Gwalihenzi
JF-Expert Member
- Oct 21, 2011
- 5,125
- 1,301
kwa umri wake angekuwa amestaafu. Huko kwenye siasa hakuna kustaafu. Taabu ni pale anapokuwa hana uwezo wa kuungoza lakini analindwa na mtandao kwa gharama ya uhai wa wawatu.Kwa kiwango chake cha elimu mbona kama si tamaa ya pesa angekuwa wodini akitibu wangojwa badala ya kupiga siasa za maangamizi na sanaa. Big girl, go and save life instead of being abused by stupid politicians. Binti, achana na siasa za ubabaishaji ulinde heshima ya taaluma yako.
ni vizuri ukauliza, ni kivipi hizi special seats zinapatikana na si kukurupuka tu.Kuna mambo yananitatiza kwenye hii CV
Moja.... Kuteuliwa kwenye viti maalum and then naibu waziri ( hii haiji labda kama alipewa huo uviti maalum ili aweze kupewa ulaji wa unaibu waziri, na kama hii ni kweli ina maana kuna mkono wa mtu hapo! Haiwezekani rais from no where aanze mteua mtu kwenye viti maalum na kumweka kwenye unaibu waziri kama hamfahamu, hapa ina maana rais anafahamiana na huyu na ndio maana inakuwa ngumu kuchukua maamuzi dhidi yake.
Ukiangalia vizuri kwenye elimu yake toka 1985 mpaka 1991, yeye alikuwa anafululiza kwenda kusoma tu tena nje ya nchi! Je alikuwa anajilipia au alikuwa analipiwa na serikali? Haiingii akilini mtu aunganishe degree baada ya degree pasipo hata kuja kupractice alichosomea mwanzo( nina imani tukichimba zaidi hapa tutaona kuna walakini kwenye huku kusoma huku).
Mara ya kwanza nilidhani viti maalumu wote ni popompo kumbe kuna wengine wana CV za ukweli!Hongera sana Dr Nkya kwa hilo.Jamani msikurupuke kukashifu mtiririko wa uandishi wa CV kwa kumshambulia muhusika moja kwa moja,hii CV imetoka katika website ya Bunge wala hajaiandika muhusika!Kutaka kujua hilo tembelea website ya bunge uone walivyochakachua CV za watu!!
Acha kutetea UPUMBAVU wewe? Una maana website ya BUNGE ndiyo imechakachua hiyo CV? Mbona CV za baadhi wa wabunge ziko chronologically? Jinsi unavyo post INFO zako kwenye WEBSITE ya Bunge ndivyo zitavyotokea. There is no way information uliyopost ya kwanza iwe ya mwisho au vice versa, and there is room to up date, correct mistakes/errors. Huyu Waziri Dr. Nkya amedhihirisha SIO MAKINI, sidhani kama anaweza kuwa MAKINI na kugundua THE FINE BLUE PRINTS zinazofichwa kwenye mikataba mbalimbali.
Uandishi wa BARUA na CVs unafundishwa kuanzia FORM ONE. Waziri hatakiwi kuandika CV kama mlevi POMBE. It is a shame not only to her but to the government and Tanzanianis as whole kwasaababu wenzetu wa nje wanazisoma hizi CVs.