Makamanda habari za wakati huu..
Nimesikitishwa sana na baadhi ya watu ambao wamekua wakielezea ndivyo sivyo CV ya Mheshimiwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la Vijana la Chama Cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA )
Kulopoka ni uvivu wa kufikiri, tuache kuelezea mambo bila kuwa na ufahamu ama tafiti! Tukumbuke, "No research, no right to speak". Nafahamu ya kuwa miongoni mwetu huenda tuna kiu ya haki kutaka kufahamu ukweli juu ya wasifu wa kiongozi wetu mpya alierithi mikoba toka kwa John Heche, mwenyekiti aliemaliza muda wake. Lakini kiu hii isiwe ni chanzo cha kubuni na kusema tusioyajua kwa kina maana kufanya hivyo si uungwana hata kidogo.
Ukweli Ni Kwamba;
Mhe. PATROBASS, Paschal Katambi amekuwa mwana CHADEMA tangu 2005.
Baada ya kumaliza kidato cha sita alijiunga na Chuo Cha Mtakatifu Agustino na kujikita katika Sheria ngazi ya shahada ya kwanza naya pili katika sharia za UCHUMI.
Amekua mwanachadema mwaminifu tangu masomoni Sekondari, Chuo Kikuu hadi Kazini na kushiriki kazi zote za Chama na hata kushika na pia kushinda nafasi nyingi za uongozi katika kukijenga Chama bila woga kwani anajiamini na anamsimamo katika mambo ya msingi na utetezi wa haki na usawa kwaajili ya CHADEMA na taifa.
Anaaminika na anaheshimu watu wote, Ametumikia nafasi zifuatazo kwa Uaminifu, Uadilifu, tija na manufaa ya wengi toka s/msingi hadi chuo kikuu :- Kilanja, Chuo kikuu Serikali za wanafunzi- m/mkt Tume marekebisho katiba SAUTSO, Katibu Mkuu SAUTSO, MKt Kamati maalumu ya Sheria Umoja wa Marais wa vyuo vikuu Tanzania Aliipinga kisheria na hoja Serikali kuondosha jina la Rais na Waziri vyuo vikuu, Akatetea haki ya kupiga kura wanafunzi 2010 hadi Mahakama kuu akiongoza jopo, Amekuwa Waziri wa Sheria, Mkt Tume ya Uchaguzi SAUTSO.
Kwa CHADEMA Amekua kiongozi tangu 2007 hadi leo katika nafasi mbalimbali za ujenzi na uhamasishaji kukuza Chama bila unafiki wala woga maana hana tabia ya kumuogopa mtu bali kuheshimu kwa kadri ya matakwa ya mila,tamaduni,desturi, sharia, taratibu na kanuni zinavyosema na matakwa ya wengi. Tangu 2007 hadi leo yeye ni kiongozi wa CHADEMA nafasi mbalimbali. Wenye akili na nia njema na chama chetu wanajua
nafasi aliyonayo sasa si ya mzaha,kuuzia sura wala kujifunzia uongozi ni nafasi ya kupanga na kutenda bila woga wala njaa.
Kuhusu kazi aliyokuwa nayo, hata makao makuu na uongozi wajuu CDM wanajua na amekifaa vipi chama na wanachama kwa ujumla. Ni mwanachama asietiliwa hata tone la shaka. Kulazimisha kumhusisha na Diallo ama CCM kwa kigezo alikua anafanya kazi hapo, wenye akili tunajua CHADEMA haina Viwanda, haina Makampuni, Haiongozi Serikali, hivyo wana CHADEMA wasomi na wasio wasomi watafanya kazi popote KWA MUJIBU WA SHERIA na si matakwa ya mwajiri (Ukiwa muislam ukaajiriwa na mkristo haikulazimu ubadili dini kwani haihusiani na itikadi hizo) Tuhukumu watu kwa ukweli na haki si kutumia elimu vibaya kupotosha na kupika maneno, CCM nawashirika wao ipo siku mtakwama na hakuna atakae ishi milele, kina Ghadafi na ubabe wao na uroho wa madaraka walifanya kila njia lakini mwisho ulifika.
Mwisho kabisa nasema, Tujenge hoja tujenge chama.
Na, MWANA WAKATI