sangujoseph
Senior Member
- Nov 30, 2015
- 164
- 184
.
By Sangu Joseph
.
Mxieeeew! Ngoja nianze kwa kumsonya ndugu Mfalme japo nahofia sana Team Kiba kuja kunishambulia, kwa sababu tu ya kuandika mawazo yangu, Ila kiukweli Mfalme Alikiba ni moja ya watu ambao wananiangusha sana, sana, sana.
Kumradhi kumtusi mfalme Ila rejea andiko langu nililoeleza kwanini Harmonize atampita Ali Kiba. Kimsingi nimeshtushwa sana vijana wenye vipaji kama Killy na Cheed kuondoka katika kipindi cha ujenzi wa Label.
Kinachonisikitisha sana unajua tuko katika nyakati ambazo tunawatazama watu 3 (Harmonize, Alikiba na Diamond) tulitarajia kuona Kings Music ikijijenga zaidi kama tunavyoona kwa Konde Boy Harmonize kwa kumuongeza kwa haraka Ibraah TZ ili kuongeza mashambulizi kwenye Uwanja wa Vita.
The same kwa Diamond tunaona anajenga ngome yake WCB kwa kununua silaha mpya aina ya @OfficialZuchu made in Tanzania.
Kwa mfalme Alikiba imekua tofauti kidogo kwa sababu badala ya kujenga ngome, kwake inabomoka na Maaskari waaminifu wanamkimbia na wanavyokimbia hawaelezi cha maana zaidi ya kutuachia vumbi na sisi tukieendelea kuisoma namba.
Unaweza ukasema kwani hii ni mara ya kwanza Msanii kukimbia ndani ya Label mbona hata Diamond ilishamtokea kwa Harmonize na Rich Mavoko, lakini nitakujibu angalia life Span ambayo alikaa Mavoko na Konde Boy unagundua nizaidi miaka 4 acha ile ya kukaa benchini bila kupewa namba.
Kwa kumbukumbu huyu ni Msanii wa tatu kuondoka chini ya usimamizi wa Mfalme ukimuongeza na Young Boy Baraka the Prince na kwa uzoefu wangu wa kufuatilia burudani mara nyingi Msanii akiondoka ndani ya label wengine huwa wanakua na makosa lakini asilimia kubwa huwa wanakua na matarajio ya kuyafikia lakini wanaona management waliyokuwa nayo hawawezi kufikia ndicho ambacho Mimi nahisi Cheed na Killy kimewafanya wametuachia vumbi.
Next post nitaeleza anaposhindwa Ali Kiba mpaka wasanii wachanga wanaondoka katika kipindi kama hichi ambacho walihitaji kukua zaidi, Ila chakumalizia tu Ali Kiba anarudi nyuma hatua wakati wenzake wakijipanga zaidi.
.
INSTA : FB : TWIT : SANGUJOSEPH
.
#KijanaMzalendo #IloveTZ
Sent using Jamii Forums mobile app
By Sangu Joseph
.
Mxieeeew! Ngoja nianze kwa kumsonya ndugu Mfalme japo nahofia sana Team Kiba kuja kunishambulia, kwa sababu tu ya kuandika mawazo yangu, Ila kiukweli Mfalme Alikiba ni moja ya watu ambao wananiangusha sana, sana, sana.
Kumradhi kumtusi mfalme Ila rejea andiko langu nililoeleza kwanini Harmonize atampita Ali Kiba. Kimsingi nimeshtushwa sana vijana wenye vipaji kama Killy na Cheed kuondoka katika kipindi cha ujenzi wa Label.
Kinachonisikitisha sana unajua tuko katika nyakati ambazo tunawatazama watu 3 (Harmonize, Alikiba na Diamond) tulitarajia kuona Kings Music ikijijenga zaidi kama tunavyoona kwa Konde Boy Harmonize kwa kumuongeza kwa haraka Ibraah TZ ili kuongeza mashambulizi kwenye Uwanja wa Vita.
The same kwa Diamond tunaona anajenga ngome yake WCB kwa kununua silaha mpya aina ya @OfficialZuchu made in Tanzania.
Kwa mfalme Alikiba imekua tofauti kidogo kwa sababu badala ya kujenga ngome, kwake inabomoka na Maaskari waaminifu wanamkimbia na wanavyokimbia hawaelezi cha maana zaidi ya kutuachia vumbi na sisi tukieendelea kuisoma namba.
Unaweza ukasema kwani hii ni mara ya kwanza Msanii kukimbia ndani ya Label mbona hata Diamond ilishamtokea kwa Harmonize na Rich Mavoko, lakini nitakujibu angalia life Span ambayo alikaa Mavoko na Konde Boy unagundua nizaidi miaka 4 acha ile ya kukaa benchini bila kupewa namba.
Kwa kumbukumbu huyu ni Msanii wa tatu kuondoka chini ya usimamizi wa Mfalme ukimuongeza na Young Boy Baraka the Prince na kwa uzoefu wangu wa kufuatilia burudani mara nyingi Msanii akiondoka ndani ya label wengine huwa wanakua na makosa lakini asilimia kubwa huwa wanakua na matarajio ya kuyafikia lakini wanaona management waliyokuwa nayo hawawezi kufikia ndicho ambacho Mimi nahisi Cheed na Killy kimewafanya wametuachia vumbi.
Next post nitaeleza anaposhindwa Ali Kiba mpaka wasanii wachanga wanaondoka katika kipindi kama hichi ambacho walihitaji kukua zaidi, Ila chakumalizia tu Ali Kiba anarudi nyuma hatua wakati wenzake wakijipanga zaidi.
.
INSTA : FB : TWIT : SANGUJOSEPH
.
#KijanaMzalendo #IloveTZ
Sent using Jamii Forums mobile app
