaume wanaangalia maumbile basi....siyo kama wanawake.
 
Sio wanawake tu zamani udukuz ulikua suna kwetu wanawake!!il a saivi nyie ndo mmetuzidi kwa umbea hadi mmefungua shirika la wambea duniani SHIWALADU!!! Pyeee
Mabadiliko ya nyakati, lakini hayatukatazi kuulizia asilia.
 
Wakuu wa baraza amani iwe nanyi.

Leo nawauliza swali hawa dada zetu, kwanini mnapenda kufanya udukuzi?
Wanatumia juhudi kubwa mno ili kupata kumjua mtu wanaokutana naye. Tuseme labda ni mfanyakazi mpya karipoti kazini, wafanyakazi wa kike watafanya juhudi na maarifa ya kila namna ili kumjua mgeni kwa undani zaidi kuliko wale wa kiume.
Lazima watataka kujua fulani anaishi wapi? anaishije, marital status yake, michepuko yake, vitu anavyotumia mfano, simu, gari, mavazi na ukikutana na makonkodi watajua hadi balance uliyonayo bank.Kwa muda mfupi sana wanafanikiwa kujua tabia za mgeni hata kama si za muhimu kwao.

Hili linakwenda sambamba na wanawake kuwa ni wateja wakubwa wa kazi za kipaparazi kama vile ununuzi wa magazeti ya udaku. Hata nyakati ninapoenda night club na rafiki zangu wa kike, tukishaingia ukumbini, mimi najitahidi kuangalia ulipo mlango wa dharura[Tahadhari kama fujo zikivuma], ilipo kaunta na mwishowe palipo na viti tupu vya kukalia. Lakini hawa rafiki zangu[KE] wataanza kuwatizama watu kujua wamevaaje, bonds zao ni za namna gani ili mradi tu kuhakikisha wanawajua watu.
Wakati wakijitahidi kuchunguza mienendo ya tabia za wengine, wao wanazidi kuwa more secretive.Ndio wanazidi kufanya maigizo zaidi ili kuficha rangi zao halisi kwa watu wengine.

Sasa nawauliza nyie kina Dada, ni nini lengo lenu hasa la kufanya udukuzi wa kujua tabia za watu wengine?
Kweli,umejuaje mkuu???
 
Back
Top Bottom