Dada wa Kazi anahitajika

Dada wa Kazi anahitajika

NAKWEDE

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2007
Posts
27,972
Reaction score
35,192
Ninahitaji dada wa kunifanyia kazi za ndani. Ninaishi Mwanza Wilaya ya Ilemela kata ya Buswelu. Mshahara utakuwa Tshs50,000/ kwa mwezi. Aanatakiwa awe na sifa zifuatazo:

1. Ajue kusoma na kuandika pia matumizi ya simu yale ya msingi eg. kupiga, kupokea na kutumia short message services
2. Awe anajua kupika vyakula vya kawaida tu vya kibantu mfano ugali, wali
3. Awe mkristo mwenye imani ya kiasi, naamanisha asiwe wale wakushinda kanisani au wakuamka usiku na kuanza kuomba kwa sauti kubwa hali ambayo itawanyima watu wengine usingizi
4. Asiwe na mapepo
5. Awe anakula vyakula vyote, asiwe ana bagua mfano hali nyama, maharage au mchicha
6. Asiwe mzururaji kwenye nyumba za watu kupiga soga
7. Awe tayari kufundisha/kufundishwa kwa kuwa hakuna anayejua kila kitu na hakuna ambaye hajui kitu.
8.Awe na "wito" wa usafi.
9. Awe mkarimu wa kiasi, asiwe mtu wa kugawa vitu kwa majirani nikiwa sipo.

MARUPURUPU:
1. Nitamnunulia vipodozi vya kawaida
2. Nitampa pads free kila mwezi
3. Nitamnunulia nguo but mitumba

NB: Sitamchangia kwenye mifuko ya hifadhi za kijamii eg. NSSF

Mawasiliano: 0629 533 764
 
Wadada wa Kazi ni pasua kichwa yaan usisahau kumuombea tu maana
 
Mimi walinisumbua sana hawa wadada wa kazi, wa kwanza nilimtoa iringa, ikifika usiku wa saa sita anapiga yowe, eti bibi yake
hahahahah imebidi nicheke (bold) pole sana ndugu yangu Siasa Basi!
 
Goodmorning sweetheart...

hebu nambie hapa unatafuta dada wa kazi au unamtafutia kaka yako mchumba kijanjajanja??
Nina shida ya dada wa kazi, mbona vigezo ni vya kawaida sana Asprin, hebu visome tena naamini hata wewe unataka upate msaidizi mwenye sifa hizo. Wasumbufu sana, ukimbeba habebeki
 
Mimi walinisumbua sana hawa wadada wa kazi, wa kwanza nilimtoa iringa, ikifika usiku wa saa sita anapiga yowe, eti bibi yake
tehe tehe tehe tehe tehe niliwai kupata mmoja, usiku wa manane nikasikia mayowe kutoka chumbani eti kuna mtu anautoa moyo wake
 
tehe tehe tehe tehe tehe niliwai kupata mmoja, usiku wa manane nikasikia mayowe kutoka chumbani eti kuna mtu anautoa moyo wake
hahaahahahahahahh kwikwi kwikwi jamani acha tucheke kama mazuri vileee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom